Kampuni ya Iran yazalisha bendeji za EB ZA ugonjwa adimu wa ngozi
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i108100-kampuni_ya_iran_yazalisha_bendeji_za_eb_za_ugonjwa_adimu_wa_ngozi
Kampuni ya kimaarifa ya kimatibabu ya Iran imeweza kuzalisha bendeji maalumu kwa wagonjwa wanaougua ugonjwa wa ngozi wa Epidermolysis Bullosa (EB), ugonjwa adimu wa kurithi ambao husababisha ngozi kuwa tete na kujeruhiwa kwa urahisi.
(last modified 2026-04-19T09:26:01+00:00 )
Feb 07, 2024 07:21 UTC
  • Kampuni ya Iran yazalisha bendeji za EB  ZA ugonjwa  adimu wa ngozi

Kampuni ya kimaarifa ya kimatibabu ya Iran imeweza kuzalisha bendeji maalumu kwa wagonjwa wanaougua ugonjwa wa ngozi wa Epidermolysis Bullosa (EB), ugonjwa adimu wa kurithi ambao husababisha ngozi kuwa tete na kujeruhiwa kwa urahisi.

Mafanikio hayo ni ya wataalamu wa Kampuni ya Teba Zist Polymer yenye msingi wa maarifa au knowledge based, ambayo ni mzalishaji wa kwanza wa bendeji hizo za kipekee za   majeraha nchini Iran. Mafanikio hayo yamepatikana licha ya vikwazo vya muda mrefu vya nchi za Magharibi dhidi ya uagizaji wa vifaa vya matibabu na bidhaa za dawa nchini humo.

Kulingana na Idara ya Sayansi, Teknolojia, na Uchumi unaotegemea Maarifa, kampuni hiyo ya Iran imeweza kupata mbinu sawa na ile inayotumiwa na shirika la Mepilex ya Uswidi. Bendeji hiyo imezingatia  miongozo ya kimataifa inayopendekezwa kwa wagonjwa wa EB na majeraha yao.

Kampuni ya Teba Zist Polymer inakusudia kuzalisha bendeji hiyo kwa wingi na jina lake la kibiashara ni , Tebaflex. Uzalishaji wa bendeji hiyo  utaboresha hali ya afya ya wagonjwa wa EB nchini.

Vidonda vya wagonjwa wa EB huchukuliwa kuwa sugu na wale wanaougua ugonjwa huu adimu wa ngozi wanapaswa kutumia bendeji maalumu ya povu ili isishikane  majeraha na kusababisha uharibifu zaidi kwa malengelenge yao na ngozi nyeti.

Kutokana na vikwazo vya kikatili dhidi ya Iran vilivyoongozwa na Marekani, Sweden ilikataa kuiuzia Iran bendeji maalumu za Mepilex kwa wagonjwa wa EB. Ukosefu wa bendeji mbadala zinazofaa umepelekea kupoteza maisha ya watoto kadhaa wanaosumbuliwa na EB.

Ijapokuwa Washington na washirika wake wa Magharibi wanadai kuwa bidhaa za kibinadamu hazijawekewa vikwazo, makumi ya maelfu ya wagonjwa nchini Iran kwa miaka mingi wamekufa au kupata maradhi sugu kutokana na kutopatikana kwa dawa muhimu.