-
Yemen: Tumeupiga tena Uwanja wa Ndege wa Israel kwa kombora la Zulfiqar
Jun 03, 2025 03:34Msemaji wa jeshi la Yemen, Meja Jenerali Yahya Saree ametangaza kuwa, usiku wa kuamkia leo Jumanne, jeshi hilo limeupiga tena Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion wa Israel huko Tel Aviv kwa kutumia kombora la balestiki la Zulfiqar.
-
Yemen yataka makampuni ya kigeni yaondoke 'Israel', mashambulizi yatashadidi
Jun 02, 2025 07:52Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Mahdi al-Mashat, ametoa onyo kali kwa makampuni ya kigeni yanayowekeza katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ambazo zimepewa jina bandia la Israel, akibainisha kuwa hatua mpya za kijeshi za Yemen ziko mbioni kuchukuliwa ikiwa uvamizi wa Gaza utaendelea.
-
Hamas: Jinai za Israel Gaza zinashinda uhalifu wa Wanazi
Jun 02, 2025 03:14Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amelaani shambulizi la karibuni la Israel dhidi ya wananchi wa Kipalestina wenye njaa waliouawa shahidi wakiendea chakula cha msaada kusini mwa Gaza, akibainisha kwamba mauaji haya yanatuma ujumbe wa wazi kwa ulimwengu wa Kiislamu kwamba wakati umefika wa kusimama dhidi ya wauaji.
-
Uwanja wa Ben Gurion wapigwa tena kombora la hypersonic
Jun 02, 2025 03:13Jeshi la Yemen limesema kuwa limeanzisha tena operesheni mpya za kulipiza kisasi dhidi ya maeneo yanayolengwa na Israel ndani kabisa ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, ili kukabiliana na jinai na uchokozi unaoendelea dhidi ya Wapalestina wa Gaza.
-
Walowezi zaidi ya 12,000 wavamia msikiti wa al-Aqswa mwezi Mei pekee
Jun 01, 2025 22:48Zaidi ya walowezi 12,000 wa Kizayuni wenye misimamo ya kufurutu ada wamevamia msikiti mtakatifu wa al-Aqswa mwezi Mei pekee uliomalizika na kufanya vitendo vya kichochezi katika eneo hilo takatifu.
-
Hamas yapongeza uamuzi wa Baraza la Jiji la Barcelona kwa kuvunja uhusiano na Israel
Jun 01, 2025 22:48Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imepongeza uamuzi wa Baraza la Jiji la Barcelona la nchini Uhispania la kuvunja uhusiano wa kitaasisi na utawala wa Israel kutokana na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huo wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Wanachama wa genge moja la kigaidi watiwa mbaroni Iraq
Jun 01, 2025 22:38Idara ya Taifa ya Ujasusi ya Iraq imetangaza habari ya kutiwa mbaroni na kusambaritishwa mtandao wa uhalifu uliokuwa na nia ya kufanya operesheni za mauaji na kuvuruga usalama wa umma nchini humo.
-
Tiketi za ndege za kukimbia Israel zawa adimu
Jun 01, 2025 06:39Soko la usafiri wa anga kutoka maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na Wazayuni limekumbwa na mgogoro usio na kifani kutokana na kuendelea mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora ya jeshi la Yemen dhidi ya miundombinu muhimu ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Israel yaua Wapalestina 30 katika vituo vya misaada vya US, Gaza
Jun 01, 2025 03:45Vikosi vya utawala haramu wa Israel vimewamiminia risasi Wapalestina waliokuwa wamekusanyika katika vituo vya kusambaza misaada vinavyoendeshwa na kundi linaloungwa mkono na Marekani kusini na katikati mwa Gaza, na kuua shahidi takriban 30 miongoni mwao huko Rafah, huku Mpalestina mwingine akiuawa shahidi karibu na korido ya Netzarim.
-
Jolani azidi kujikomba kwa Wazayuni, adai Syria, Israel zina maadui wa pamoja!
Jun 01, 2025 03:38Abu Mohammed al-Jolani, Mkuu wa utawala wa Hay’at Tahrir al-Sham (HTS) unaoongoza nchini Syria ameliambia gazeti linalohudumia jumuiya ya Wayahudi huko Damascus kwamba, "ukweli ni kwamba, tuna maadui wa pamoja - na tunaweza kuwa na jukumu kubwa katika usalama wa kikanda."