-
Kukaribia mwisho wa kisiasa wa Starmer na kuzidi kupata nguvu Iran
May 13, 2026 18:54Pars Today - Magazeti ya Uingereza yameripoti kwa wingi habari inayosisitiza kuwa, kusambaratika kisiasa Waziri mkuu wa nchi hiyo Keir Starmer kumekaribia.
-
Viongozi wa dini wafanya maandamano ya amani ya 'Moral Monday' mjini Washington kulaani 'vita visivyo vitakatifu' vya Trump
May 13, 2026 12:11Viongozi wa imani za dini walifanya maandamano ya amani ya Jumatatu ya Maadili (Moral Monday) nje ya Ikulu ya White House dhidi ya 'vita visivyo vitakatifu' katika eneo la Asia Magharibi.
-
Ripoti: Watu milioni 83 watalazimika kuhama makazi yao ifikapo mwaka wa 2026
May 13, 2026 08:18Idadi ya watu waliokimbia makazi yao ndani ya nchi zao kutokana na migogoro na machafuko imeongezeka katika mwaka uliopita ikilinganishwa na watu waliokimbia makazi yao kutokana na majanga ya asili, idadi ambayo imeweka rekodi ya watu milioni 32, hasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Bolton: Trump amenaswa katika mtego wa kujitengenezea wa Iran
May 13, 2026 08:15Mshauri wa zamani wa Usalama wa Taifa wa Marekani amesema: Donald Trump, Rais wa nchi hiyo, amenaswa katika mtego wa kujitengenezea mwenyewe wa Iran.
-
Yamal apongezwa kwa kupeperusha bendera ya Palestina katika sherehe ya ubingwa wa Barça
May 13, 2026 08:12Nyota wa timu ya soka ya Barçelona, Lamine Yamal, alimeonyesha kitendo cha kupigiwa mfano kwa kupeperusha bendera ya Palestina wakati wa sherehe ya ubingwa wa timu hiyo kama ishara ya kuwaunga mkono watu wanaokandamizwa wa Palestina.
-
Uchunguzi wa Maoni: Wamarekani waliowengi wanasema Trump hakuwa na hoja ya wazi ya vita dhidi ya Iran
May 12, 2026 09:12Uchunguzi mpya wa maoni unaonyesha kuwa asilimia 66 Wamarekani wanaamini kuwa Rais Donald Trump ameshindwa kutoa hoja iliyo wazi kuhusu vita vya kichokozi vya na Marekani na Israel dhidi ya Iran. Aidha Wamarekani waliwengi wanasema wamekumbwa na hali ngumu ya kifedha kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta baada ya mashambulizi hayo.
-
China yakataa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, yaapa kulinda kampuni zake
May 12, 2026 03:59China imepinga vikali vikwazo vipya vilivyowekwa na Marekani dhidi ya kampuni zake tatu kwa madai ya kusaidia shughuli za kijeshi za Iran, na imeahidi kulinda biashara zake dhidi ya hatua hizo ambazo imezitaja kuwa za upande mmoja na zisizo halali.
-
Sera ya US ya Mwiko wa Kutosema Chochote Kuhusu Silaha za Nyuklia ya Israel Inamomonyoka?
May 09, 2026 13:08Katika hali isiyo ya kawaida na ya nadra kuwahi kushuhudiwa, wajumbe 29 wa Baraza la Wawakilishi la Marekani wamemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio wakiitaka Washington ifichue na kuweka hadharani mpango wa silaha za nyuklia wa Israel. Barua hiyo inataka kukomeshwa sera ya kiitwacho "kimya rasmi" kuhusu uwezo wa nyuklia wa Israel.
-
New York Times: Gharama ya vita vya Marekani dhidi ya Iran ni trilioni kadhaa
May 09, 2026 09:51Justin Wolfers, profesa wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Michigan, katika makala ya New York Times, amekadiria gharama ya vita vya Marekani dhidi ya Iran kuwa trilioni kadhaa za dola.
-
WHO: Virusi vya Hanta si sawa na vya COVID-19
May 09, 2026 09:39Kufuatia mlipuko wa virusi vya Hanta au kwa kiingereza Hantavirus kuzua taharuki miongoni mwa umma kufuatia vifo vya watu watatu na wengine kadhaa wanapata matibabu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limesisitiza kuwa mlipuko wa virusi huo kutoka meli ya kifahari ya kitalii ya MV Hondius si sawa na wa virusi vya COVID-19 na kwamba hatari ya virusi hivyo kuenea kwa jamii kwa ujumla bado ni ndogo sana.