Jan 21, 2024 07:47
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelikosoa Baraza la Usalama la umoja huo kwa kutokuwa na mwakilishi wa kudumu kutoka Afrika. Guterres amehoji katika ukurasa wake wa X kwamba: "Je, tunawezaje kukubali kwamba Afrika haina hata mwanachama mmoja wa kudumu katika Baraza la Usalama?"