-
Rais Samia: Russia inashiriki katika juhudi za maendeleo Afrika
Jun 11, 2026 03:06Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa Russia ina nia ya kusaidia Afrika kujenga mpangilio mpya wa uchumi wa dunia na inaendelea kujitolea kuunga mkono maendeleo ya bara hilo.
-
Ripoti: Watu 12 wauawa na 9 kujeruhiwa katika ufyatuaji risasi katika kitongoji cha Johannesburg
Jun 10, 2026 10:46Watu 12 wameuawa na wengine 9 kujeruhiwa katika ufyatuaji risasi katika makazi yasiyo rasmi katika kitongoji cha Cleveland jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.
-
Refa bora wa Kisomali aliyezuiwa kuingia Marekani alakiwa kishujaa nyumbani
Jun 10, 2026 10:43Omar Abdulkadir Artan mwamuzi mashuhuri wa kandanda kutoka Somalia amelakiwa kishujaa wakati alipowasili nchini humo hii leo baada ya kuzuiwa kuingia Marekani; uamuzi ambao umemzuia kuchezesha katika mashindano ya Kombe la Dunia la Kandanda la FIFA mwaka huu.
-
Uganda: Kizza Besigye apinga kuwekwa kizuizini katika kesi ya uhaini inayomkabili
Jun 10, 2026 03:46Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, amewasilisha ombi mahakamani akitaka kutolewe uamuzi wa kusimamisha kuendelea kushikiliwa kizuizini na kufunguliwa mashtaka.
-
Maandamano dhidi ya kituo cha kupambana na Ebola cha Marekani huko Kenya yageuka kuwa vurugu
Jun 09, 2026 13:42Polisi wa Kenya wametumia gesi ya kutoa machozi dhidi ya raia waliokuwa wakiandamana huko Nanyuki leo Jumanne kupinga kuanzishwa kituo cha karantini cha Marekani ndani ya kambi ya kijeshi ili kuwapokea raia wa Marekani wanaoshukiwa kuwa na Ebola.
-
Refa bora wa Afrika azuiwa kuingia Marekani licha ya kuteuliwa na FIFA kwa Kombe la Dunia
Jun 09, 2026 02:57Katika tukio jingine la kashfa siku chache kabla ya Kombe la Dunia 2026, mwamuzi mashuhuri kutoka Somalia, anayesifiwa sana kuwa miongoni mwa marefa bora zaidi barani Afrika, amezuiwa kuingia nchini Marekani.
-
Visa vya Ebola vyazidi 500 nchini DRC huku tahadhari ya kuenea zaidi ikitolewa
Jun 08, 2026 11:12Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imefikia 515, vikiwemo vifo 91, huku mamlaka za afya zikionya kuwa maambukizi bado yanaendelea na huenda visa vikazidi kuongezeka ikiwa hatua za udhibiti hazitaimarishwa haraka.
-
Ramaphosa atangaza hatua mpya kukabili uhamiaji haramu Afrika Kusini
Jun 08, 2026 11:10Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametangaza msururu wa hatua mpya zinazolenga kukabiliana na uhamiaji haramu, kufuatia kuongezeka kwa wasiwasi wa umma kuhusu suala hilo.
-
Nigeria: Mamia ya wanawake na watoto waliotekwa nyara na magaidi waachiliwa
Jun 08, 2026 03:12Mamia ya wanawake na watoto waliokuwa wametekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria wameachiwa huru mwishoni mwa wiki.
-
Raia 11 wauawa katika shambulio la droni sokoni Kordofan Kaskazini nchini Sudan
Jun 07, 2026 11:08Shambulio la ndege zisizo na rubani sokoni katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan limeua takriban raia 11 na kujeruhi makumi ya wengine.