-
Madaktari Wasio na Mipaka: Zaidi ya Wapalestina 300 wameuawa shahidi tangu kusitishwa vita Gaza
Nov 22, 2025 03:46Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka limetangaza kuwa, utawala ghasibu wa Israel umewauwa shahidi Wapalestina zaidi ya 300 katika Ukanda wa Gaza tangu kufikiwa kwa usitishaji vita katika Ukanda huo.
-
The Guardian: Israel imetumia mabomu yaliyopigwa marufuku dhidi ya Lebanon
Nov 21, 2025 06:27Uchunguzi mpya uliofanywa na gazeti la Uingereza, The Guardian, umebaini kuwa Israel ilitumia mabomu yaliyopigwa marufuku wakati wa vita vyake vya hivi karibuni dhidi ya Lebanon.
-
Watoto wa Kipalestina katika jahanamu ya jela za Israel
Nov 21, 2025 05:27Jana, tarehe 20 Novemba, dunia iliadhimisha"Siku ya Watoto Duniani," huku hali ya mambo huko Palestina ikionyesha picha tofauti kabisa, ambapo watoto ndio wanaoongoza katika janga linaloendelea kulitesa eneo la Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Save the Children: Israel imeua takriban watoto 20,000 huko Gaza
Nov 20, 2025 23:31Shirika la Save the Children limesema katika taarifa yake kuwa silaha za kijeshi na mada za milipuko zimeua idadi kubwa zaidi ya watoto duniani kote mwaka 2024, huku Ukanda wa Gaza ukiripoti idadi kubwa zaidi ya vifo.
-
UNRWA yaonya kuhusu mgogoro wa kibinadamu wa Ghaza majira ya baridi kali
Nov 20, 2025 06:45Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la UNRWA amesema kwamba, usitishaji mapigano haujawa na athari yoyote katika kuboresha hali ya watu wa Ghaza, na kwamba mateso makubwa ya binadamu katika ukanda huo yanaendelea na misaada inayoingizwa ni midogo sana hasa wakati huu wa kuwadia msimu wa baridi kali.
-
Israel yafanya mashambulio ya kinyama Ghaza, yaua Wapalestina 28 na kujeruhi 77
Nov 20, 2025 02:39Wapalestina wasiopunguua 28 wameuawa shahidi katika wimbi jipya la mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza, yakiwa ni moja ya ukiukaji mkubwa zaidi wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa mwezi uliopita wa Oktoba.
-
Wataalamu: Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Gaza ni la kuwakoloni Wapalestina
Nov 19, 2025 23:29Azimio jipya la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC), linaloruhusu kile kinachoitwa kikosi cha kimataifa kutumia “mbinu zozote zinazohitajika kutekeleza wajibu wake” katika Ukanda wa Gaza limeelezwa na wataalamu kama sura nyingine ya “ukoloni” katika historia ya Palestina.
-
Kwa nini hati ya makubaliano ya kijeshi kati ya India na utawala wa Kizayuni ni hatua ya kuleta ukosefu wa utulivu Asia?
Nov 19, 2025 23:23India na utawala wa Kizayuni wa Israel zimepanua ushirikiano wao wa kijeshi na kiviwanda kwa kutiliana saini hati mpya ya maelewano na ushirikiano.
-
Kampuni ya silaha ya Israel ya Elbit imeingiza mapato makubwa wakati wa mauaji ya kimbari ya Gaza
Nov 19, 2025 09:00Kampuni ya Israel inayoongoza kwa utengenezaji wa silaha, Elbit Systems, imetangaza ongezeko kubwa la faida iliyopatikana katika muda wa robo mwaka kufuatia miezi kadhaa ya ushiriki wa kampuni hiyo katika mauaji ya halaiki ya Israel huko Gaza kupitia utoaji silaha, zana za kijeshi na mifumo ya ufuatiliaji, huku ikipata mikataba mipya barani Ulaya.
-
Watu 15 wauawa katika hujuma ya anga ya Israel katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina huko Lebanon
Nov 19, 2025 03:28Utawala wa Israel umefanya mashambulizi ya anga na kuuwa watu wasiopungua 15 kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi wa Kipalestina kusini mwa Lebanon.