-
Shambulio la RSF dhidi ya msafara wa misaada wa UN Kordofan Kusini, Sudan lauwa mtu 1 na kujeruhi 2
Sep 03, 2026 10:15Wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan wameshambulia msafara wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika jimbo la Kordofan Kusini, na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine wawili.
-
Umoja wa Afrika walaani hatua za kuvuruga amani nchini Niger
Sep 03, 2026 03:23Umoja wa Afrika (AU) umelaani jaribio la uasi wa kijeshi lililozimwa NCHINI Niger. Mwenyekiti wa Kamisheni ya umoja huo Mahmoud Ali Youssouf ameikosoa hatua hiyo na kuonya dhidi ya hatua yoyote ya kuchukua madaraka kwa kutumia nguvu.
-
Guinea-Bissau yapiga kura ya 'ndiyo' katika kura ya maoni ya katiba mpya
Sep 02, 2026 12:49Wapigakura nchini Guinea-Bissau wameidhinisha mabadiliko ya katiba kupitia kura ya maoni ambayo itampa rais mamlaka zaidi.
-
Ripoti: Gaddafi wa Libya alimuua Imamu Musa Sadr kwa kumpiga risasi mbili kifuani
Sep 02, 2026 02:46Aliyekuwa dikteta wa Libya, Muammar Gaddafi, anadaiwa kumpiga risasi mbili kifuani mwanazuoni mashuhuri wa Kiislamu kutoka Lebanon, Allamah Imamu Musa Sadr, baada ya Imamu kukosoa vikali kile kilichoitwa “Kitabu cha Kijani” (The Green Book) na kukitaja kuwa cha kipuuzi na kisicho na mashiko, huku akimueleza mwandishi wake kama mtu mwenye hitilafu ya kiakili. Ufichuzi huu umetolewa na mwanahistoria, mtafiti na mwanahabari maarufu wa Iraq, Dkt. Hamid Abdullah.
-
Watu 5 waliopona Ebola waruhusiwa kurejea nyumbani Kongo huku idadi ya maambukizi ikipindukia 6,000
Sep 01, 2026 14:15Watu watano waliopona ugonjwa wa Ebola jana waliruhusiwa kutoka katika kituo cha matibabu huko Béni, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Rais wa Algeria aamuru kutekelezwa adhabu ya kifo kwa wale wanaochoma moto misitu kimakusudi
Sep 01, 2026 03:09Rais wa Algeria aamuru kutekelezwa adhabu ya kifo kwa wale wanaochoma moto misitu kimakusudi
-
Wahamiaji waliofukuzwa na Trump na kupelekwa Afrika wasimulia sulubu walizokumbana nazo
Sep 01, 2026 03:08Wahamiaji kumi kutoka Marekani hadi Liberia wameliambia gazeti la The New York Times maelezo ya kutisha kuhusu miezi waliyotumia wakiwa kizuizini na safari ya saa 14 kwenda Afrika Magharibi, wakisema walipigwa, kufungwa minyororo na kutendewa vibaya, kabla ya baadhi yao kujikuta katika nchi ambazo hawana uhusiano nazo.
-
Umoja wa Afrika: Mapigano yanaendelea DRC licha ya makubaliano ya amani
Aug 31, 2026 11:58Umoja wa Afrika (AU) umetangaza kuwa, mapigano yanaendelea kushuhudiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo licha ya makubaliano yaliyosainiwa na michakato ya amani inayoendelea.
-
Sheikh Zakzaky: Vita dhidi ya Iran ni mwendelezo wa vita vilivyopiganwa dhidi ya Mtume Muhammad (SAW)
Aug 31, 2026 11:29Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria Sheikh Ibrahim Zakzaky, ameelezea vita vinavyoendelea, vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mhimili wa Muqawama kuwa ni mwendelezo wa vita vilivyowahi kupiganwa dhidi ya Mtume Muhammad (SAW) katika jaribio la kuzuia haki kutawala.
-
Kamati ya mazungumzo ya Libya yatia saini rasimu ya makubaliano ili kurekebisha muundo wa tume ya uchaguzi
Aug 31, 2026 04:36Kamati ndogo ya Mazungumzo ya Libya ya '4+4' jana Jumapili ilitangaza kuhusu kusainiwa rasimu ya makubaliano ya mwisho kwa lengo la kuifanyia marekebisho ya kimuundo Tume Kuu ya ya Taifa ya Uchaguzi ya nchi hiyo na kupitia upya sheria za uchaguzi.