-
Rais wa Burkina Faso atoa tamko kuhusu mivutano ya madaraka nchini humo
Jul 23, 2026 11:47Rais wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traore, ametoa kauli nzito inayolenga kukomesha uvumi wa kuwepo kwa mivutano ya madaraka ndani ya safu za uongozi wake, akisisitiza dhamira yake ya kusalia kama kiongozi mkuu pekee wa taifa hilo. Traore aliwaambia viongozi wa jamii hivi karibuni mjini Ouahigouya, kaskazini mwa nchi hiyo kwamba: “Meli haiwezi kuwa na manahodha wawili,”
-
Trump anatafakari hujuma za kijeshi dhidi ya Mali, nchi yenye utajiri wa dhahabu
Jul 23, 2026 11:39Utawala wa Rais Donald Trump umeripotiwa kuanza kutafakari kutekeleza hujuma za kijeshi dhidi ya Mali, nchi ya Afrika Magharibi ambayo ni maarufu kwa utajiri mkubwa wa dhahabu. Hatua hii, ikiidhinishwa, itaiongeza nchi hiyo katika orodha ndefu ya mataifa yaliyolengwa na Washington tangu Rais huyo mpenda vita kurejea madarakani mwaka jana.
-
Africa CDA: Mlipuko wa ugonjwa wa Ebola DRC unaenea kwa kasi ya kutisha
Jul 23, 2026 02:49Mkurugenzi Mkuu wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa barani Afrika (Africa CDC) ametoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua za haraka ili kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola unaoendelea kuenea kwa kasi ya kutisha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
-
Zaidi ya watu 140 wafariki au kutoweka baada ya boti ya wakimbizi kukwama katika pwani ya Mauritania
Jul 22, 2026 09:45Zaidi ya watu 140 wamefariki dunia au kutoweka baada ya boti iliyokuwa imebeba wakimbizi kukwama karibu na mwambao wa Mauritania.
-
Ripoti ya Umoja wa Mataifa yafichua: Afrika imeipiku Asia kama kitovu cha njaa duniani
Jul 22, 2026 03:20Mkuu wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) wenye makao yake makuu huko Roma ameonya kuwa, migogoro na machafuko katika masoko ya nishati duniani vinaweza kuwasukuma mamilioni zaidi ya watu kwenye njaa kwa kuzidisha gharama za mafuta, mbolea na chakula. Taarifa hii imetolewa huku ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa maendeleo ya kimataifa dhidi ya njaa bado yako tete.
-
Misri yaishutumu Ethiopia kuwa inasimamia Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance kwa "njia ya kisiasa"
Jul 22, 2026 03:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty ameituhumu Ethiopia kuwa inasimamia Bwawa Kuu la Renaissance (GERD) kwenye Mto Nile "kwa njia ya kisiasa" kupitia hatua za upande mmoja dhidi ya Misri na Sudan.
-
Upinzani Cameroon wataka kuchukuliwe hatua ya kikatiba na kutangazwa nafasi wazi ya urais
Jul 22, 2026 03:01Kutokuwepo nchini kwa muda mrefu Rais wa Cameroon, Paul Biya, kunasababisha utata mkubwa nchini humo, zaidi ya siku 44 baada ya kuondoka nchini Juni 7, 2026, katika safari iliyoelezwa rasmi kama "kukaa kwa muda mfupi faraghani barani Ulaya," bila ya kurudi nyumbani hadi sasa.
-
UN: Wakimbizi 144 wamefariki au kutoweka pwani ya Mauritania wakijaribu kufika Ulaya
Jul 21, 2026 11:21Wakala wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi (UNHCR) umetangaza kuwa watu 144 wameripotiwa kufariki dunia au kutoweka katika pwani ya Mauritania walipokuwa wakijaribu kuelwkea Ulaya.
-
Wanaharakati Kenya waituhumu serikali kwa kupuuza amri ya mahakama
Jul 21, 2026 03:31Wanaharakati nchini Kenya wamezituhumu mamlaka za nchi hiyo kwa kukiuka amri ya mahakama iliyozuia kuanzishwa kituo cha karantini kwa wagonjwa wa Ebola
-
Makumi ya watu wanahofiwa kupoteza maisha baada ya boti kupinduka na kuzama Nigeria
Jul 21, 2026 02:57Wafanyakazi wa huduma za uokoaji kaskazini-magharibi mwa Nigeria jana waliendelea kuwatafuta manusura baada ya boti iliyokuwa imebeba watu kadhaa kupinduka na kuzama katika jimbo la Jigawa.