-
Wananchi wa Algeria washiriki uchaguzi wa pili wa Bunge tangu maandamano ya mwaka 2019
Jul 02, 2026 11:41Vituo vya kupigia kura vilifunguliwa mapema leo kote nchini Algeria kwa ajili ya uchaguzi wa pili wa Bunge tangu baada ya maandamano makubwa mwaka 2019 yaliyopelekea kujiuzulu Rais wa nchi hiyo, Abdelaziz Bouteflika.
-
ICC 'yahofia' kuhusu kujiondoa kwa Mali, Burkina Faso na Niger
Jul 02, 2026 11:35Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imeeleza wasiwasi wake kuhusu kujiondoa Mali, Burkina Faso na Niger kwenye mahakama hiyo, ikisema kunadhoofisha harakati za kimataifa za kutafuta haki.
-
Ripoti ya Amnesty: RSF imefanya maangamizi ya kikabila nchini Sudan
Jul 02, 2026 03:22Kikosi cha Msaada wa Haraka nchini Sudan (RSF) kilitenda uhalifu dhidi ya ubinadamu na maangamizi ya kikabila wakati wa mashambulizi yake katika mji wa El-Fasher kati ya 2024 na 2025.
-
Umoja wa Mataifa: Ebola kuigharimu Afrika dola Bilioni 3.6
Jul 01, 2026 10:13Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, mlipuko wa virusi vya Ebola huenda ukaligharimu bara la Afrika kiasi cha dola za Marekani bilioni 3.6 pamoja na maelfu ya ajira na pengine kusababisha mzozo wa kimaendeleo kwenye bara hilo.
-
Umoja wa Mataifa: Unyanyasaji wa kingono na mauaji yaongezeka DRC
Jul 01, 2026 03:28Uchunguzi katika mikoa miwili ya mashariki mwa DRC ya Kivu Kaskazini na Kusini waonesha ukikwaji wa haki za binadamu umeongezeka kwa kiasi kikubwa.
-
Polisi wa Afrika Kusini wakabiliana na waandamanaji wanaopinga wageni
Jun 30, 2026 11:18Mamlaka nchini Afrika Kusini zimeimarisha ulinzi kwa kupeleka vikosi vya polisi katika miji mikuu ya nchi hiyo, kufuatia wimbi la maandamano dhidi ya raia wa kigeni wasio na nyaraka rasmi za ukaazi.
-
Ghasia dhidi ya wahamiaji Afrika Kusini zatarajiwa leo
Jun 30, 2026 03:42Afrika Kusini inakabiliwa na mtihani mkubwa wa kiusalama baada ya magenge ya wahalifu kuapa kuwatimu raia wa kigeni nchini humo kuanzia leo.
-
Wakenya wapinga sheria za ukaguzi wa magari, wataka zikomeshwe
Jun 29, 2026 12:15Mpango wa serikali ya Kenya wa kulazimisha magari ya kibinafsi kufanyiwa ukaguzi kila mwaka umezua hisia kali miongoni mwa umma, huku waendeshaji magari na viongozi wa upinzani wakitaka ukomeshwe na kuishutumu serikali kwa kuwatwika mzigo mwingine Wakenya wanaopambana na hali ngumu ya maisha.
-
Ripoti ya HRW: Pande zinazopigana Mali zinahusika na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu
Jun 29, 2026 12:10Pande zinazopigana nchini Mali zinahusika na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW).
-
Wanaharakati waliotoweka Kenya katika maandamano ya Gen Z wapatikana wakiwa wameteswa
Jun 28, 2026 14:07Wanaharakati watano waliotoweka baada ya kukamatwa katika maandamano ya kumbukumbu ya Gen Z ya Juni 25, wamepatikana wakiwa na majeraha na sasa wanapewa matibabu katika Hospitali ya Nairobi Women’s.