-
Muungano wa upinzani DRC wasisitiza msimamo wa mazungumzo jumuuishi ya kitaifa
Aug 14, 2026 03:02Muungano wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) unaojulikana kama C64 (Coalition Article 64), umesisitiza msimamo wake wa kumtaka Rais Félix Tshisekedi kuitisha mazungumzo ya kitaifa yanayowahusisha watu wote kabla ya tarehe 15 Agosti 2026, au wachukue hatua za kisiasa.
-
Indhari ya UN na SADC kuhusu El Niño, Kenya yatangaza maeneo yaliyo katika hatari kubwa
Aug 13, 2026 04:35Uchambuzi mpya wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani (WFP) unaonyesha kuwa mfumo wa hali ya hewa wa El Niño unaozidi kuimarika kwa kasi unatarajiwa kuzidisha kwa kiasi kikubwa ukosefu wa usalama wa chakula katika baadhi ya nchi zilizo katika hali hatarishi zaidi duniani hadi mwaka 2027.
-
Zambia yaelekea kwenye uchaguzi; Rais Hichilema anawania muhula wa pili
Aug 13, 2026 04:32Watu wa Zambia leo Alhamisi wanashiriki katika uchaguzi ili kuamua iwapo Rais Hakainde Hichilema atapata muhula wa pili wa miaka mitano kama zawadi ya mpango wake wa ufufuzi wa uchumi katika taifa hilo la Kusini mwa Afrika, ambalo ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa shaba duniani lakini lilikumbwa na mgogoro wa madeni hivi karibuni.
-
Kongo: Mkurugenzi Mkuu wa WHO atahadharisha kuhusu mlipuko wa Ebola
Aug 13, 2026 03:39Baada ya kurejea kutoka ziarani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametahadharisha kuhusu mlipuko wa Ebola.
-
Watu 95 wafariki dunia Zimbabwe baada ya kivuko kuzama kwenye Ziwa Kariba
Aug 12, 2026 11:49Watu 95 wamefariki dunia nchini Zimbabwe, baada ya kivuko walichokuwa wakisafiria kuzama kwenye Ziwa Kariba.
-
Mtawala wa Dubai 'azongwa' kwenye mitaa ya London kwa kuhusika UAE katika vita vya Sudan
Aug 12, 2026 03:31Mtawala wa Dubai ambaye ni waziri mkuu wa Muungano wa Falme za Kiarabu, UAE amezongwa kwa maneno katika mitaa ya katikati mwa mji mkuu wa Uingereza, London kuhusiana na ushiriki wa nchi yake katika vita vya ndani nchini Sudan.
-
Wachimba migodi haramu wasiopungua 14 wamepoteza maisha mgodini Afrika Kusini
Aug 11, 2026 11:22Polisi ya Afrika Kusini leo imetangaza kuwa wachimbaji wadogo wa madini wasiopungua 14 wamefariki dunia na wengine wengi kujeruhiwa katika mgodi ambao hautumiki nchini humo.
-
Shirika la Taifa la Mafuta la Libya lasema halitaweza kutekeleza mikataba katika kituo cha Zawiya baada ya hujuma ya droni
Aug 11, 2026 11:20Shirika la Taifa la Mafuta la Libya leo Jumanne limetangaza kuwa halitaweza kutekeleza mikataba na kwamba litasimamisha kikamilifu utendaji katika eneo la mafuta la Zawiya, magharibi mwa Libya, kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya ndege zisizo na rubani kwenye vituo vyake.
-
Muungano wa Sahel na Nigeria: Mgogoro wa kauli na malumbano ya kidiplomasia
Aug 11, 2026 03:01Wikendi iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso, Karamoko Jean Marie Traore, alimwita balozi wa Nigeria huko Ouagadougou kupinga kauli za Rais wa Nigeria, Bola Ahmad Tinubu, kuhusu athari za hali ya usalama katika nchi za Muungano wa Sahel kwa nchi yake, mbele ya mabalozi wa Mali na Nigeria.
-
Uchaguzi wa urais nchini Zambia kufanyika wiki hii
Aug 10, 2026 11:00Raia wa Zambia waliotimiza masharti ya kupiga kura, Alkhamisi ya wiki hii wataelekea katika vituo vya kupigia kura katika uchaguzi wa rais unaofuatiliwa kwa karibu na ambao utakuwa kipimo cha mafanikio ya kiuchumi ya Rais wa sasa Hakainde Hichilema anayewania kuchaguliwa kwa muhula mwingine.