-
Gavana wa Darfur: Katika kipindi cha siku tatu tu, RSF iliua Wasudan 27,000 El-Fasher
Nov 26, 2025 10:51Gavana wa Jimbo la Darfur nchini Sudan, Minni Arko Minnawi, ameviambia vyombo vya habari kuwa, katika kipindi cha siku tatu tu Wasudan 27,000 waliuliwa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) wakati wanamgambo wa vikosi hivyo walipoendeleza wimbi la mauaji baada ya kuuteka mji wa el-Fasher mwishoni mwa mwezi uliopita.
-
UN: Tangazo la RSF la kusitisha mapigano ni 'hatua katika mwelekeo sahihi'
Nov 26, 2025 07:13Umoja wa Mataifa umekaribisha kwa tahadhari tangazo la kibinadamu la kusitisha mapigano lililotolewa jana na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), ukisema kuwa linawakilisha kupiga hatua lakini linahitaji kuidhinishwa kupitia hatua maidanini.
-
Rais wa Nigeria: Wanafunzi wa kike 24 waliotekwa nyara wiki jana wakombolewa
Nov 26, 2025 07:13Wanafunzi wa kike 24 waliokuwa wametekwa nyara kutoka katika shule yao ya bweni wiki iliyopita kaskazini magharibi mwa Nigeria wamekombolewa. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Rais.
-
Russia: Tupo tayari kuisaidia Nigeria katika mapambano dhidi ya ugaidi
Nov 26, 2025 07:12Maria Zakharova Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa nchi hiyo ipo tayari kusaidia na kuung amkono juhudu za nigeria za kupambana na ugaidi. Bi Zakharova aidha amepongeza jitihada kubwa za serikali ya Abuja za kukabiliana na makundi yenye misimamo mikali.
-
Wakuu wa usalama Nigeria waripoti maendeleo katika operesheni ya kuokoa wanafunzi waliotekwa nyara
Nov 25, 2025 07:29Maafisa wa jeshi la Nigeria wametangaza kuwa kumepigwa hatua nzuri za maenedelea katika jitihada za kukomboa mamia ya wanafunzi wa kike na walimu wao kadhaa waliotekwa nyara na kundi la watu waliokuwa na silaha katika jimbo la Niger, kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Hemedti atangaza kusitisha mapigano kwa upande mmoja, raia wanaendelea kukimbia makazi yao Sudan
Nov 25, 2025 06:39Kamanda wa waasi wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo “Hemedti”, ametangaza kusitisha mapigano ya ndani kwa kipindi cha miezi mitatu kwa "sababu za kibinadamu", ambako kunajumuisha kusitishwa uhasama; siku moja baada ya mkuu wa Baraza la Mpito la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, kukaataa pendekezo la Marekani kwa ajili ya kusitisha mapigano.
-
IEBC yawataka wanasiasa wa Kenya wasichochee machafuko na uvunjivu wa amani
Nov 25, 2025 06:34Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC), imewataka wanasiasa kuelekeza nguvu zao katika kuhimiza amani na utulivu, badala ya kutoa matamshi yanayoweza kuchochea taharuki miongoni mwa wananchi.
-
Familia za watoto waliotekwa nyara Nigeria zachanganyikiwa kutokana na kukaririwa vitendo hivyo mashuleni
Nov 25, 2025 02:43Familia za wanafunzi waliotekwa nyara nchini Nigeria zimenasa kati ya matumaini na kukatishwa tamaa kutokana na vitendo vya kukaririwa vya utekaji nyara wanafunzi wakiwa mashuleni.
-
Mamluki wa kigeni wana jukumu gani katika kuchochea vita nchini Sudan?
Nov 25, 2025 02:39Kamati ya Uchunguzi wa Haki za Binadamu imetangaza kuhusu ushirikiano uliopo kati ya mamluki wa kigeni na Vikosi vya Msaada wa Haraka vya Sudan RSF katika vita vya ndani nchini humo.
-
Al Burhan akataa pendekezo la Marekani, alitaja kuwa baya zaidi kwa ajili ya utatuzi wa mgogoro wa Sudan
Nov 24, 2025 15:24Mkuu wa Baraza la Utawala wa Mpito nchini Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, amekataa pendekezo lililowasilishwa na mshauri wa Rais wa Marekani kuhusu masuala ya Kiarabu na Afrika, Massad Boulos, juu ya utatuzi wa mgogoro wa Sudan.