-
HAMAS yapongeza jitihada za kupokonywa Israel uanachama wa AU
Oct 18, 2021 00:23Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imepongeza na kuunga mkono jitihada zinazoendelea za kuupokonya utawala wa Kizayuni wa Israel kibali cha kuwa mwanachama mtazamaji wa Umoja wa Afrika (AU).
-
Faki Mahamat: Utegemezi unatishia uhuru wa kujitawala AU
Oct 15, 2021 00:49Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amesema mataifa ya bara hilo yanapaswa kushirikiana na kufanya kazi pamoja, ili kuhakikisha kuwa yanaondokana na utegemezi na vilevile yanajikomboa kifedha.
-
AU yaunga mkono kuundwa kikosi cha pamoja nchini Somalia
Oct 12, 2021 04:37Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limetangaza kuunga mkono pendekezo la kuundwa kikosi cha pamoja cha Umoja wa Mataifa nchini Somalia, kitakachochukua nafasi ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini humo (Amisom), iwapo wazo hilo litapasishwa.
-
Russia: Matatizo ya bara la Afrika inapasa yatatuliwe na viongozi wa nchi za Afrika
Oct 07, 2021 23:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema, matatizo ya baraza la Afrika inapasa yatatuliwe na viongozi wa nchi za Afrika na akaongeza kwamba Russia inaweza kuandaa mazingira ya kuwekwa askari wa kulinda amani barani humo.
-
Kesi za Corona barani Afrika zapungua kwa asilimia 13
Oct 07, 2021 21:19Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa cha Afrika (Africa CDC) kimesema bara la Afrika limeshuhudia kupungua kwa maambukizo ya ugonjwa wa COVID-19 katika kipindi cha wiki moja.
-
Kesi za Corona barani Afrika zapindukia milioni 8 na laki 3
Oct 05, 2021 04:34Kesi zilizothibitishwa za maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 katika nchi 55 za Kiafrika hadi kufikia jana Jumatatu zimepindukia watu milioni nane na laki tatu.
-
WHO: Asilimia 4 tu ya Waafrika ndio waliopata chanjo ya corona
Sep 30, 2021 08:24Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, nchi 14 za Afrika pekee ndizo zilizokuwa zimetoa chanjo ya corona kwa zaidi ya asilimiia 10 ya jamii zao hadi kufikia mwishoni mwa mwezi uliopita wa Septemba.
-
WHO yatahadharisha kuhusu aina mpya ya maambukizi ya kirusi cha corona Afrika
Sep 24, 2021 08:08Wanasayansi na wasomi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) wametahadharisha kuhusu mambukizo mapya ya kirusi cha corona katika miezi ya mwisho ya mwaka huu barani Afrika.
-
Mwenyekiti wa AU ataka Afrika iwe na kiti cha uanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la UN
Sep 22, 2021 09:14Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambaye ni mwenyekiti sasa wa Umoja wa Afrika AU amewasilisha malalamiko kadhaa ya bara hilo katika mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ulioanza jana mjini New York, likiwemo la bara la Afrika kupatiwa uanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la UN.
-
Wafanyamapinduzi Guinea wakataa wito wa kuachia madaraka, wasema hawababaishwi na vikwazo
Sep 19, 2021 12:04Kundi la wanajeshi waliotwaa madaraka ya nchi huko Guinea kupitia mapinduzi limepinga mashinikizo ya kimataifa yanayotaka kuachiliwa huru rais wa zamani wa nchi hiyo aliyeshikiliwa kizuizini, Alpha Conde na kurejeshwa kwa utawala wa kiraia.