Sep 29, 2017 07:57
Alkhamisi ya jana tarehe 28 Septemba, Rais Vladimir Putin wa Russia alikutana na kufanya mazungumzo mjini Ankara Uturuki na Rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdoğan, ambapo viongozi hao wawili wamebadilishana mawazo kuhusiana na hali ya mambo katika eneo la Mashariki ya Kati pamoja na uhusiano wa pande mbili.