-
Afrika Kusini yazika miili 30 iliyotelekezwa kwenye mgodi wa dhahabu
Jun 11, 2025 07:19Afrika Kusini jana Jumanne ilifanya maziko ya kwanza ya 'kimaskini' ya miili 30 ambayo haikuchukuliwa na jamaa zao, baada ya kupatikana kwenye mgodi wa dhahabu uliotelekezwa huko Stilfontein, mkoa wa Kaskazini Magharibi mwezi Januari mwaka huu.
-
Afrika Kusini yaanza kuchunguza jinai za enzi za 'apartheid'
May 31, 2025 10:45Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amemteua Jaji mstaafu wa Mahakama ya Kikatiba, Sisi Khampepe kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ukweli na Maridhiano (TRC) ya kuchunguza ucheleweshaji wa mashtaka na uchunguzi wa jinai zilizofanyika enzi za ubaguzi wa rangi (apartheid) nchini humo.
-
Kwa nini Trump anasema uongo kuhusu mauaji ya watu weupe nchini Afrika Kusini?
May 26, 2025 06:01Senzo Mchunu, Waziri wa Polisi wa Afrika Kusini amefichua uongo wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu mauaji ya wakulima wa kizungu nchini Afrika Kusini, na kusema: "Katika robo ya kwanza ya mwaka huu, jumla ya mauaji sita yanayohusiana na ardhi yalitokea Afrika Kusini, ambapo watano kati yao walikuwa watu weusi."
-
Waafrika Kusini wamjia juu Trump kwa kuongopa kwenye kikao na Ramaphosa
May 23, 2025 11:55Wananchi wa Afrika Kusini wameeleza kughadhabishwa na madai ya uwongo yaliyobuliwa na Rais wa Marekani Donald Trump wakati wa mazungumzo yake na Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini katika Ikulu ya White House.
-
Je, kwa nini Trump amenyamazia kimya mauaji ya kimbari huko Gaza, huku akidai yametokea Afrika Kusini?
May 23, 2025 05:57Akizungumza siku ya Jumatano katika kikao chenye mvutano na Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Rais Donald Trump wa Marekani alichukua hatua ya kushanga kwa kumuonyesha video ya kiongozi mmoja wa mrengo wa kulia wa Afrika Kusini aliyetoa wito wa kuuawa wakulima weupe ili kuthibitisha madai yake kuhusu kile kinachodaiwa kuwa mauaji ya kimbari dhidi ya wazungu wa nchi hiyo.
-
Kutoweza Afrika Kusini kuachana na Muqawama na ukombozi wa Palestina
Apr 25, 2025 07:17Tarehe 29 Disemba 2023 imerekodiwa katika kumbukumbu za historia ya baada ya mwaka 1994 ya Afrika Kusini kama siku muhimu sana baada ya Pretoria kufungua kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika mahakama ya ICJ, ikiwasilisha hoja za kisheria za kina na zenye mashiko kwamba ukatili wa Israel katika Ukanda wa Ghaza unakanyaga Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia Mauaji ya Kimbari.
-
Pandor ahimiza mageuzi ya kimataifa kutekeleza uamuzi wa ICJ kuhusu Gaza
Apr 23, 2025 02:12Naledi Pandor Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini amesema kuwa kushindwa kusitishwa mashambulizi na mauaji ya kimbari ya Israel katika Ukanda wa Gaza kumefichua mapungufu ya mifumo ya kisheria ya kimataifa na kuibua upya wito kuhusu udharura wa kufanyika mageuzi katika Umoja wa Mataifa.
-
A/Kusini: Russia ni mshirika wetu mkuu katika sekta ya anga za mbali
Apr 15, 2025 03:14Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Kitaifa la Anga za Mbali la Afrika Kusini (SANSA) amesema Russia ni mshirika mkuu wa Afrika Kusini katika kuendeleza mipango yake ya kitaifa ya anga za juu.
-
Marekani yamfukuza Balozi wa Afrika Kusini kwa 'kujieleza'
Mar 15, 2025 07:11Msuguano baina ya Marekani na Afrika Kusini umeendelea kutokota, baada ya Washington kumtangaza Balozi wa nchi hiyo ya Kiafrika mjini Washington, Ebrahim Rasool, kuwa mtu asiyetakiwa, kufuatia matamshi yake ya kumkosoa Rais Donald Trump.
-
Je, Afrika Kusini itasalimu amri mbele ya ubabe wa Trump?
Mar 11, 2025 08:03Kwa kuendelea msimamo wa kuingilia kati wa Rais Donald Trump wa Marekani katika masuala ya ndani ya Afrika Kusini, serikali ya Pretoria imetangaza kuwa haitajiingiza katika diplomasia isiyo na tija ya "kupiga kelele kupitia vipaza sauti" na Marekani.