-
Mashirika ya Kiislamu ya Marekani: Warepublican wamegeuza vikao vya Kongresi kuwa silaha dhidi ya Waislamu
May 16, 2026 02:21Mashirika ya Kiislamu nchini Marekani yametangaza kwamba vikao vya Kongresi, ambavyo wabunge wa Republican wametangaza kuwa lengo lake ni kuondoa Sharia nchini Marekani, vimekuwa silaha dhidi ya Waislamu waliowachache kwa kusababisha hofu dhidi ya wafusi wa dini hiiyo.
-
Mwanzo wa mpasuko wa kimkakati kati ya pande mbili za Atlantiki
May 15, 2026 10:16José Manuel Albares Bueno, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uhispania, akisisitiza tena sera ya serikali ya nchi yake katika kupinga uvamizi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema: 'Marekani haiwezi kutumia vituo vyetu vya anga kwa ajili ya vita dhidi ya Iran.
-
Mahakama yasitisha vikwazo vya Marekani dhidi ya Albanese kwa kauli zake kuhusu mauaji ya kimbari Gaza
May 15, 2026 04:38Jaji wa mahakama ya shirikisho katika Wilaya ya Columbia nchini Marekani amesitisha vikwazo vilivyowekwa na serikali ya Marekani dhidi ya Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina.
-
Havana yatahadharisha: Mashambulizi ya Marekani dhidi ya Cuba yatasababisha umwagaji damu
May 14, 2026 10:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba ametahadharisha kuwa: Hujuma yoyote ya kijeshi ya Marekani dhidi ya nchi hiyo itasababisha maafa ya binadamu na umwagaji damu.
-
Madaktari wa magonjwa ya akili wa Marekani: Trump anapasa kuuzuliwa mamlakani
May 14, 2026 10:11Makumi ya madaktari wa magonjwa ya akili na wataalam wakuu wa afya ya akili nchini Marekani wametia saini taarifa ambayo imemtaja Rais Donald Trump kuwa "hatari ya wazi na ya haraka" na kutaka hatua za haraka zichukuliwe ili kumuondoa madarakani.
-
Rais wa China amuonya Trump kuhusu Taiwan; usifanye makosa
May 14, 2026 09:13Rais wa China ameonya katika mazungumzo yake na mwenzake wa Marekani, Donald Trump huko Beijing kuhusu hatua zozote za Washington katika Kisiwa cha Taiwan, akisema: Kosa lolote linaweza kusababisha mzozo kati ya nchi hizo mbili.
-
Waziri Mkuu wa Uhispania ampongeza Lamine Yamal kwa kusherehekea ubingwa na bendera ya Palestina
May 14, 2026 03:29Waziri Mkuu wa Uhispania, Pedro Sanchez, amesisitiza uungaji mkono wa nchi yake kwa haki ya Wapalestina ya kuanzisha nchi yao wenyewe, akitoa maoni yake kuhusu utata uliosababishwa na hatua ya nyoka wa timu ya soka ya Barcelona, Lamine Yamal, wakati timu yake ilipokuwa ikisherehekea taji la ubingwa wa ligi ya Uhispania.
-
Barua ya wanasayansi zaidi ya 1,000 yasisitiza kulindwa vyuo vikuu vya Iran dhidi mashambulizi ya Marekani na Israel
May 14, 2026 03:27Mamia ya wanachama wa Muungano wa Kimataifa wa Wanasayansi Duniani wameandika barua ya wazi kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UNESCO, na Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wakitaka kulindwa taasisi za kisayansi nchini Iran, na pande vamizi yaani Marekani na Israel ziwajibishwe.
-
Putin apongeza uzinduzi wa 'kombora lenye nguvu zaidi duniani'
May 14, 2026 03:24Russia imefanya majaribio ya kombora jipya la balestiki lenye uwezo wa kupiga shabaha kutoka bara moja hadi jingine, huku Rais Vladimir Putin wa nchi hiyo akilitaja kombora hilo lenye uwezo wa kutumia silaha za nyuklia kwa jina la "Sarmat" kuwa kombora "lenye nguvu zaidi" duniani.
-
China yaionya Marekani kuhusu mauzo ya silaha kwa Taiwan
May 14, 2026 03:20China kwa mara nyingine tena imepinga vikali hatua ya Marekani kuzidisha himaya na uungaji mkono wake wa kijeshi kwa Taiwan sambamba na ziara ya Rais Trump mjini Beijing.