-
Chama cha Ben-Gvir chajitoa kwenye serikali ya Israel kupinga makubaliano ya usitishaji vita Ghaza
Jan 19, 2025 07:10Chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Nguvu za Kiyahudi (Otzma Yehudit) cha waziri wa usalama wa ndani Itamar Ben-Gvir kimejiondoa kwenye serikali ya muungano ya utawala wa Kizayuni kulalamikia makubaliano ya kusitishwa vita katika Ukanda wa Ghaza.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel akiri kushindwa mbele ya Hamas
Jan 19, 2025 02:38Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Gideon Sa'ar, amekiri kwamba utawala huo umeshindwa mbele ya harakati ya Hamas na kwamba ulishindwa kuwakomboa mateka wake waliokuwa wakishikiliwa huko Gaza.
-
UNICEF: Watoto 15,000 wameuawa Gaza tangu Oktoba 2023
Jan 18, 2025 23:09Mfuko wa Kudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, watoto wasiopungua 15,000 wameuawa katika Ukanda wa Gaza tangu utawala wa Kizayuni wa Israel ulipoanzisha vita vyake dhidi ya ukanda huo Oktoba 7 mwaka 2023.
-
Kukiri viongozi wa Kizayuni kuwa wameshindwa na Muqawama kwenye vita vya Ghaza
Jan 18, 2025 23:06Baada ya kupita saa chache tu tokea kutangazwa usitishaji mapigano katika vita vya Ghaza, viongozi wa Kizayuni wamekiri kuwa wameshindwa na Muqawama wa Palestina katika vita hivyo.
-
Sheikh Naim Qassim: Nafasi ya Gaza itasajiliwa katika historia
Jan 18, 2025 08:16Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amepongeza makubaliano ya kustisha vita katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa nafasi ya Gaza katika kujitolea itasajiliwa katika historia.
-
Abu Sharif: Wananchi wa Gaza wamezuia ushindi wa utawala wa Israel
Jan 18, 2025 07:28Mwakilishi wa harakati ya Jihad Islami ya Palestina mjini Tehran amesema: Licha ya uchache wa suhula waliokuwa nao, wananchi wa Gaza waliweza kuendeleza mapambano yao ya ukombozi na kuzuia kusonga mbele utawala wa Kizayuni kutokana na uungaji mkono na msaada mkubwa wa Mhimili wa Muqawama unaojumuisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Lebanon, Iraq na Yemen.
-
Yemen yaitwanga meli ya kivita ya Marekani kwa mara ya saba
Jan 18, 2025 03:14Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kuwa, jeshi la nchi hiyo limefanya operesheni nne za kijeshi dhidi ya utawala wa Kizayuni na Marekani, muhimu zaidi ikiwa ni kuishambulia manuwari ya kubebea ndege ya Marekani iitwayo "Truman" kaskazini mwa Bahari Nyekundu.
-
Qatar: Inabidi UN itoe azimio la kuilazimisha Israel iheshimu usimamishaji vita Ghaza
Jan 18, 2025 03:14Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesisitiza kuwa jumuiya ya kimataifa inapaswa kutoa msaada unaohitajika wa kuzisaidia familia zilizoathirika katika mashambulizi ya kikatili ya Israel huko Ghaza na kuhakikisha kunatolewa azimio ambalo litaulazimisha utawala wa Kizayuni kuheshimu usimamishaji vita.
-
Guterres aitaka Israel kusitisha ukiukaji wa azimio nambari 1701 kusini mwa Lebanon
Jan 17, 2025 23:11Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ameitaka Israel ikomeshe kukalia kwa mabavu ardhi ya Lebanon na kufanya operesheni za kijeshi ndani ya nchi hiyo, akisisitiza kuwa vitendo hivi vinakiuka azimio nambari 1701 la Baraza la Usalama.
-
Israel imewauwa shahidi Wapalestina zaidi ya 100 huko Gaza licha ya tangazo la usitishaji vita
Jan 17, 2025 10:27Idara ya Ulinzi wa Raia ya Gaza imetangaza leo Ijumaa kuwa Wapalestina wasiopungua 101, wakiwemo watoto 27 na wanawake 31, wameuawa shahidi katika mashambulizi ya Israel tangu kutangazwa makubaliano ya kusitisha mapigano juzi Jumatano.