-
DRC yajipanga kwa sensa ya kwanza ya kitaifa baada ya miaka 42
Aug 10, 2026 03:12Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) inajiandaa kufanya sensa yake ya kwanza ya kitaifa baada ya zaidi ya miongo minne, kazi kubwa inayolenga kuwapatia hadhi rasmi mamilioni ya raia ambao wameishi bila vitambulisho vya kitaifa vilivyotolewa na serikali.
-
Wanajeshi wasiopungua 10 wauawa katika shambulio katikati mwa Mali
Aug 10, 2026 03:09Wanajeshi wasiopungua 10 waliuawa jana Jumapili katika shambulio lililofanywa katika kambi ya jeshi katikati mwa Mali. Kundi moja la kigaidi lenye mfungamano na mtandano wa al Qaida limedai kuhusika na hujuma hiyo.
-
Mamia ya watu wanaandamana Afrika Kusini kupinga chuki dhidi ya wageni
Aug 09, 2026 11:04Mamia ya watu wameandmana katika miji mbalimbali nchini Afrika Kusini wakitaka kukomeshwa ghasia dhidi ya wahamiaji, ambazo zimewalazimisha makumi ya maelfu ya watu kukimbia nchi hiyo.
-
Wabunge Kenya: Hakuna makubaliano mapya ya ushirikiano wa kijeshi na Uingereza
Aug 09, 2026 10:20Wabunge wa Kenya wamesema kuwa hakuna makubaliano mapya yaliyofikiwa kati ya Kenya na Uingereza kuhusu mkataba wa ushirikiano wa kijeshi (BATUK).
-
Afrika Kusini yaadhimisha Maandamano ya Wanawake ya 1956 – mapambano ya uhuru bado yanaendelea
Aug 09, 2026 03:00Afrika Kusini, leo Jumapili, inaadhimisha miaka 70 tangu Maandamano ya Wanawake ya 1956, wakati wanawake wapatao 20,000 wa mbari na rangi zote walipoandamana hadi mji mkuu wa utawala, Pretoria, kupinga sheria za ubaguzi wa rangi zilizowalazimisha wanawake weusi kubeba vibali vilivyowazuia kutembea.
-
UN: Watoto zaidi ya 300 wamefariki dunia kwa Ebola tangu kuanza mlipuko huo huko Kongo
Aug 08, 2026 12:55Watoto zaidi ya 300 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola tangu mlipuko huo uliopoikumba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Idadi hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotangazwa jana Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq.
-
Wakulima wa Kenya wakanusha madai ya matumizi ya sianidi baada ya tembo 15 kufa huko Amboseli
Aug 08, 2026 02:43Wakulima wanaopakana na Hifadhi ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya wamekanusha kutumia sianidi baada ya tembo 15 kufariki dunia baada ya kudaiwa kuwa tembo hao wamekufa kutokana na sumu hiyo.
-
Mlipuko wa Ebola Kongo wapindukia maambukizi 4,000
Aug 08, 2026 02:42Idadi ya kesi za Ebola zilizothibitishwa hadi kufikia jana Ijumaa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikuwa zimepindukia 4,000 huku maeneo ya afya yaliyoathirika yakiongezeka.
-
Wabunge wa Uganda watilia shaka uamuzi wa serikali kutaka kupeleka wanajeshi Ghaza
Aug 07, 2026 12:27Baadhi ya wabunge wa upinzani nchini Uganda wametilia shaka uamuzi wa serikali wa kutaka kupeleka wanajeshi wa nchi hiyo huko Ukanda wa Ghaza watakaokuwa sehemu ya kikosi cha kimataifa cha kurejesha uthabiti katika eneo hilo la ardhi ya Palestina.
-
UNSC: Kundi la DAESH (ISIS) lingali ni tishio kubwa kwa usalama barani Afrika
Aug 07, 2026 03:35Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetahadharisha kuwa, kundi la kigaidi la ISIS (DAESH) lingali ni tishio kubwa kwa usalama wa kimataifa licha ya operesheni za kupambana na ugaidi zilizodhoofisha uongozi wake wa juu.