Jan 27, 2024 11:55
Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria ameitaka Ofisi ya Kudumu ya nchi hiyo ya Kiarabu katika Umoja wa Mataifa iwasilishe ombi la kufanyika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la umoja huo, wa kujadili namna Israel itashinikizwa kuheshimu kivitendo maamuzi ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).