-
Malori ya misaada 986 tu kati ya 6,600 yameingia Gaza tangu kufikiwa makubaliano ya kusitisha vita
Oct 22, 2025 09:39Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Serikali ya Gaza imeripoti kuwa ni malori 986 pekee ya misaada yaliyoingia katika eneo hilo linalozingirwa tangu kusitishwa kwa mapigano kati ya Harakati ya Mapambano ya Palestina (Hamas) na utawala wa Israel tarehe 10 mwezi huu.
-
Utaratibu Mpya wa Kiuchumi wa Kikanda; Nafasi ya kimkakati ya Iran katika Ushirikiano na Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia
Oct 22, 2025 09:11Mkutano wa Nne wa Kistratijia wa "Iran na Eurasia; Biashara, Diplomasia na Utaratibu Mpya wa Kikanda," umefanyika leo katika Kituo cha Mikutano cha Shirika la Utangazaji la Sauti na Televisheni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Tehran.
-
Yemen nchi ya kwanza ya Kiarabu kujizalishia yenyewe silaha za maana
Oct 22, 2025 02:46Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema: Kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu Yemen imefanikiwa kuwa nchi ya kwanza kati ya nchi zote za Kiarabu katika uzalishaji wa silaha na zana za kijeshi. Uzalishaji wa makombora katika nchi yetu uko kwenye njia inayozidi kustawi na tuna mafanikio makubwa katika uzalishaji wa droni na ndege zisizo na rubani.
-
Hamas: Israel lazima igharamie ujenzi mpya wa Gaza
Oct 21, 2025 08:01Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Mousa Abu Marzouk ametoa wito kwa Israel kufadhili kikamilifu ukarabati na ujenzi mpya wa Ukanda wa Gaza, akitaja uharibifu mkubwa na haki za Wapalestina zaidi ya milioni mbili ambao wamepoteza makazi yao, makazi na riziki.
-
Hizbullah: Trump anajiona mtu wa amani ilhali ni gaidi namba moja duniani
Oct 21, 2025 03:32Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Siasa la Hizbullah amesisitiza kuwa, Rais wa Marekani anajiona ni “mtu wa amani” duniani ilhali kiuhalisia yeye ni “mchekeshaji, muigizaji, mdanganyifu na mzandiki, na ndiye gaidi namba moja duniani” aliyemuua shahidi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sayyed Hassan Nasrullah (Radhi za Allah ziwe juu yake), kwa mabomu ya Marekani.
-
Amir wa Qatar: Vita vya Israel dhidi ya Ghaza si kingine chochote ila ni mauaji ya kimbari
Oct 21, 2025 03:30Amir wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani amesema, vita vya utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza si kitu kingine ila ni mauaji ya kimbari sambamba na kuulaani utawala huo ghasibu kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Netanyahu ajigamba kuwa siku ya Jumapili Israel iliidondoshea Ghaza tani 153 za mabomu
Oct 21, 2025 03:30Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amejigamba kuwa jeshi lake lilishambulia Ukanda wa Ghaza siku ya Jumapili kwa tani 153 za mabomu, ambayo ni sawa na kukiri kwamba utawala huo ghasibu umekiuka makubaliano ya kusitisha mapigano uliyofikia na harakati ya Hamas kupitia mpango uliopendekezwa na Rais wa Marekani.
-
HAMAS yaimarisha nguvu na udhibiti wake Ghaza
Oct 20, 2025 23:52Vyombo vya usalama vya Israel vimetangaza kuwa Hamas imekuwa ikiimarisha udhibiti wake katika Ukanda wa Ghaza tangu dakika za mwanzo za kusitishwa mapigano na inaendelea kurejesha utulivu na usalama katika maeneo mbalimbali ya ukanda huo, licha ya uharibifu na jinai kubwa za miaka miwili zilizofanywa na utawala wa Kizayuni kwenye eneo hilo.
-
Mufti wa Oman aunga mkono utayarifu wa Wayemen kukabiliana na Israel
Oct 20, 2025 23:30Mufti wa Oman ametangaza himaya na uungaji mkono wake kikamilifu utayarifu wa Wayemen kukabiliana na utawala haramu wa Israel.
-
Kushner: Hamas 'inatekeleza kwa nia njema' makubaliano ya usitishaji vita Ghaza
Oct 20, 2025 07:15Mkwe wa Rais Donald Trump wa Marekani, Jared Kushner, ambaye ni mmoja wa wapatanishi wake wakuu katika mpango wa kusitisha mapigano Ghaza, amesema harakati ya Palestina ya Hamas imekuwa "ikitekeleza kwa nia njema" makubaliano hayo, akiashiria taarifa zilizopokelewa kutoka kwa wapatanishi wa kikanda waliohusika katika mazungumzo ya usitishaji huo wa vita.