-
Makumi wauawa katika mashambulizi pacha ya magaidi Nigeria
Feb 26, 2026 05:10Watu wasiopungua 25 wameuawa huku nyumba kadhaa zikichomwa moto baada ya watu wenye silaha kushambulia vijiji viwili katika Jimbo la Adamawa, kaskazini mashariki mwa Nigeria usiku wa kuamkia jana.
-
Waafrika 1,700 wadaiwa kushiriki katika vita vya Russia, Ukraine
Feb 26, 2026 04:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha amedai kwamba, zaidi ya Waafrika 1,700 wanapigana kwa niaba ya Russia katika vita vyake dhidi ya Ukraine, na kuongeza kwamba Moscow inatumia hadaa kuwasajili jeshini raia hao wa Kiafrika.
-
Tanzania yatoa tahadhari ya kuongezeka maambukizi ya mafua, Covid 19 na Dengue
Feb 26, 2026 03:44Wizara ya Afya ya Tanzania imetoa tahadhari ya afya kwa umma ya kuongezeka kwa maambukizi ya mafua na Uviko-19 na kuongezeka kwa hatari ya homa ya dengue, huku ikiwataka wananchi kuchukua hatua za haraka za kujikinga hasa katika kipindi cha msimu wa mvua.
-
Kampuni ya Mali yachukua vituo vya mafuta vya TotalEnergies
Feb 26, 2026 03:21Kampuni ya NDC Energie ya Mali imenunua takriban vituo 80 vya mafuta nchini Mali ambavyo awali vilikuwa vinaendeshwa na shirika la Ufaransa la TotalEnergies.
-
UN yalaani mashambulizi ya RSF huko Sudan, yataka vita vikomeshwe
Feb 25, 2026 09:23Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) limeelezea "wasiwasi mkubwa" kuhusu kuongezeka kwa ghasia na machafuko katika nchi iliyoathiriwa ba vita ya Sudan, hasa katika majimbo ya Darfur na Kordofan, likitaka mapigano yasitishwe mara moja.
-
Al-Burhan atoa fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa RSF watakaoweka silaha zao chini
Feb 25, 2026 06:59Mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, ametangaza fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) ikiwa wataweka silaha zao chini.
-
UN yatoa wito wa msaada wa dharura kwa wakimbizi wa Burundi waliopo na wanaorudi nchini
Feb 25, 2026 06:58Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, (UNHCR) limetangaza kuwa, ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi kwa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi, wakati huu ambapo kambi zinzowahifadhi zinakabiliwa na msongamano mkubwa na uhaba wa huduma muhimu.
-
Takriban watu milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioikumba Somalia
Feb 25, 2026 04:27Serikali ya Somalia na Umoja wa Mataifa zimetangaza kuwa wananchi wa Somalia wasiopungua milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioiathiri nchi hiyo.
-
Msemaji wa M23 auawa katika shambulio la droni mashariki mwa DRC
Feb 25, 2026 02:24Msemaji wa waasi wa M23 ameripotiwa kuuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Madagascar: Ushirikiano wetu na BRICS utatupa fursa mpya
Feb 25, 2026 02:24Rais wa mpito wa Madagascar, Michael Randrianirina amesema kwamba, nchi hiyo inatazama ushirikiano na jumuya ya BRICS kama njia ya kuelekea kwenye fursa mpya za kiuchumi na ushirikiano wa kimataifa.