Majasusi wa Magharibi: Iran haiundi silaha za nyuklia
https://parstoday.ir/sw/news/world-i136138-majasusi_wa_magharibi_iran_haiundi_silaha_za_nyuklia
Mashirika ya ujasusi ya nchi za Magharibi yamesema hakuna dalili yoyote inayoashiria kwamba Iran inarutubisha urani kwa ajili ya "kufikia kiwango cha mabomu," gazeti la New York Times limeripoti, likinukuu vyanzo mbali mbali.
(last modified 2026-02-01T09:41:44+00:00 )
Feb 01, 2026 09:41 UTC
  • Majasusi wa Magharibi: Iran haiundi silaha za nyuklia

Mashirika ya ujasusi ya nchi za Magharibi yamesema hakuna dalili yoyote inayoashiria kwamba Iran inarutubisha urani kwa ajili ya "kufikia kiwango cha mabomu," gazeti la New York Times limeripoti, likinukuu vyanzo mbali mbali.

Ingawaje shughuli zimegunduliwa katika vituo vya nyuklia, vikiwemo vilivyoharibiwa na mashambulizi ya kichokozi ya Marekani ya Juni mwaka jana, hakuna urutubuishaji wa kiwango cha juu unaoendelea, ripoti hiyo ya NYT imedai.

Marekani na utawala haramu wa Israel Juni 2025 zilifanya mashambulizi ya pamoja kwenye vituo vya nyuklia vya Iran, zikihalalisha kampeni hiyo kama njia ya kuizuia Tehran kupata silaha za nyuklia - jambo ambalo Iran imekuwa ikikanusha.

Mashambulizi hayo yalilenga viwanda vya urutubishaji urani vya Fordow na Natanz na kituo cha utafiti cha Isfahan. Katika ripoti yake hiyo, NYT imedai kuwa, urani iliyozikwa katika maeneo yaliyoshambuliwa - nyenzo zilizo karibu na viwango vya kiwango cha silaha - bado ipo. Kazi katika maeneo hayo inaonekana kuwa mdogo kwa uchimbaji unaolenga kuunda vituo salama zaidi.

Rais Donald Trump wa Marekani alidai kuwa mashambulizi hayo ya Juni "yalifuta kikamilifu" uwezo wa Iran wa kurutubisha urani, lakini kwa mujibu wa ripoti ya Idara ya Strateji ya Ulinzi wa Kitaifa wa Marekani iliyotolewa hivi karibuni, mashambulizi hayo "yalidhoofisha kwa kiasi kikubwa" mpango huo.

Vyanzo vya habari vimeiambia NYT kwamba, Iran inaweza kuanzisha tena mitambo ya kusukuma maji kwa kasi katika miezi miwili na kufikia kiwango cha kurutubisha urani kwa 'kiwango cha bomu' katika kipindi cha hadi mwaka mmoja, mara tu itakapopata fueli yake illiyozikwa.

Viongozi wa Iran akiwemo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei wamesisitiza mara chungu nzima kwamba, ustawi wa sekta ya nyuklia hapa nchini una malengo ya amani na kwa ajili ya kuimarisha ustawi wa taifa, na wala si kwa ajili ya kuzalisha silaha za nyuklia.