-
Uingereza yamtaka Trump aheshimu JCPOA
Oct 11, 2017 04:48Waziri Mkuu wa Uingereza amekariri kuwa London itaendelea kufungamana na kutekeleza makubaliano ya nyuklia ya Iran, huku akimtaka Rais Donald Trump wa Marekani kuheshimu mapatano hayo ya kimataifa.
-
Malumbano ya Rais Trump na viongozi wa chama cha Repulican
Oct 09, 2017 23:39Rais Donald Trump wa Marekani amemshambulia na kumkosoa kwa maneno makali mmoja wa viongozi wenzake wa chama cha Republican katika Kongresi ya nchi hiyo.
-
Rais wa Venezuela amkejeli Trump, asema amemfanya mashuhuri
Oct 09, 2017 04:34Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ametumia kinaya kumkejeli Donald Trump na kusema kuwa rais huyo wa Marekani amemfanya awe shakhsia maarufu duniani.
-
Zarif: Iran itatoa jibu mwafaka kwa misimamo ya Trump kuhusu JCPOA
Oct 08, 2017 23:02Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran itatoa jibu mwafaka kujibu mapigo ya hatua yoyote ya kiuhasa itakayochukuliwa na Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya makubaliano ya nyuklia ya Iran ya JCPOA.
-
Wendy Sherman atetea tena makubaliano ya nyuklia ya Iran
Oct 08, 2017 04:08Mwanadiplomasia wa zamani wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani amesema kuwa, uhusiano kati ya nchi hiyo na Korea ya Kaskazini utaharibika zaidi iwapo Rais wa nchi hiyo Donald Trump atakataa kuthibitisha kwamba Iran imeheshimu na kutekeleza makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Trump akataa kuzungumzia 'umiliki wa bunduki' licha ya mauaji ya Las Vegas
Oct 05, 2017 11:00Licha ya makumi ya watu kuuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika hujuma ya ufyatuaji risasi siku chache zilizopita nchini Marekani, lakini Rais Donald Trump wa nchi hiyo amekataa katakata kuzungumzia uwezekano wa kuangaliwa upya sheria ya raia kumiliki silaha nchini humo.
-
Mashirika ya kutetea haki za binadamu Marekani yampeleka Trump kotini
Sep 30, 2017 04:40Mashirika ya kutetea haki za binadamu katika jimbo la Maryland nchini Marekani yameenda mahakamani kuushtaki utawala wa Rais Donald Trump wa nchi hiyo juu ya marufuku mpya iliyo dhidi ya wahajiri.
-
New York Times: Serikali ya Trump ndio ya kifisadi zaidi katika historia ya Marekani
Sep 25, 2017 23:21Gazeti la kila wiki la New York Times, sambamba na kuashiria kesi za ufisadi za baadhi ya viongozi wa Marekani, limeitaja serikali ya Rais Donald Trump kuwa ya kifisadi zaidi katika historia ya nchi hiyo.
-
Wananchi wa Marekani wanapinga kushambuliwa kijeshi Korea ya Kaskazini
Sep 25, 2017 23:19Uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani unaonyesha kuwa aghalabu ya wananchi wanapinga kushambuliwa kijeshi Korea ya Kaskazini.
-
Wanamichezo wa Marekani wapinga matamshi ya Trump
Sep 25, 2017 04:43Wachezaji wa Ligi ya mchezo wa Ragbi, soka (NFL) na mpira wa kikapu (NBA) wa Marekani wameingia ulingoni kupinga matamshi ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo.