-
Ghannouchi akataa kukata rufaa ya kifungo cha miaka 20 jela kutokana na "ukosefu wa dhamana ya haki"
Feb 04, 2026 07:21Rached Ghannouchi, mkuu wa harakati ya Ennahda na spika wa zamani wa Bunge la Tunisia, alitangaza jana Jumanne kwamba hatakata rufaa mahakamani dhidi ya hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela aliyokatiwa katika kile kinachojulikana katika vyombo vya habari kama "Kesi ya Kula Njama - 2," akisema kwamba kesi hiyo haina dhamana ya haki.
-
Abiy Ahmed: Ethiopia kuzindua chuo kikuu cha pili duniani cha AI mwaka 2027
Feb 04, 2026 07:18Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, jana alieleza kuwa Chuo Kikuu cha pili duniani kilichojikita katika akili mnemba (AI) kinatarajiwa kuzinduliwa nchini Ethiopia mwaka kesho wa 2027.
-
Makomando 4 walizima kamera na kumpiga risasi... Maelezo mapya yaibuka kuhusu mauaji ya Saif al-Islam Gaddafi
Feb 04, 2026 03:26Timu ya kisiasa ya Saif al-Islam Gaddafi, mtoto wa kiume wa kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi, imefichua kwamba mauaji yake yamefanywa na watu wanne wasiojulikana waliokuwa na silaha, ambao walivamia nyumba yake katika mji wa Zintan (kilomita 200 kusini-magharibi mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli) alasiri ya jana Jumanne.
-
Ethiopia yakanusha madai ya Trump kuwa Marekani ilifadhili mradi wa Bwawa la Renaissance
Feb 04, 2026 03:16Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, amesema kuwa nchi hiyo haikupokea “hata senti moja” kutoka kwa serikali yoyote ya kigeni kwa ajili ya kufadhili ujenzi wa Bwawa Kuu la Renaissance la Ethiopia (GERD), akikanusha madai ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kwamba Marekani imefadhili mradi huo.
-
Jeshi la Sudan lapata mafanikio katika vita dhidi ya waasi wa RSF
Feb 04, 2026 03:10Jeshi la Sudan limevunja mzingiro uliowekwa na waasi dhidi ya mji muhimu wa Kusini, Kadugli, Jumanne. Hayo yametangazwa na Rais wa mpito na Mkuu wa Jeshi la Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan.
-
Umoja wa Mataifa kutuma ujumbe wa kusimamia usitishaji mapigano nchini Congo DR
Feb 03, 2026 10:45Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imetangaza kwamba ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Congo utatuma timu yake ya kwanza kusimamia usitishaji mapigano kati ya serikali na muungano wa "Mto Kongo", (Alliance Fleuve Congo) kwa Kifaransa, unaojumuisha harakati ya M-23, katika siku zijazo.
-
Wakenya waendelea kujiunga na vita Ukraine licha ya maafa yanayowapata
Feb 03, 2026 10:18Uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya Wakenya wanaopigana katika vita vinavyoendelea huko Ukraine waliajiriwa kupitia maombi ya moja kwa moja na kampuni moja ya nchini Kenya, ambapo walitakiwa kurekodi video wakieleza nia yao ya kuajiriwa kama wanajeshi.
-
Nigeria yawafungulia mashtaka watu 9 kwa mauaji ya watu 150 mwaka jana huko Yelwata
Feb 03, 2026 08:07Waendesha mashtaka wamewafungulia mashtaka watu tisa kwa makosa ya ugaidi kuhusiana na moja ya mauaji mabaya zaidi yaliyojiri jimbo la Benue mnamo mwezi Juni mwaka jana. Mauaji hayo yalilenga pakubwa jamii ya Yelwata.
-
Taasisi ya Zuma yakadhibisha kuwa na uhusiano na Epstein; yasema ni kampeni chafu dhidi ya Jacob Zuma
Feb 03, 2026 08:01Taasisi ya Jacob Zuma imetoa taarifa kali baada ya jina la rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini kutajwa katika hati mpya za wazi mahakama zenye mfungamana na Jeffrey Epstein, mfadhili na mhusika wa kashfa za ngono aliyefia jela huko Marekani.
-
Ufaransa yashutumiwa kupanga kuangusha serikali pinzani barani Afrika
Feb 03, 2026 02:28Ufaransa inapanga “mapinduzi ya kikoloni mamboleo” katika mataifa mbalimbali ya Afrika kwa lengo la kuangusha serikali inazoziona kuwa “zisizohitajika,” hususan katika eneo la Sahel ambako imepata pigo kubwa katika miaka ya hivi karibuni. Shirika la Ujasusi wa Kigeni la Urusi (SVR) limedai.