Kenya na Burundi zakubaliana kuimarisha uhusiano wa pande mbili
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i70778-kenya_na_burundi_zakubaliana_kuimarisha_uhusiano_wa_pande_mbili
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake wa Burundi, Evariste Ndayishimiye wamesaini mapatano ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa Nairobi na Bujumbura katika nyuga mbalimbali.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Jun 01, 2021 08:18 UTC
  • Kenya na Burundi zakubaliana kuimarisha uhusiano wa pande mbili

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake wa Burundi, Evariste Ndayishimiye wamesaini mapatano ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa Nairobi na Bujumbura katika nyuga mbalimbali.

Mapatano hayo yalisainiwa jana mjini Kisumu, magharibi mwa Kenya, ambapo mataifa hayo mawili wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yamekubaliana kuboresha mahusiano yao katika nyuga za kilimo, michezo, utamaduni, biashara na mambo ya nje. 

Kadhalika pande mbili hizo zimesisitizia azma yao ya kuiendelea na kuistawisha jumuiya ya EAC. 

Marais wa Kenya na Burundi wameafikiana juu ya kuangalia upya makubaliano ya Kamisheni ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano ya mwaka 2018, kwa lengo la kuimarisha zaidi uhusiano wa nchi mbili hizo.

Bendera za nchi wanachama wa EAC

Aidha Kenya na Burundi zimekubaliana kulipa kipaumbele suala la elimu katika mipango yao ya baada ya janga la Corona ambalo linaendelea kuitikisa dunia.

Kenya na Burundi ni nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambayo mwaka 2010, ilizindua soko la pamoja.