-
Wachimba migodi haramu wasiopungua 14 wamepoteza maisha mgodini Afrika Kusini
Aug 11, 2026 11:22Polisi ya Afrika Kusini leo imetangaza kuwa wachimbaji wadogo wa madini wasiopungua 14 wamefariki dunia na wengine wengi kujeruhiwa katika mgodi ambao hautumiki nchini humo.
-
Mamia ya watu wanaandamana Afrika Kusini kupinga chuki dhidi ya wageni
Aug 09, 2026 11:04Mamia ya watu wameandmana katika miji mbalimbali nchini Afrika Kusini wakitaka kukomeshwa ghasia dhidi ya wahamiaji, ambazo zimewalazimisha makumi ya maelfu ya watu kukimbia nchi hiyo.
-
Waghana waiomba ICC kuchunguza ukatili wa chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini
Jul 24, 2026 02:48Raia wawili wa Ghana wamewasilisha ombi kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wakiitaka kufungua uchunguzi wa awali kuhusu vitendo vya ukatili vinavyowalenga wageni nchini Afrika Kusini, wakisema kwamba muundo, ukubwa na kukaririwa mashambulizi yanayowalenga wahamiaji vinaweza kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.
-
Raia wa Zimbabwe warejea nyumbani kutoka Afrika Kusini huku ghasia dhidi ya wahamiaji zikiendelea
Jul 13, 2026 03:03Raia wa Zimbabwe wanaokimbia vurugu na vitisho vya chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini wamewasili katika kituo cha mapokezi katika mji wa mpakani wa Beitbridge, Zimbabwe.
-
Nigeria na Afrika Kusini zavutana kwa kifo cha raia katika seli za polisi
Jul 09, 2026 11:36Polisi ya Afrika Kusini imethibitisha kuwa kifo cha raia wa Nigeria akiwa korokoroni hakikutokana na maandamano dhidi ya wahamiaji wa kigeni nchini humo yaliyofanyika wiki iliyopita.
-
Ghasia dhidi ya wahamiaji Afrika Kusini zatarajiwa leo
Jun 30, 2026 03:42Afrika Kusini inakabiliwa na mtihani mkubwa wa kiusalama baada ya magenge ya wahalifu kuapa kuwatimu raia wa kigeni nchini humo kuanzia leo.
-
Afrika Kusini yaapa kukabiliana vikali na ukatili dhidi ya wahamiaji
Jun 26, 2026 11:10Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ameapa kukabiliana na jaribio lolote la kuyumbisha taifa wakati wa maandamano yaliyopangwa kufanywa wiki ijayo dhidi ya wahamiaji, huku wimbi la chuki dhidi ya wageni lizidi kuongezeka nchini humo.
-
Serikali ya Afrika Kusini yasema imewarejesha nyumbani wageni 2,745 ndani ya wiki moja
Jun 15, 2026 12:20Afrika Kusini imewarejesha nyumbani wageni 2,745 katika wiki moja baada ya Rais Cyril Ramaphosa kuapa kuchukua hatua kali dhidi ya uhamiaji haramu.
-
Ripoti: Watu 12 wauawa na 9 kujeruhiwa katika ufyatuaji risasi katika kitongoji cha Johannesburg
Jun 10, 2026 10:46Watu 12 wameuawa na wengine 9 kujeruhiwa katika ufyatuaji risasi katika makazi yasiyo rasmi katika kitongoji cha Cleveland jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.
-
Ramaphosa: Waafrika Kusini si wachukia wageni
Jun 05, 2026 02:57Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, amemweleza mwenzake wa Kenya, Rais William Ruto, kwamba maandamano ya hivi karibuni dhidi ya uhamiaji haramu nchini humo hayamaanishi kuwa Waafrika Kusini wana chuki dhidi ya wageni.