Dec 17, 2016 04:24
Khatibu wa Sala ya Ijumaa katika msikiti mtukufu wa Al-Aqsa, Palestina inayokaliwa kwa mabavu amesema, kuhamishiwa Baitul Muqaddas ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv na kuitambua rasmi Quds kuwa mji mkuu wa utawala bandia wa Israel ni sawa na kutangaza vita na Wapalestina.