-
Idadi ya vifo Gaza yafikia 51,240, Israel yaendeleza mashambulizi ya kinyama
Apr 21, 2025 23:31Idadi ya mashahidi wa Palestina waliouawa shahidi kufuatia mashambulio ya kinyama ya utawala ghasibu wa Israel inazidi kuongezeka huku utawala huo haramu ukikithirisha hujuma zake.
-
Makundi yenye silaha Syria yaendelea kufanya uhalifu na kutupa miili kwenye mabonde
Apr 21, 2025 23:30Vyanzo vya ndani vya Syria vimeripoti kuhusu kuendelea jinai zinazofanywa na makundi yenye silaha katika miji mbalimbali ya nchi hiyo na kutelekeza miili ya kwenye mabonde na milima kwa lengo la kuficha jinai zao.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia Israel na meli za kivita za Marekani
Apr 21, 2025 07:22Vikosi vya Jeshi la Yemen vimeendesha msururu wa operesheni kulipiza kisasi kutokana na mashambulizi yanayoendelea ya Marekani katika nchi hiyo ya Kiarabu, vikishambulia ngome muhimu za Isarel katika ardhi zinazikaliwa kwa mabavu pamoja na meli za kivita za Marekani katika Bahari Nyekundu ya Kaskazini na Bahari ya Arabia.
-
Mkuu wa Umoja wa Maulamaa wa Muqawama: Kuitetea Ghaza ni jukumu la Waislamu wote
Apr 21, 2025 03:46Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Muqawama amesema, kuitetea na kuiunga mkono Ghaza ni jukumu la watu wote, na akatoa wito kwa mataifa ya Kiislamu na wanazuoni wa Kiislamu kuwasaidia ndugu zao wanaodhulumiwa huko Palestina na katika Ukanda wa Ghaza, wakati huu ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel unaendeleza jinai zake dhidi yao.
-
Shambulio la anga la Marekani katika mji mkuu wa Yemen laua raia wasiopungua 12, lajeruhi 30
Apr 21, 2025 03:46Marekani imefanya mashambulizi mengine ya anga dhidi ya mji mkuu wa Yemen, Sana’a na kuwaua shahidi raia wasiopungua 12 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 30.
-
Hilali Nyekundu ya Palestina: Ripoti ya Israel ya mauaji ya wahudumu wa tiba 'imejaa uwongo'
Apr 21, 2025 03:45Shirika la Hilali Nyekundu la Palestina limekanusha vikali ripoti ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu mauaji liliyofanya mwezi uliopita ya zaidi ya wafanyakazi 15 wahudumu wa sekta ya tiba huko Ghaza, ambayo utawala huo umedai waliuawa kimakosa.
-
Muqawama Iraq: Huenda kongozi wa Hayat Tahrir al-Sham ya Syria akamatwa akija Baghdad
Apr 20, 2025 22:55Kiongozi wa kundi la Muqawama na kupambana na ugaidi la Asa’ib Ahl al-Haq nchini Iraq ameonya kwamba, anayejiita rais wa Syria Abu Mohammed al-Jolani anaweza kukamatwa atakapowasili Baghdad, kutokana na kuwepo hati ya kukamatwa kwake.
-
Misafara ya askari, silaha za Marekani yaingia Ain al-Asad, Iraq ikitokea Syria
Apr 20, 2025 22:54Jeshi la Marekani limeripotiwa kutuma misafara mingi ya malori yaliyobeba wanajeshi, silaha na zana kivita, pamoja na suhula za kilojistiki kutoka ndani kabisa ya Syria hadi katika kambi kubwa ya anga ya Ain al-Asad katika jimbo la Anbar nchini Iraq, ambayo ina wanajeshi na wakufunzi wa Marekani.
-
Qatar yalaani mpango wa Wazayuni wa kubomoa Msikiti wa Al-Aqswa
Apr 20, 2025 22:52Qatar imelaani vikali mpango wa taasisi za Wazayuni wenye misimamo mikali ya kubomoa msikiti wa Al-Aqswa katika mji wa Baytul-Muqaddas.
-
Wapalestina 18 wauawa shahidi katika unyama mwingine wa Israel
Apr 20, 2025 08:38Mashambulizi ya leo ya utawala haramu wa Israel katika maeneo mbalimbali ya Gaza yamesababisha vifo vya watu 18 na wengi kujeruhiwa.