-
Tanzania yatoa tahadhari ya kuongezeka maambukizi ya mafua, Covid 19 na Dengue
Feb 26, 2026 00:14Wizara ya Afya ya Tanzania imetoa tahadhari ya afya kwa umma ya kuongezeka kwa maambukizi ya mafua na Uviko-19 na kuongezeka kwa hatari ya homa ya dengue, huku ikiwataka wananchi kuchukua hatua za haraka za kujikinga hasa katika kipindi cha msimu wa mvua.
-
Kampuni ya Mali yachukua vituo vya mafuta vya TotalEnergies
Feb 25, 2026 23:51Kampuni ya NDC Energie ya Mali imenunua takriban vituo 80 vya mafuta nchini Mali ambavyo awali vilikuwa vinaendeshwa na shirika la Ufaransa la TotalEnergies.
-
UN yalaani mashambulizi ya RSF huko Sudan, yataka vita vikomeshwe
Feb 25, 2026 05:53Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) limeelezea "wasiwasi mkubwa" kuhusu kuongezeka kwa ghasia na machafuko katika nchi iliyoathiriwa ba vita ya Sudan, hasa katika majimbo ya Darfur na Kordofan, likitaka mapigano yasitishwe mara moja.
-
Al-Burhan atoa fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa RSF watakaoweka silaha zao chini
Feb 25, 2026 03:29Mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, ametangaza fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) ikiwa wataweka silaha zao chini.
-
UN yatoa wito wa msaada wa dharura kwa wakimbizi wa Burundi waliopo na wanaorudi nchini
Feb 25, 2026 03:28Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, (UNHCR) limetangaza kuwa, ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi kwa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi, wakati huu ambapo kambi zinzowahifadhi zinakabiliwa na msongamano mkubwa na uhaba wa huduma muhimu.
-
Takriban watu milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioikumba Somalia
Feb 25, 2026 00:57Serikali ya Somalia na Umoja wa Mataifa zimetangaza kuwa wananchi wa Somalia wasiopungua milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioiathiri nchi hiyo.
-
Msemaji wa M23 auawa katika shambulio la droni mashariki mwa DRC
Feb 24, 2026 22:54Msemaji wa waasi wa M23 ameripotiwa kuuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Madagascar: Ushirikiano wetu na BRICS utatupa fursa mpya
Feb 24, 2026 22:54Rais wa mpito wa Madagascar, Michael Randrianirina amesema kwamba, nchi hiyo inatazama ushirikiano na jumuya ya BRICS kama njia ya kuelekea kwenye fursa mpya za kiuchumi na ushirikiano wa kimataifa.
-
Mwana wa Rais wa Uganda amuita 'Hitler' kiongozi wa RSF aliyekutana na baba yake hivi karibuni
Feb 24, 2026 07:43Mwana mtatanishi wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye ni mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Muhoozi Kainerugaba ametoa matamshi yasiyo ya kawaida katika kumshambulia kiongozi wa wanamgambo wa Sudan wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo ambaye hivi karibuni alikutana na baba yake huko nchini Uganda.
-
Afrika Kusini: Tutafuta zaidi ya viza 2,000 zilizotolewa kupitia mitandao ya rushwa
Feb 24, 2026 07:41Afrika Kusini inajiandaa kufuta zaidi ya viza 2,000 ambazo zimepatikana kwa njia isiyo sahihi, huku serikali ikiendesha msako mkali wa kupambana na rushwa ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani.