-
Waziri Mkuu wa zamani na mkongwe wa siasa za Kenya Raila Odinga afariki dunia akiwa matibabuni India
Oct 15, 2025 07:57Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga amefariki dunia leo asubuhi huko Koothattukulam, wilayani Ernakulam nchini India, baada ya kupata mshtuko wa moyo wakati anafanya matembezi yake ya kila asubuhi.
-
Ruto: Kuondolewa viza Afrika kutatatua changamoto za bara hilo
Oct 10, 2025 06:35Rais William Ruto wa Kenya ameahidi kuongoza juhudi za kuondoa masharti ya viza kwa Waafrika na kutatua mizozo inayokumba bara hilo.
-
Kenya yawahakikishia raia wake wanaofanya biashara Tanzania: Hamtaguswa na agizo jipya la leseni
Oct 03, 2025 10:35Serikali ya Kenya imewahakikishia raia wake wanaofanya biashara nchini Tanzania kwamba hawataguswa na agizo jipya la leseni lililotolewa hivi karibuni na serikali ya Tanzania.
-
Rais wa Kenya atoa hotuba kali UNGA, asema mabadiliko ya Baraza la Usalama si 'kuifanyia fadhila Afrika'
Sep 25, 2025 06:41Rais wa Kenya William Ruto ametoa hotuba kali katika kikao cha 80 cha Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York siku ya Jumatano.
-
Wakenya 66,000 kupoteza ajira ikiwa makubaliano ya AGOA hayatatazamwa upya
Sep 08, 2025 12:22Sheria ya Ukuaji na Fursa Barani Afrika (AGOA) inatazamiwa kumalizika muda wake ifikapo tarehe 30 mwezi huu wa Septemba, na hivyo kuhitimisha mpango muhimu wa biashara bila ushuru kati ya Kenya na Marekani.
-
Watu wa Afrika walaani jinai za utawala wa Israel dhidi ya Yemen na Gaza
Sep 05, 2025 10:24Wananchi wa nchi kadhaa za Afrika wamefanya maandamano makubwa kulaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Yemen na Gaza, wakionesha mshikamano wa wazi na harakati za ukombozi wa Wapalestina.
-
DRC yapinga kupelekwa balozi mdogo wa Kenya mjini Goma
Aug 17, 2025 11:37Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imepinga hatua ya Kenya ya kumteua balozi mdogo anayetazamiwa kutumwa katika mji wa Goma ulioko mashariki mwa DRC, ikiuelezea uamuzi huo kuwa "usiofaa".
-
IPOA yafichua: Polisi wa Kenya waliua watu 65 katika maandamano Juni, Julai
Jul 25, 2025 05:44Ripoti mpya ya Mamlaka Huru ya Kuchunguza Utendakazi wa Polisi (IPOA) imefichua kwamba watu 65 walipoteza maisha, 41 kati yao kwa kupigwa risasi na maafisa wa polisi, huku raia 342 wakijeruhiwa vibaya wakati wa maandamano ya Juni 25 na Julai 7 mwaka huu dhidi ya serikali ya Rais William Ruto wa Kenya.
-
Kaunti za Busia, Bungoma na Kakamega nchini Kenya zathibitisha maambukizo ya ugonjwa wa Mpox
Jul 23, 2025 12:07Magharibi mwa Kenya sasa ndio kitovu cha mlipuko wa ugonjwa wa Mpox huku kaunti za Busia, Bungoma na Kakamega nchini humo zikithibitisha kuwa na wagonjwa kadhaa walioambukizwa ugonjwa huo unaosababishwa na virusi.
-
Mwanaharakati wa haki za binadamu Kenya aachiwa kwa dhamana, ashtakiwa kwa kumiliki silaha kinyume cha sheria
Jul 21, 2025 13:38Boniface Mwangi, mwanaharakati wa haki za binadamu wa Kenya ambaye amekuwa na nafasi kuu katika maandamano dhidi ya serikali, ameachiwa huru kwa dhamana leo Jumatatu baada ya kushtakiwa kwa kupatikana na gesi ya kutoa machozi na silaha nyumbani kwake.