May 20, 2018 02:21
Muungano wa As- Sairun unaoongozwa na Muqtada Sadr umeibuka mshindi katika uchaguzi wa bunge uliofanyika hivi karibuni nchini Iraq kwa kupata viti 54 vya uwakilishi bungeni huku muungano wa Fat-h unaoongozwa na Hadi al Amiri Katibu Mkuu wa Taasisi ya Badr ukinyakua viti 47 na muungano wa An- Nasr unaoongozwa na Waziri Mkuu Haidari al Abadi ukipata viti 42.