-
UN: Makubaliano ya amani ya Kongo na Rwanda 'hayaheshimiwi'
Oct 14, 2025 12:47Umoja wa Mataifa umesema kuwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda "hayaheshimiwi."
-
Kiongozi wa upinzani Cameroon Issa Tchiroma Bakary ajitangaza mshindi wa kiti cha urais
Oct 14, 2025 12:46Issa Tchiroma Bakary kiongozi wa upinzani nchini Cameroon ametangaza kwa upande mmoja kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais wa juzi Jumapili akimbwaga mshindani wake mkuu Rais Paul Biya ambaye amekuwa madarakani Cameroon kwa miaka 43.
-
Mkutano wa G20 kuhusu mazingira waanza kufanyika nchini Afrika Kusini
Oct 14, 2025 06:20Mkutano wa Tatu na G20 wa mwisho wa Kikosi Kazi cha Mazingira na Ulinzi Endelevu wa Hali ya Hewa (ECSWG) ulifunguliwa rasmi jana Jumatatu mjini Cape Town, Afrika Kusini.
-
Baadhi ya ripoti: Rais wa Madagascar ametorokea Ufaransa
Oct 14, 2025 03:53Baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais Andry Rajoelina wa Madagascar ameikimbia nchi hiyo na kuelekea Ufaransa.
-
Jeshi la Sudan ladai kuua zaidi ya wapiganaji 100 wa RSF magharibi mwa nchi
Oct 14, 2025 02:28Jeshi la Sudan (SAF) limetoa taarifa na kudai kuwa, zaidi ya wapiganaji 100 wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) wameuawa katika mapigano ya El Fasher, makao makuu ya Jimbo la Darfur Kaskazini huko magharibi mwa Sudan.
-
Mali yajibu mapigo, yawawekea Wamarekani vikwazo
Oct 13, 2025 11:29Serikali ya Mali imeweka masharti ya bondi ya viza kwa raia wa Marekani, ili kulipiza kisasi cha uamuzi wa Washington wa kuwawekea vikwazo vya usafiri raia wa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
AU yampongeza Patrick Herminie kwa kushinda urais Ushelisheli
Oct 13, 2025 10:11Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC) Mahmoud Ali Youssouf amempongeza Patrick Herminie kwa kuchaguliwa kuwa rais mpya wa Ushelisheli.
-
Ajali ya basi yaua watu 42 nchini Afrika Kusini
Oct 13, 2025 09:29Watu wasiopungua 42 wamepoteza maisha baada ya basi walilokuwa wakisafiria kubingiria katika jimbo la Limpopo, kaskazini mwa Afrika Kusini.
-
Waislamu wa Nigeria washerehekea usitishaji vita Gaza
Oct 13, 2025 06:24Wanachama wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria katika Jimbo la Bauchi wamesherehekea makubaliano ya kusitisha vita Gaza, ambayo yanaruhusu maelfu ya watu kurejea kwenye nyumba zao zilizobomolewa katika ukanda wa Gaza, kuondolewa kwa vikosi vya mauaji ya halaiki ya Israel na kubadilishana mateka.
-
Mabinti barani Afrika watoa wito wa kuheshimiwa haki zao
Oct 13, 2025 06:24Mabinti barani Afrika wametoa mwito wa kuheshimiwa na kupatiwa kipaumbele haki zao za kimsingi. Wito huo umetolewa katika kongamano la kieneo la mabinti magharibi mwa Afrika. Imeelezwa kuwa, haki za mabinti Afrika ni sauti ambayo haiwezi tena kupuuzwa.