-
Yasser Abu Shabab, mshirika wa Israel na msaliti wa Wapalestina wa Ghaza aripotiwa kuuawa
Dec 05, 2025 03:25Yasser Abu Shabab, mshirika wa kijeshi wa utawala wa kizayuni wa Israel mwenye uhusiano pia na kundi la kigaidi la DAESH (ISIS), maarufu kwa kuongoza uporaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza na kwa kuwalenga kwa kuwaua raia wa Palestina, ameripotiwa kuuawa katika eneo hilo.
-
Hamas: Israel iwajibishwe kwa kuzika mamia ya miili ya Wapalestina kwenye makaburi ya umati
Dec 04, 2025 23:27Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imezitaka mahakama za kimataifa na vyombo husika kuwafungulia mashtaka wale waliohusika wa uhalifu wa kivita baada ya uchunguzi kufichua kwamba wanajeshi wa Israel waliteketeza miili ya Wapalestina waliokuwa katika safu za kupokea misaada na kuizika katika makaburi yasiyo na kina huko Gaza.
-
Vita vya Kijasusi; Kadi ya Ushindi ya Iran dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Dec 04, 2025 08:41Meya wa Bat Yam katikati ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, zilizopachikwa jina bandia la Israel, amekiri kuongezeka kwa ushawishi wa kijasusi wa Iran.
-
Microsoft yalaumiwa kuhusika na jinai za Israel za maauaji kimbari dhidi ya Gaza
Dec 04, 2025 08:35Muungano wa makundi ya kisheria umelionya shirika la Microsoft kwamba utoaji wake wa huduma kwa Israel wakati wa vita vya mauaji ya kimbari huko Gaza huenda ukaifanya kampuni hiyo kubwa ya teknolojia ya Marekani ishtakiwe katika mahakama za kimataifa.
-
Baraza Kuu la UN lapasisha azimio linaloitaka Israel iondoke katika maeneo ya Wapalestina
Dec 04, 2025 04:15Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha rasimu ya azimio llinaloitaka Israeli iondoke kwenye maeneo ya Palestina iliyoyavamia na kuyakaliwa kwa mabavu tangu 1967, ikiwa ni pamoja na al-Quds Mashariki. Rasimu ya azimipia imeitaka Israel itambue haki ya watu wa Palestina ya kujitawala na kuasisi nchi huru.
-
Azimio la UN: Israel inaikalia "kinyume cha sheria" Miinuko ya Golan ya Syria, iondoke kikamilifu
Dec 03, 2025 07:24Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotangaza kuwa, kuendelea Israel kuikalia kwa mabavu na kuiunganisha na upande wake Miinuko ya Golan ya Syria ni "kinyume cha sheria" na limeutaka utawala huo uondoke kikamilifu katika eneo hilo hadi kwenye mstari wa mpaka wa Juni 4, 1967.
-
Netanyahu amramba miguu Trump amuokoe na kitanzi cha kesi mahakamani
Dec 03, 2025 03:07Duru za kuaminika za Marekani na Israel zimefichua kuwa, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu amemuomba kwa kumsisitiza rais wa Marekani, Donald Trump afanye kila awezalo kuhakikisha kuwa anafutiwa kesi zake za ufisadi.
-
Utajiri wa madini ya Yemen na jicho la tamaa la madola ya kibeberu
Dec 02, 2025 22:52Yemen imegundua utajiri mkubwa wa rasilimali za madini, ikiwa ni pamoja na akiba kubwa ya dhahabu, chuma, titani na madini ya viwandani. Rasilimali hizi zinaweza kufungua njia ya maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha nafasi ya kimkakati ya Yemen katika eneo hili zima.
-
Watetezi wa Haki za Binadamu wataka ICC iwakamate Netanyahu na Gallant kwa uhalifu wa vita Gaza
Dec 02, 2025 09:53Kundi la mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu limeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kutekeleza hati za kukamatwa zilizotolewa dhidi ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na aliyekuwa waziri wa masuala ya kijeshi Yoav Gallant, kwa uhalifu wa vita uliofanywa katika vita vya mauaji ya halaiki Gaza.
-
Ma'ariv: Jeshi la Israel limechoka baada ya miaka miwili ya vita
Dec 01, 2025 23:12Chombo cha habari cha Kizayuni kimefichua katika ripoti yake kwamba baada ya miaka miwili na miezi miwili ya vita vikali katika pande saba, jeshi la Israel limechakaa, maafisa wake wamechoka, na wanajeshi wana ndoto ya kurudi majumbani mwao.