-
Mawaziri 13 wa Mambo ya Nje wakiwemo 6 wa G7 waitaka Israel isitishe uvamizi wa ardhini wa Rafah
May 17, 2024 04:46Shirika la habari la DPA la Ujerumani limeripoti kuwa mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 13 wametia saini barua ya kuuonya na kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usitishe uvamizi wake wa ardhini katika eneo la Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza na kuruhusu misaada zaidi kuwafikia Wapalestina.
-
HAMAS: Mashambulio ya Israel yameua 70% ya mateka wa Kizayuni
May 17, 2024 04:43Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel katika Ukanda wa Ghaza, unaokabiliwa na vita vya mauaji ya kimbari ya utawala huo ghasibu, yameua asilimia 70 ya mateka wa Kizayuni, ambao wanashikiliwa na harakati hiyo ya muqawama tangu ilipotekelezwa operesheni ya mwezi Oktoba ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
"Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu"
May 17, 2024 03:40Rais wa Chuo cha Da'awa ya Kiislamu cha Lebanon amesema ibada ya Hija ya mwaka huu ina umuhimu wa kipekee wakati huu ambapo Wazayuni wanaendelea kumwaga damu za Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, "Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu."
-
Viongozi wa Kiarabu waondoka Bahrain bila ya msimamo wowote wa kuiadhibu Israel kwa jinai za Ghaza
May 17, 2024 03:40Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imetoa wito katika mkutano wa viongozi wa nchi wanachama uliofanyika nchini Bahrain wa kuundwa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina na kuitishwa mkutano wa kimataifa wa amani, lakini imeshindwa kuidhinisha hatua yoyote ya kuuadhibu kiuchumi na kisiasa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa mauaji ya kimbari unayoendelea kufanya dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
-
Zaidi ya watoto 15,000 wameuawa na jeshi la Israel katika Ukanda wa Gaza
May 16, 2024 08:52Zaidi ya watoto 15,000 wanaripotiwa kuuawa shahidi na jeshi la utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
AFC yataka FIFA iifutie uanachama Israel kutokana na jinai zake Gaza
May 16, 2024 08:51Shirikisho la Soka Asia (AFC) limetangaza kuunga mkono ombi la Palestina la kulitaka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) liifutie uanachama Israel katika taasisi hiyo kubwa zaidi ya kandanda duniani, kutokana na utawala huo wa Kizayuni kutenda jinai kubwa dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Maandamano ya Wazayuni dhidi ya Baraza la Mawaziri la Netanyahu katika Siku ya Nakba
May 16, 2024 05:47Moja ya matukio muhimu yaliyojiri katika Siku ya Nakba mwaka huu ni maandamano yaliyofanywa na Wazayuni wanaopinga vita dhidi ya Gaza. Wazayuni hao waliandamana mbele ya jengo la Wizara ya Vita ya Israel huko Tel Aviv.
-
HAMAS: Tumeangamiza askari 12 wa Israel katika 'operesheni tata' Jabalia, Ghaza
May 16, 2024 03:55Izzuddin-al Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa wapiganaji wake wamewaangamiza wanajeshi 12 wa Israel katika eneo lililozingirwa la kaskazini mwa Ghaza.
-
Haniyah Katika Siku ya Nakba: Bila shaka Israel itatimuliwa Palestina
May 16, 2024 01:08Ismail Haniyah, Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amesema bila shaka utawala wa Kizayuni wa Israel hatimaye utaondolewa katika maeneo yote ya Wapalestina.
-
Marekani kukanusha tena kutokea mauaji ya kimbari huko Ukanda wa Gaza, ni kukana ukweli ulio wazi
May 16, 2024 00:55Licha ya Wapalestina zaidi ya elfu 35,000 kuuawa shahidi na utawala wa kigaidi wa Israel huko Ukanda wa Gaza, lakini Jake Sullivan, Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Ikulu ya White House nchini Marekani amedai bila kuona haya kwamba serikali ya Rais Joe Biden haiyachukulii mauaji hayo kuwa ni mauaji ya halaiki.