-
ANC yamkosoa Mfalme wa Afrika Kusini kwa kuwaalika maafisa wa Israel
Feb 04, 2026 10:23Chama tawala cha African National Congress (ANC) kimemkosoa vikali Mfalme wa Afrika Kusini, Buyelekhaya Dalindyebo kufuatia uamuzi wake tata wa kuwaalika maafisa kutoka Ubalozi wa Israel kutembelea hospitali za umma katika mkoa wa Eastern Cape. Dalindyebo ni mfalme wa watu wa AbaThembu, mojawapo ya jamii kubwa zaidi za kitamaduni za Afrika Kusini.
-
Taasisi ya Zuma yakadhibisha kuwa na uhusiano na Epstein; yasema ni kampeni chafu dhidi ya Jacob Zuma
Feb 03, 2026 08:01Taasisi ya Jacob Zuma imetoa taarifa kali baada ya jina la rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini kutajwa katika hati mpya za wazi mahakama zenye mfungamana na Jeffrey Epstein, mfadhili na mhusika wa kashfa za ngono aliyefia jela huko Marekani.
-
DA yakanusha madai ya Trump ya kuwepo mauaji ya Wazungu A/Kusini
Jan 24, 2026 02:48Kiongozi wa chama cha Democratic Alliance cha Afrika Kusini (DA), John Steenhuisen amekadhibisha madai ya kuwepo "mauaji ya kimbari ya Wazungu" nchini Afrika Kusini.
-
Afrika Kusini yatangaza janga la kitaifa kufuatia mvua na mafuriko yaliyouwa watu 30
Jan 19, 2026 11:35Afrika Kusini imetangaza janga la kitaifa kutokana na mvua kubwa na mafuriko ambayo yamesababisha vifo vya takriban watu 30 kaskazini mwa nchi hiyo, kuharibu maelfu ya nyumba na kusomba barabara na madaraja.
-
Mafuriko yasababisha vifo vya watu 10 Afrika Kusini, na kusababisha kufungwa Hifadhi ya Kruger
Jan 16, 2026 07:14Mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa kaskazini-mashariki mwa Afrika Kusini yamesababisha vifo vya watu 10 kwa usiku mmoja na kupelekea kufungwa kwa Hifadhi ya Taifa ya Kruger.
-
ANC yaonya kuhusu njama za 'mapinduzi' nchini Iran
Jan 16, 2026 02:13Mkuu wa vuguvugu la Mshikamano wa Kimataifa wa chama tawala cha African National Congress (ANC) katika jimbo la Western Cape nchini Afrika Kusini ameonya kwamba, machafuko ya hivi karibuni nchini Iran yana mkono wa Marekani na washirika wake wa Kizayuni.
-
Afrika Kusini: Hatutazuia mpango wa Washington wa kuwapa hifadhi wazungu waliowachache
Jan 08, 2026 13:03Afrika Kusini imesema haitapinga mpango wenye utata wa serikali ya Washington wa kuwapeleka Marekani raia wazungu walio wachache wa Afrika Kusini.
-
Afrika Kusini yataka UN iitishe kikao cha dharura kufuatia mashambulizi ya Marekani dhidi ya Venezuela
Jan 04, 2026 03:01Afrika Kusini imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuitisha kikao cha dharura kufuatia mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Venezuela, na kukamatwa Rais wa nchi hiyo Nicholas Maduro na mkewe.
-
Kisu cha ngariba; Vijana 41 waaga dunia Afrika Kusini wakipashwa tohara
Dec 31, 2025 10:17Takriban vijana 41 wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na taratibu 'zisizofaa' za upashaji tohara nchini Afrika Kusini mwezi Novemba na Desemba mwaka huu unaomalizika wa 2025, mamlaka za nchi hiyo zilitangaza hayo jana Jumanne.
-
Makundi ya kiraia A/Kusini yataka kupewa dhamana wanaharakati wa Palestina waliogoma kula katika jela za UK
Dec 23, 2025 08:08Makundi kadhaa ya kiraia nchini Afrika Kusini yametoa wito yakitaka kupewa dhamana haraka iwezekanavyo wanaharakati wawili watetezi wa Palestina waliogoma kula katika jela za Uingereza yakisema kuwa kuendelea kufungwa raia hao kunahatarisha maisha yao.