-
Mashinikizo ya Marekani kwa Pakistan kushiriki katika 'Kikosi cha Usalama cha Kimataifa' cha Gaza na kukataa Islamabad
Dec 23, 2025 23:08Licha ya mashinikizo ya Marekani kwa Pakistan ili kushiriki katika "Kikosi cha Usalama cha Kimataifa" cha Gaza, lakini Islamabad ilitangaza kwamba bado hakuna uamuzi uliochukuliwa nan chi hiyo wa kutuma wanajeshi katika Ukanda wa Gaza.
-
Abu Hatab wa Ghaza asimulia alivyoshiriki kuzika Wapalestina 18,000 waliouliwa kinyama na Israel
Dec 23, 2025 08:32Mzikamaiti Yousef Abu Hatab mkazi wa Ukanda wa Ghaza na mmoja wa mashuhuda wa moja ya majanga makubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Palestina, amesema ameshiriki kuzika karibu miili 18,000 ya Wapalestina waliouliwa shahidi wakati wa vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel katika eneo hilo la Palestina.
-
HAMAS yaonya kuhusu mipango hatari ya Israel dhidi ya Baytul-Muqaddas
Dec 22, 2025 23:46Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeonya kuhusu mipango hatari ya Israel dhidi ya Baytul-Muqaddas na kuwafanya Wapalestina kuwa wakimbizi.
-
Uhaba wa dawa za matibabu Gaza umefikia viwango vya kutisha kufuatia mzingiro wa Israel
Dec 22, 2025 07:22Wizara ya Afya ya Gaza imetahadharisha kuhusu uhaba mkubwa na hatari zaidi wa dawa na vifaa vya matibabu. Imesema kuwa uhaba huo umelemaza uwezo wa eneo hilo wa kutoa huduma ya dharura ya matibabu na kuokoa maisha ya wagonjwa kufuatia kuendelea mzingiro wa Israel dhidi ya Gaza.
-
Arabi21: Utawala wa Kizayuni wa Israel unasambaza dawa za kulevya huko Gaza
Dec 22, 2025 06:50Chombo cha habari cha Arabi21 kimeripoti kuwa, ingawa jeshi la Israel limezuia kuingia bidhaa nyingi muhimu huko Gaza, ripoti zinaonyesha kuwa usafirishaji haramu wa dawa za kulevya katika eneo hilo unarahisishwa.
-
Albanese: Misri inaunga mkono mauaji ya halaiki ya Wapalestina
Dec 21, 2025 23:21Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa ameitaja hatua ya Misri ya kuidhinisha makubaliano ya ununuzi wa gesi kutoka kwa utawala wa Israel kuwa ni uungaji mkono wa nchi hiyo kwa mauaji ya halaiki yanayofanywa na Wazayuni huko Gaza.
-
Hali mbaya ya wakimbizi Wazayuni; ukurasa wa kuuza viporo wapata umaarufu Israel
Dec 21, 2025 23:20Ukurasa mmoja wa mitandao ya kijamii unaouza viporo na masalia ya chakula yaliyobaki mikahawani umepata umaarufu mkubwa huko Israel kiasi kwamba kutokana na hali ngumu ya maisha, Wazayuni wengi wanajitokeza kwenye ukurasa huo kununua chakula kilichobaki mikahawani na matunda yaliyoharibika madukani.
-
Maulamaa wa Yemen walaani kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Marekani
Dec 21, 2025 08:46Maulamaa na wanazuoni wa Yemen wamelaani kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Marekani. Tukio la hivi karibuni la uhalifu huo limefanywa na mgombea mmoja wa Baraza la Seneti la Marekani.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza, Ukingo wa Magharibi
Dec 21, 2025 07:43Wapalestina wawili, akiwemo kijana mmoja, wameuawa shahidi huku wengine wawili wakijeruhiwa kwa risasi baada ya vikosi vya Israel kufanya mashambulizi tofauti katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, katika ghasia za hivi punde dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu.
-
Kwa nini mpango wa Al‑Ahram kuhusu usalama wa Asia Magharibi ni wa kupotosha na ni hatari?
Dec 21, 2025 04:27Tovuti ya Ahram Online (sehemu ya Kiingereza ya gazeti la Al-Ahram la Misri) katika makala yake imependekeza kufanyika kwa mkutano wa usalama katika eneo la Asia ya Magharibi, kwa ushiriki wa madola yenye nguvu zaidi duniani, ili kuzuia kuanza tena kwa vita kati ya Iran na utawala wa Kizayuni wa Israel.