-
Afrika Kusini: Hatutazuia mpango wa Washington wa kuwapa hifadhi wazungu waliowachache
Jan 08, 2026 13:03Afrika Kusini imesema haitapinga mpango wenye utata wa serikali ya Washington wa kuwapeleka Marekani raia wazungu walio wachache wa Afrika Kusini.
-
Afrika Kusini yataka UN iitishe kikao cha dharura kufuatia mashambulizi ya Marekani dhidi ya Venezuela
Jan 04, 2026 03:01Afrika Kusini imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuitisha kikao cha dharura kufuatia mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Venezuela, na kukamatwa Rais wa nchi hiyo Nicholas Maduro na mkewe.
-
Kisu cha ngariba; Vijana 41 waaga dunia Afrika Kusini wakipashwa tohara
Dec 31, 2025 10:17Takriban vijana 41 wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na taratibu 'zisizofaa' za upashaji tohara nchini Afrika Kusini mwezi Novemba na Desemba mwaka huu unaomalizika wa 2025, mamlaka za nchi hiyo zilitangaza hayo jana Jumanne.
-
Makundi ya kiraia A/Kusini yataka kupewa dhamana wanaharakati wa Palestina waliogoma kula katika jela za UK
Dec 23, 2025 08:08Makundi kadhaa ya kiraia nchini Afrika Kusini yametoa wito yakitaka kupewa dhamana haraka iwezekanavyo wanaharakati wawili watetezi wa Palestina waliogoma kula katika jela za Uingereza yakisema kuwa kuendelea kufungwa raia hao kunahatarisha maisha yao.
-
Ufyatuaji risasi Afrika Kusini; watu wenye silaha waua 9 karibu na Johannesburg
Dec 21, 2025 07:43Watu waliokuwa na silaha, usiku wa kuamkia leo, wamefyatua risasi kiholela katika kitongoji kimoja karibu na Johannesburg nchini Afrika Kusini na kuua takriban watu 9 na kujeruhi wengine kadhaa.
-
Rais wa Afrika Kusini amtuhumu Trump kwa kutoa 'kauli zisizo za kweli' kuhusu nchi yake
Dec 01, 2025 03:07Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini jana alimtuhumu Rais Donald Trump wa Marekani kwa kuendelea kutoa "taarifa zisizo za kweli" kuhusu nchi yake.
-
Kwa nini Macron anaamini kuwa G20 inakaribia kuporomoka?
Nov 24, 2025 07:54Katika ufunguzi wa mkutano wa kilele wa G20 mjini Johannesburg, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alisema katika hotuba isiyo ya kawaida kuwa kundi hilo limepoteza uwezo wake wa kutatua migogoro ya kimataifa.
-
Marekani yabatilisha viza ya waziri wa zamani wa Afrika Kusini aliyefanikisha kesi ya ICJ dhidi ya Israel
Nov 23, 2025 07:01Marekani imefuta viza ya waziri wa zamani wa Mahusiano ya Kimataifa wa Afrika Kusini Naledi Pandor mapema wiki hii, katika kile kinachoonekana kama hatua za hivi karibuni za Washington za kuiadhibu Pretoria kwa sababu kuuburuza utawala wa kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwa mauaji ya kimbari uliyofanya dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
-
Afrika Kusini yasema haitakabidhi kwa balozi mdogo wa Marekani urais wa G20 wa 2026
Nov 22, 2025 03:27Msemaji wa Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Vincent Magwenya amesema, kiongozi huyo hatomkabidhi balozi mdogo wa Marekani urais wa mkutano wa G20 kwa mwaka 2026 baada ya Marekani kusisitiza kuwa haitohudhuria mkutano huo rasmi jijini Johannesburg.
-
Kwa nini Afrika Kusini imedhamiria kufuatilia kesi ya mauaji ya halaiki huko Gaza?
Nov 19, 2025 02:12Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa, itaendelea kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwa tuhuma za kutenda mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.