-
Tume ya kupambana na uhalifu wa kiuchumi Nigeria yafunga akaunti za serikali ya jimbo
Aug 07, 2026 03:34Tume ya kupambana na uhalifu wa kiuchumi na kifedha nchini Nigeria, Economic and Financial Crimes Commission (EFCC), imeagiza kufungwa akaunti za Serikali ya Jimbo la Osun la Kusini Magharibi mwa nchi hiyo, ikieleza wasiwasi wake kuhusu fedha za umma zinazohusishwa na uchunguzi unaoendelea wa madai ya ubadhirifu wa fedha karibu Naira bilioni 11 ($8,080,000).
-
Raia zaidi ya 300 waliotekwa nyara Nigeria waokolewa katika operesheni kubwa
Aug 06, 2026 11:02Nigeria imesema kuwa zaidi ya watu 300 waliotekwa nyara katika mashambulizi tofauti ya watu wenye silaha wameokolewa kupitia operesheni ya pamoja ya kiintelijensia na kiusalama.
-
Mbu vamizi azua hofu ya malaria kote barani Afrika
Aug 06, 2026 10:59Aina ya mbu vamizi inayoenea kwa kasi imezua hofu kote barani Afrika, huku wanasayansi wakionya kuwa inaweza kuchochea kuibuka upya kwa ugonjwa wa malaria katika miji mikubwa.
-
Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola DRC huku maambukizi yakienea
Aug 06, 2026 03:49Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kimefunguliwa wiki hii na wadau wa Umoja wa Mataifa ikiwa ni hatua inayolenga kuimarisha mwitikio dhidi ya mlipuko wa sasa wa virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo unaoendelea kuenea kwa kasi katika jimbo la Ituri, mashariki mwa taifa hilo.
-
Interpol: Akili Mnemba (AI) inatumika katika 55% ya uhalifu wa mtandaoni barani Afrika
Aug 06, 2026 03:43Ripoti ya karibuni ya Polisi ya Kimataifa, Interpol, kuhusu tishio la uhalifu wa mtandaoni barani Afrika kwa mwaka 2026 imetoa onyo kali kuhusu jinsi teknolojia ya Akili Mnemba (AI) inavyotumiwa kudhoofisha usalama wa kiuchumi na kijamii katika mataifa bara hilo.
-
Ruto asema serikali imetekeleza ahadi ilizowapa Waislamu wa Kenya
Aug 06, 2026 03:24Rais William Ruto wa Kenya amesema serikali imetekeleza ahadi muhimu ilizotoa kwa jamii ya Waislamu wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2022.
-
Africa CDC yatoa tahadhari kufuatia mlipuko wa Ebola Kongo kushindwa kudhibitiwa
Aug 05, 2026 12:08Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa barani Afrika ( AFRICA CDC) kimetahadharisha kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unazidi kuwa nje ya udhibiti, huku vifo zaidi ya 1,700 vikirekodiwa ndani ya wiki 14 pekee. Hii ni katika hali ambayo juhudi za kuwafuatilia watu waliotangamana na wagonjwa zimeshindwa kudhibiti msambao wa virusi hivyo.
-
Mapigano kati ya jeshi la Ethiopia na Tigray yapanuka hadi mpakani mwa Sudan
Aug 04, 2026 10:22Makabiliano ya kijeshi kati ya vikosi vya Serikali ya Shirikisho nchini Ethiopia na Kikosi cha Ukombozi wa Watu wa Tigray yanaongezeka baada ya siku kadhaa za mapigano, na sasa yanaripotiwa kupanuka hadi kwenye maeneo ya mpakani na Sudan.
-
WHO: DRC inakabiliwa na mlipuko mbaya zaidi wa Ebola katika historia
Aug 04, 2026 03:02Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kuwa mlipuko wa Ebola unaoendelea kusambaa kwa kasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ndio mkubwa zaidi kuwahi kuikumba nchi hiyo katika rekodi zake zote.
-
Rais wa Somalia: Tutazuia Israel kuimarisha ushawishi wake Somaliland
Aug 03, 2026 11:10Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud, amesema kwamba Serikali ya Shirikisho itachanganya "nguvu na hekima" ili kuzuia "Israel" kupata nafasi au kuanzisha ushawishi wa kudumu katika eneo la "Somaliland," akisisitiza kwamba Mogadishu ingali inashikamana na umoja wa ardhi na mamlaka ya Somalia, na inapinga kwa nguvu zote kuhamisha migogoro ya "Mashariki ya Kati" hadi eneo la Pembe ya Afrika.