-
Hizbullah yatungua ndege ya kivita ya Israel isiyo na rubani
Oct 16, 2024 00:53Wapiganaji wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon wameiangusha ndege ya kivita isiyo na rubani ya jeshi katili la Israel kusini mwa Lebanon sambamba na kuvurumisha makombora katika maeneo ya kijeshi ya Israel katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ili kulipiza kisasi jinai zinazoendelea za utawala wa Tel Aviv dhidi ya Ukanda wa Gaza na Lebanon.
-
Uwepo wa Wamarekani katika kambi za kijeshi za utawala wa Israel
Oct 15, 2024 08:33Gazeti la The Guardian, linalochapishwa mjini London, limeripoti kuwepo kwa maafisa wa Marekani katika mikutano ya kila siku inayofanyika katika kambi za kijeshi za utawala ghasibu wa Israel.
-
Arab League: Mauaji ya kimbari ya Israel Gaza yanalenga kuwatimua Wapalestina
Oct 14, 2024 22:48Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imelaani operesheni za mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni huko Gaza na kuzitaja hatua hizo kuwa ni sehemu ya mpango mpana kuwatimua kwa lazima Wapalestina wa eneo hilo.
-
Umoja wa Mataifa wataka kusitishwa mapigano katika Ukanda wa Gaza na Lebanon
Oct 14, 2024 22:48Umoja wa Mataifa umesisitizia wito wa kusitishwa kwa mapigano nchini Lebanon na katika Ukanda wa Gaza kama njia moja ya kuzuia kutokea kwa mzozo zaidi mashariki ya kati, hatua ambayo UN inasema itaathiri dunia nzima.
-
'Hizbullah iko katika mkao wa vita, siku ngumu zinaisubiri Israel'
Oct 14, 2024 10:13Kamanda Mkuu wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ameuonya utawala haramu Israel kuhusu "siku ngumu" zijazo huku harakati ya muqawama ya Lebanon Hizbullah ikijiimarisha kivita ili kukabiliana na uvamizi wa Israel.
-
Kushindwa Wazayuni kukabiliana na oparesheni za kibunifu za Hizbullah ya Lebanon
Oct 14, 2024 08:33Shambulio la ubunifu la Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon katika makao makuu ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu, kwa mara nyingine tena limefichua kushindwa na udhaifu wa Wazayuni mkabala wa oparesheni za kijeshi za makundi ya muqawama.
-
Wanajeshi wa Kizayuni waangamizwa Gaza na wanamuqawama wa HAMAS
Oct 14, 2024 08:07Wanajeshi kadhaa wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameangamizwa na kujeruhiwa na Mujahidina wa Brigedi za Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Israel yateketeza mahema kwenye Hospitali ya Ghaza na kuwachoma moto Wapalestina wakiwa hai
Oct 14, 2024 02:42Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeishambulia kwa mabomu kambi ya wakimbizi katika eneo la kati la Ukanda wa Ghaza na kusababisha moto mkubwa uliopelekea kuuawa shahidi Wapalestina waliokuwa wametafuta hifadhi kwenye eneo hilo kutokana na hilaki ya vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala huo ghasibu.
-
Hizbullah: Israel imemimina mabomu yaliyopigwa marufuku ya vishada kusini mwa Lebanon
Oct 14, 2024 02:12Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah imesema utawala wa Kizayuni wa Israel umemimina "makombora yaliyosheheni mabomu ya vishada" kwenye vitongoji vya kusini mwa Lebanon.
-
Makumi ya wanajeshi wa Israel wauawa, kujeruhiwa; Hizbullah yapiga kambi ya jeshi huko Haifa
Oct 13, 2024 23:51Mujahidina wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon wamefanya mashambulizi makali dhidi ya vituo vya kijeshi na maeneo ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji wa Haifa, na kuua wanajeshi kadhaa wa utawala huo.