-
HAMAS: Israel imeshambulia kwa mabomu mahali alipokuwa anashikiliwa mateka mmoja wa Israel
Jan 16, 2025 23:49Abu Ubaydah, msemaji wa Brigedi za Izzuddin Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel jana Alkhamisi lilishambuliwa kwa makusudi eneo ambalo mateka mmoja wa kike wa Israel alikuwa akishikiliwa kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Vikwazo; Fimbo ya Magharibi katika sera ya kigeni
Jan 16, 2025 23:25Wakati Marekani na nchi za Ulaya zimekuwa na nafasi kubwa katika kuwawekea mashinikizo ya kiuchumi watu wa Syria kwa kutumia vikwazo vya kikatili, sasa baada ya kuanguka utawala wa Bashar al-Assad na kushika madaraka kundi la Hay'at Tahrir al-Sham, kuna minong'ono kwamba nchi hizo zina nia ya kupunguza vikwazo dhidi ya nchi hiyo.
-
Kuchunguzwa matokeo ya usitishaji vita Ukanda wa Gaza
Jan 16, 2025 09:50Baada ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) kutangaza rasmi kukubali usitishaji vita na kuanza mchakato wa kuhitimisha vita katika ukanda huo, hapana shaka kuwa masuuala ya kimedani na kisiasa katika eneo hilo yataathiriwa na tukio hilo.
-
Gaza imeshinda: Watumiaji wa mitandao ya kijamii wazungumzia usitishaji mapigano Gaza
Jan 16, 2025 07:47Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamezungumzia habari ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Hamas na Israel katika Ukanda wa Gaza kwa hisia mchanganyiko za furaha na matumaini ya mustakbali mwema.
-
Israel yasalimu amri baada ya kushindwa kuiangamiza HAMAS
Jan 16, 2025 04:07Baada ya mapigano ya miezi 15 huko Ghaza hatimaye utawala wa Kizayuni wa Israel umelazimika kusalimu amri na kukubali makubaliano ya kusitisha mapigano bila ya kufanikiwa kuiangamiza Hamas wala kokomboa mateka wa Kizayuni.
-
Hamas: Makubaliano ya kusitisha vita ni matunda na Muqawama wa miezi 15 wa wananchi wa Ghaza
Jan 16, 2025 04:03Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imesema kuwa, kulazimika utawala wa Kizayuni kukubali kusimamisha vita na kukomesha mauaji yake ya kimbari dhidi ya wananchi wa Ghaza, ni matunda ya Muqawama na kusimama imara wananchi wa ukanda huo kwa zaidi ya miezi 15.
-
Israel imeshaua Wapalestina 40 Ghaza tangu baada ya kutangazwa makubaliano ya kusitisha vita
Jan 16, 2025 00:07Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeendeleza mashambulio katika Ukanda wa Ghaza licha ya kutangazwa makubaliano ya kusitisha vita kati ya utawala huo ghasibu na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS. Hadi wakati huu, Wapalestina wasiopungua 40 wameshauliwa shahidi na jeshi hilo.
-
Mapigano ya silaha yazuka kati ya wanamgambo wa Al-Joulani, wawania mamlaka ya kuendesha miji ya Syria
Jan 15, 2025 23:07Duru za Syria zimeripoti kuwa yamezuka mapigano ya silaha kati ya wanamgambo wenye mfungamano na Al-Joulani, kamanda wa kundi la wabeba silaha la Hay-at Tahrir al-Sham.
-
Waziri Mkuu wa Iraq: Iran ilikuwa Syria kwa ombi la serikali ya Assad kwa ajili ya kupambana na ugaidi
Jan 15, 2025 23:07Waziri Mkuu wa Iraq, Mohammed Shia' al-Sudani amesema Iran ilikuwa nchini Syria kutokana na ombi rasmi la serikali ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Bashar al-Assad, kwa lengo la kuisaidia nchi hiyo ya Kiarabu katika vita dhidi ya ugaidi.
-
TV ya Marekani yaonyesha mabaki ya silaha za nchi hiyo Ghaza zinazotumika katika mauaji ya kimbari
Jan 15, 2025 08:07Kanda za video zilizorushwa hewani na chaneli kubwa ya televisheni ya Marekani ya CBS zimefichua kuwepo kwa silaha nyingi ambazo serikali ya Washington imeupatia utawala wa Kizayuni wa Israel uzitumie katika mauaji ya kimbari ya Wapalestina unayofanya katika Ukanda wa Ghaza, suala ambalo limekabiliwa na malalamiko na ukosoaji mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.