-
Qassemi: Trump hajui lolote isipokuwa mafuta, dola na kudansi kwa panga
Sep 23, 2017 12:25Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Rais Donald Trump wa Marekani hajui lolote kuhusu dunia na eneo nyeti la Mashariki ya Kati isipokuwa fedha, mafuta na kudansi akiwa ameshika upanga.
-
Sayyid Hassan Nasrullah tumejiweka imara kukabiliana na adui hata ikiwa ni Marekani
Sep 22, 2017 04:13Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya nchini Lebanon Sayyid Hassan Nasrullah amesema kuwa harakati hiyo haitaki vita, lakini ikiwa itashambuliwa basi itasimama imara kukabiliana vikali na adui hata kama atakuwa ni Marekani.
-
Kim Jong-un: Trump ana matatizo ya kiakili, nitamfanya ajutie matamshi yake ya vitisho
Sep 22, 2017 01:15Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini amejibu matamshi ya vitisho ya Rais Donald Trump wa Marekani na kusema kuwa, rais huyo wa Marekani ana matatizo ya kiakili na kwamba atalipa gharama ya matamshi yake ya vitisho dhidi ya Pyongyang.
-
Wamarekani waendelea kukosoa hotuba ya Trump katika UN
Sep 21, 2017 11:45Viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa wameendelea kukosoa vikali hotuba na matamshi yaliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani katika mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.
-
Iran: Umefika wakati kwa Tehran kusahihisha makosa ya Marekani na kutoa jibu kali
Sep 20, 2017 22:01Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH), Muhammad Ali Jafari amesema kuwa, tuhuma za Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Iran, zinaashiria ubeberu wa Marekani na utawala wake wa kifisadi na kusisitiza kuwa, sasa umefika wakati wa Tehran kusahihisha makosa hayo ya Marekani.
-
Rais Hassan Rouhani atoa hotuba UN akosoa vikali hotuba yaTrump, aitaja kuwa ya kijahili na kijinga
Sep 20, 2017 12:51Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya lran amesema kuwa, miamala ya kijahili, michafu, chuki na iliyokosa uelewa na utoaji tuhuma zisizokuwa na msingi wowote ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya taifa la Iran katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) si tu kwamba, haiendani na umoja huo, bali inakinzana pia na matakwa na matarajio ya leo ya watu wa mataifa yote ya dunia katika kikao hicho.
-
Hotuba ya kifidhuli ya Trump UN yakosolewa vikali duniani
Sep 20, 2017 03:35Matamshi ya kifedhuli aliyotoa Rais Donald Trump wa Marekani katika hotuba yake ya kwanza katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) yamekosolewa vikali na viongozi na shakhsia mbalimbali wa kisiasa duniani.
-
Philip Roth: Rais Trump ni mtu mwongo na mpumbavu
Sep 17, 2017 09:36Mwandishi mmoja wa Kimarekani amemshambulia kwa maneno makali Rais Donald wa Marekani na kumuita kuwa ni mtu mwongo na mpumbavu.
-
Upinzani wa Wapalestina dhidi ya mipango ya hadaa ya Rais Trump wa Marekani
Sep 15, 2017 22:05Kuongezeka hatua za upuuzaji wa haki za Wapalestina, zikiwemo za kuundwa nchi yao huru, katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani, kumeongeza hasira na malalamiko ya wananchi hao wanaodhulumiwa na utawala kandamizi na ghasibu wa Israel katika siku za hivi karibuni.
-
Kuchanganyikiwa serikali ya Trump kuhusiana na Iran
Sep 15, 2017 08:57Sambamba na kutangazwa majina mapya ya raia na mashirika ya Iran ambayo yameongezwa kwenye orodha ya vikwazo ya Marekani, serikali ya nchi hiyo kwa mara nyingine tena imeakhirisha vikwazo vya nyuklia dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa siku nyingine 120.