-
Mfumo wa THAAD wa Marekani ulioko Israel wafeli kuzuia makombora ya Yemen
May 10, 2025 00:56Kombora lililovurumishwa kutoka Yemen limefika katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel huku mfumo wa ulinzi wa anga wa THAAD wa Marekani ukishindwa tena, na kulazimisha mamilioni ya Wazayuni kukimbilia katika mahandaki wakiwa na hofu na wahka.
-
Abdul-Malik al-Houthi: Umma wa Kiislamu unabeba jukumu la mauaji ya kimbari Gaza
May 09, 2025 07:23Sayyid Abdul-Malik Badr al-Din al-Houthi, Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen ameeleza kuwa, jamii za Kiarabu na Umma wa Kiislamu zinabeba jukumu la msingi la mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza akisisitiza matokeo mabaya ya kutochukua kwao hatua.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Muqawama utaendelea hadi ushindi kamili
May 09, 2025 04:09Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema Muqawama utaendelea hadi ushindi kamili utakapopatikana na kuangamizwa kikamilifu utawala ghasibu na vamizi wa Kizayuni wa Israel.
-
Jeshi la utawala wa Kizayuni lakiri kuwa askari wake wawili wameangamizwa Ghaza
May 09, 2025 03:50Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limekiri kuwa wanajeshi wake wawili wameuawa katika Ukanda wa Ghaza.
-
Ansarullah: Tutavigeuza Jahannam viwanja vya ndege vya Israel
May 08, 2025 23:34Vyombo vya habari vilivyoko karibuni na Ansarullah ya Yemen vimesambaza mkanda wa video unaotishia kulengwa viwanja vya ndege vya utawala ghasibu wa Kizayuni na kuvigeuza Jahannam na harakati hiyo.
-
Israel yaendelea kupata pigo, mashirika makubwa ya ndege yagoma kwenda Tel Aviv
May 08, 2025 23:03Mashambulizi ya Jeshi la Yemen dhidi ya uwanja wa ndege wa Ben Gurion huko Tel Aviv yanaendelea kuutia hasara kubwa utawala wa Kizayuni ikiwa ni pamoja na mashirika mawili maarufu ya British Airways na Air Europa kuendelea kugoma kupeleka ndege zao kwenye uwanja huo wa Israel.
-
Jolani: Hay’at Tahrir al-Sham inafanya mazungumzo na Israel
May 08, 2025 03:34Mkuu wa utawala wa Hay’at Tahrir al-Sham (HTS) unaoongoza nchini Syria amethibitisha habari ya kuwepo mazungumzo "yasiyo ya moja kwa moja" kati ya utawala huo na utawala wa Israel eti kwa lengo la kuzuia kile alichokiita mripuko usioweza kudhibitiwa wa hali ya mambo, wakati huu ambapo Tel Aviv inaendeleza uchokozi wa kijeshi usiokoma dhidi ya Syria.
-
Ansarullah: Mapatano na Marekani hayatazuia mashambulizi ya Yemen dhidi ya Israel
May 07, 2025 09:01Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen imesema kuwa kusitishwa kwa mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen mkabala wa kusitisha mashambulizi dhidi ya meli za kivita za Marekani katika Bahari ya Shamu hakutabadilisha msimamo wa Yemen kuhusu kushambulia Israel.
-
Vyombo vya usalama vya Israel vyaonya kuhusu kupanua vita Ukanda wa Gaza
May 07, 2025 03:02Vyombo vya usalama vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimewatahadharisha viongozi wa utawala huo kwamba kupanuliwa oparsheni za kijeshi katika Ukanda wa Gaza kutapelekea kuuawa mateka wa Kizayuni wanaoshikkiliwa na wanamapambano wa Kipalestina.
-
Hali si hali, mamia ya wanajeshi wa Israel wakamatwa wakitoroka jeshini
May 06, 2025 07:31Wakati jeshi la utawala wa Kizayuni likikaribia kusambaratika kutokaana na uhaba wa wafanyakazi, wimbi la wanajeshi wa Israel wanaokwepa kuhudumu jeshini nalo linazidi kuongezeka hususan kutokana na hofu ya kutumwa kwenye kinamasi cha Ghaza.