-
Palestina: Walowezi wa Kizayuni wenye misimamo ya chuki wanachochea Msikiti wa Al-Aqsa uripuliwe
Apr 20, 2025 02:03Wizara ya Mambo ya Nje ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina imetoa indhari kutokana na kuongezeka uchochezi unaofanywa na makundi ya walowezi wa Kizayuni wa mrengo wa kulia wanaotaka kubomolewa Msikiti wa Al-Aqsa ulioko Baitul-Muqaddas Mashariki inayokaliwa kwa mabavu.
-
Wagonjwa laki mbili hatarini kufariki dunia Ghaza kutokana na Israel kuendelea kufunga vivuko
Apr 19, 2025 22:56Wizara ya Afya ya Palestina imetahadharisha kuwa watu 200,000 wenye maradhi thakili wako hatarini kupoteza maisha kutokana na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kuendelea kuvifunga vivuko, jambo ambalo linavuruga pia utendaji kazi wa hospitali katika Ukanda huo.
-
Mkuu wa Umoja wa Maulamaa aghadhibishwa vikali na kimya cha Ulimwengu wa Kiislamu kuhusiana na Ghaza
Apr 19, 2025 22:54Mkuu wa Umoja wa Maulamaa wa Kiislamu amekosoa vikali kimya cha Ulimwengu wa Kiislamu kuhusiana na mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Waislamu Wapalestina wa Ghaza.
-
Muqawama wa Ghaza watoa pigo jingine, waangamiza na kujeruhi Wazayuni 6
Apr 19, 2025 09:43Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimeripoti "tukio kubwa la usalama" katika Ukanda wa Ghaza na pigo jingine jipya kutoka kwa Muqawama dhidi ya wanajeshi vamizi wa Israel.
-
Iran yataka kusitishwa kimya cha jamii ya kimataifa mkabala wa mashambulizi ya Marekani huko Yemen
Apr 18, 2025 22:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko bega kwa bega na wananchi wanamapambano wa Yemen na ametoa wito wa kukomeshwa kimya cha jamii ya kimataifa mbele ya ukiukwaji wa wazi wa sheria za kibinadamu na kanuni za kimataifa unaofanywa na Marekani dhidi ya watu wa Yemen.
-
Ansarullah: US inashajiisha mauaji ya kimbari Gaza, yataka Wapalestina wapewe silaha
Apr 18, 2025 03:00Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema Marekani inaihimiza na kuishajiisha Israel kuendeleza vita vya mauaji ya halaiki huko Gaza na kusisitiza kuwa Washington ni mshiriki wa utawala wa Kizayuni katika mauaji hayo ya kimbari.
-
Mashambulizi ya anga ya US kwenye bandari ya mafuta ya Ras Isa, Yemen yaua watu 33
Apr 17, 2025 23:33Jeshi la Marekani limeshambulia bandari ya mafuta ya Ras Isa magharibi mwa Yemen, na kuua makumi ya wafanyakazi na wahudumu wa afya, huku makumi ya wengine wakijeruhiwa.
-
Taasisi ya Palestina: Siku ya mateka wa Palestina; nembo ya mapambano yao katika jela za Israel
Apr 17, 2025 23:10Ofisi ya Habari ya serikali katika Ukanda wa Gaza imetaja tarehe 17 Aprili liyoadhimishwa jana Alhamisi ambayo imepewa jina la Siku ya Mateka wa Palestina kuwa ni inakumbusha mateso, maumivu na masaibu wanayopitia zaidi ya mateka elfu kumi wa Kipalestina wanaoshikiliwa katika jela za utawala wa Kizayuni.
-
HAMAS yakataa pendekezo la kuweka silaha chini
Apr 17, 2025 09:10Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeripotiwa kupinga pendekezo la utawala haramu wa Israel la kusitisha vita kwa muda wa wiki sita katika Ukanda Gaza, sambamba na kulitaka kundi hilo la muqawama kuafiki kupokonywa silaha.
-
Jasusi mzoa taka anaswa kwenye mtego wa vikosi vya Muqawama Ghaza
Apr 17, 2025 02:12Vikosi vya Muqawama huko Ghaza vimemnasa kwenye mtego, jasusi wa utawala katili wa Kizayuni wa Israel ambaye alijifanya ni mzoa taka kumbe alikuwa anafanya ujasusi wa kujua walipo mateka wa Kizayuni.