-
Safari ya kwanza ya Rais wa Iran barani Afrika baada ya miaka 11
Jul 10, 2023 22:56Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Jumanne ya leo ameondoka nchini kuelekea barani Afrika kwa ziara ya siku tatu ya kuzitembelea nchi za Kenya, Uganda na Zimbabwe.
-
Siku 500 za vita huko Ukraine na mustakbali wake
Jul 10, 2023 09:30Vita vya Ukraine vimepitisha siku 500 tangu kuanza na hakuonekani matarajio ya kumalizika vita hivyo vya umwagaji damu barani Ulaya. Vita hivyo ambavyo awali ilidhaniwa kwamba huwenda vingechukua muda mfupi na kumalizka haraka, sasa vimekuwa mapigano ya kijeshi ya muda mrefu na ya umwagaji damu.
-
Mzigo mzito wa gharama za kiuchumi ambao serikali ya Erdogan inawabebesha Waturuki
Jul 09, 2023 23:13Serikali ya Recep Tayyip Erdoğan imeongeza kodi inazowatoza wananchi wa Uturuki ili kuongeza mapato yake sambamba na kukabiliana na hali mbaya ya uchumi inayoikabili nchi hiyo.
-
Mashauriano ya kirafiki yanayotawala katika uhusiano wa Iran na Algeria
Jul 09, 2023 04:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria Ahmed Attaf, ambaye amekuwa ziarani hapa nchini kwa mwaliko wa Hossein Amir-Abdollahian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ametoa matamshi ya kirafiki na ya heshima sana kuhusu uhusiano wa Algeria na Iran katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari aliofanya na mwenyeji wake.
-
Umoja wa Mataifa wataka kuondolewa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran
Jul 08, 2023 23:08Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Kisiasa, amehutubia kikao cha Baraza la Usalama cha kukagua utekelezwaji wa azimio nambari 2231, na kuelezea kuwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ndio chaguo bora zaidi la kuhakikisha "hali ya amani ya mpango wa nyuklia wa Iran."
-
NAM yasisitiza ulazima wa kulindwa haki za watu wa Palestina
Jul 08, 2023 10:48Mawaziri wa mambo ya nje wa Vuguvugu la Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM), wameeleza katika taarifa ya mwisho ya mkutano ulofanyika katika mji mkuu wa Jamhuri ya Azerbaijan, Baku, kwamba kuna haja ya kufanyika juhudi zaidi kimataifa za kutafuta njia ya ufumbuzi wa kiuadilifu utakaohakikisha Wapalestina wanarejeshewa haki zao.
-
Tahadhari ya China kuhusu uingiliaji wa nchi za Magharibi katika masuala ya ndani ya nchi nyingine
Jul 07, 2023 23:07Rais wa China, Xi Jinping, ametoa wito kwa nchi mbalimbali kusimama dhidi ya "mapinduzi ya rangi ya nchi za Magharibi". Jinping ametoa wito huo katika mkutano Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai, uliofanyika kwa njia ya mtandao.
-
Ripoti yenye malengo maalumu ya Baraza la Haki za Kibinadamu dhidi ya Iran sambamba na ghasia za Ufaransa
Jul 07, 2023 04:07Kamati eti ya kutafuta ukweli iliyoundwa na Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa kuhusu Iran imetoa ripoti yake ya awali kuhusu kile ilichokiita 'ukandamizaji wa Iran dhidi ya maandamano ya nchi nzima'.
-
Utawala wa Israel umeambulia patupu katika jinai zake dhidi ya Wapalestina huko Jenin
Jul 06, 2023 23:37Oparesheni ya kikatili ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina huko Jenin katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan imemalizika baada ya siku 2, na kwa mujibu wa Wazayuni, operesheni hiyo haijafanikiwa chochote.
-
Kuendelea maandamano nchini Ufaransa; Macron aweka vikwazo dhidi ya mitandao ya kijamii
Jul 06, 2023 05:35Zaidi ya wiki moja imepita tangu maandamano yaanze huko Ufaransa na sasa serikali ya nchi hiyo ya Ulaya imeweka ksheria kali dhidi ya mitandao ya kijamii. Kuhusiana na hilo, viongozi wa Ufaransa wameituhumu mitandao ya kijamii ya Tik Tok, Snapchat na majukwaa mengine ya kijamii kuwa inachochea machafuko ambayo yameenea nchini baada ya afisa mmoja wa polisi kumpiga risasi na kumuua kijana mwenye umri wa miaka 17.