-
Vikosi vya Yemen vyatumia kombora jipya la balistiki dhidi ya Israel
Jun 04, 2024 08:23Vikosi vya Wanajeshi vya Yemen vimetangaza kutumia kombora jipya la balistiki dhidi ya shabaha ya eneo la kijeshi la utawala haramu wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu katika operesheni mpya ya kuiunga mkono Palestina.
-
Kiongozi wa Hizbullah aishukuru Iran kwa kuunga mkono muqawama, mataifa ya eneo
Jun 04, 2024 08:01Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon ametoa shukurani zake za dhati kwa Iran kwa uungaji mkono wake "imara" kwa mataifa ya eneo na harakati za muqawama (mapambano ya Kiislamu) katika eneo.
-
Watoto zaidi ya 3,500 hatarini kufariki dunia Ghaza kutokana na sera ya 'mateso ya njaa' ya Israel
Jun 03, 2024 23:58Ofisi ya habari ya Serikali katika Ukanda wa Ghaza imetangaza kuwa, zaidi ya watoto 3,500 wako hatarini kufariki dunia kutokana na uhaba wa chakula na njaa inayosababishwa na sera ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuwatesa kwa njaa Wapalestina wa eneo hilo.
-
UN: Wapalestina milioni moja wamelazimika kukimbia Rafah
Jun 03, 2024 22:48Wapalestina zaidi ya milioni moja sasa wamefungasha virago na kuukimbia mji wa Rafah kusini mwa Gaza huku utawala katili wa Israel ukiendeleza mashambulizi ya kinyama dhidi ya wakimbizi katika eneo hilo.
-
Utawala wa Kizayuni wakiri kushindwa katika kukabiliana na nguvu za kijeshi za muqawama wa Kiislamu wa Lebanon.
Jun 03, 2024 22:45Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimekiri kwamba nguvu za utawala huo za kuzuia mashambulio ya muqawama wa Kiislamu wa Lebanon katika eneo la kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel) zimedhoofika na kutoweka kabisa.
-
Makumi wauawa shahidi Gaza katika hujuma za anga za Israel
Jun 03, 2024 07:58Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel zimefanya mashambulizi ya anga katika maeneo kadhaa ya Ukanda wa Gaza zikiwemo kambi za wakimbizi na kuua shahidi makumi ya Wapalestina.
-
Adhabu kwa wanachuo wa Marekani wanaounga mkono Palestina
Jun 03, 2024 03:41Makumi ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Chicago nchini Marekani wameondoka katika chuo hicho wakipinga hatua ya bodi ya wakurugenzi ya kukataa kutoa shahada za wanafunzi wanaounga mkono Palestina.
-
Wanachama wa WHO wakaribisha Palestina kupatiwa haki sawa za uanachama
Jun 03, 2024 03:23Nchi za wanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO) zimekubaliana na suala la Palestina kupatiwa haki sawa za uanachama katika shirika hilo la kimataifa.
-
Harakati ya Kiislamu ya Iraq yatekeleza mashambulizi mapya dhidi ya Israel
Jun 02, 2024 23:19Katika kukabiliana na hujuma za utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza hususan katika mpaka wa kusini mwa mji wa Rafah, wapiganaji wa Harakati ya Kiislamu ya Iraq wamefanya operesheni mbili tofauti dhidi ya mitambo ya kimkakati ya ardhi za Palestina zilizokaliwa kwa mabavu mwaka 1948 na kupachikwa jina bandia la Israel
-
Maandamano ya kutaka kusitishwa 'jinai za kivita' Gaza yaendelea kufanyika Ulaya na Asia
Jun 02, 2024 05:54Maandamano ya kulaani mauaji ya halaiki yanayofanywa na jeshi la uutawala haramu wa Israel huko Gaza yanaendelea kushuuhudiwa katika mataifa mbalimbali barani Ulaya na Asia.