-
Rais wa Afrika Kusini atoa mwito wa kuwepo taifa huru la Palestina
Sep 23, 2025 11:55Wakati vita vya Israel dhidi ya Gaza vikiendelea, Rais wa Afrika Kusini amesisitiza kuhusu dhamira ya nchi yake ya kupatikana njia ya ufumbuzi wa mataifa mawili ili kuhitimisha mzozo uliodumu kwa muda mrefu kati ya Israel na Palestina.
-
Burkina Faso, Mali na Niger zatangaza kujiondoa ICC
Sep 23, 2025 11:55Mataifa ya Afrika Magharibi ya Burkina Faso, Mali na Niger yametangaza kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) na kusema mahakama hiyo ni chombo cha ubeberu cha "Ukoloni Mamboleo".
-
WHO: Wagonjwa wa kipindupidu Sudan wafikia 113,500; chanjo yaendelea kutolewa
Sep 23, 2025 11:53Shirika la Afya Duniani leo Jumanne limetangaza kuwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu umewaathiri watu zaidi ya 113,600 na kuuwa zaidi ya 3,000 kote nchini humo tangu Julai mwaka jana.
-
Jeshi la DRC laanzisha mashambulizi ya anga dhidi ya ngome za M23 Kivu Kaskazini mashariki
Sep 23, 2025 02:58Jeshi la DRC limeanzisha mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo ya waasi katika maeneo ya Masisi na Walikale katika jimbo la Kivu Kaskazini mashariki. Hayo ni kwa mujibu wa redio ya Umoja wa Mataifa Okapi.
-
Afrika yazindua mpango wa dola bilioni 3.2 kwa ajili ya uzalishaji wa dawa na chanjo
Sep 23, 2025 02:58Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Afrika (Africa CDC) kimetangaza mpango wa ufadhili wa dola bilioni 3.2 ili kuimarisha uzalishaji wa dawa na chanjo ndani ya bara la Afrika.
-
UN, AU na EU zaahidi kushirikiana kwa ajili ya amani na maendeleo barani Afrika
Sep 23, 2025 02:57Viongozi wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika AU na Umoja wa Ulaya EU, wametilia mkazo tena dhamira yao ya kuendeleza amani na maendeleo endelevu barani Afrika, kwa kuahidi ushirikiano wa kina zaidi ili kukomesha migogoro, kuimarisha mnepo na kukabiliana na changamoto za kimataifa kuanzia madeni hadi mabadiliko ya tabianchi.
-
Makamu wa Rais wa Sudan Kusini apandishwa kizimbani, ashtakiwa kwa makosa kadhaa ukiwemo uhaini
Sep 22, 2025 12:42Mahakama ya Sudan Kusini leo Jumatatu imeanza kusikiliza kesi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar, ambaye amefutwa kazi na hasimu wake wa miongo kadhaa, Rais Salva Kiir, huku akikabiliwa na mashtaka kadhaa yakiwemo ya mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu yanayohusishwa na uasi na shambulio lililofanywa na wanamgambo wanaojulikana kama Jeshi Jeupe.
-
Mapigano makali yazuka upya magharibi mwa mji mkuu wa Libya
Sep 22, 2025 11:53Mapigano makali yamezuka upya katika eneo la Janzour, yapata kilomita 12 magharibi mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli, kati ya makundi hasimu yenye silaha ambayo yako chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) ya Waziri Mkuu Abdul Hamid Dbeibah.
-
Polisi 3 wauawa na 7 watekwa nyara katika hujuma ya wanamgambo wenye silaha Nigeria
Sep 22, 2025 09:08Maafisa watatu wa polisi wameuawa na wengine saba kutekwa nyara jana Jumapili katika shambulio la wanamgambo wenye silaha katika Jimbo la Benue nchini Nigeria.
-
Maandamano makubwa ya kuunga mkono Palestina yawavutia maelfu jijini Nairobi
Sep 22, 2025 07:42Maelfu ya Wakenya, wakiwemo Waislamu na Wakristo kwa pamoja wamejitokeza kwa wingi jijini Nairobi kushiriki maandamano na tamasha la mshikamano wa kuunga mkono Palestina, yaliyoandaliwa na kikundi cha 'Kenyans for Palestine' kwa ushirikiano na mashirika kadhaa ya kiraia.