-
Tume: Watu 210 wameuawa katika mapigano magharibi mwa Ethiopia
Aug 26, 2021 22:42Kamisheni ya Haki za Binadamu ya Ethiopia (EHRC) imesema watu wasiopungua 210 wameuawa katika ghasia na mapigano ya kikabila yaliyojiri kwa siku kadhaa katika eneo la Oromia, magharibi mwa Ethiopia.
-
Mapigano baina ya jeshi la serikali na waasi wa Tigray yapamba moto Ethiopia
Aug 13, 2021 19:30Mapigano makali yameripotiwa baina ya vikosi vya jeshi la serikali ya Ethiopia na wapiganaji wa kundi la waasi wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF) katika maeneo ya mpaka wa jimbo hilo na Amhara kaskazini mwa Ethiopia.
-
Ethiopia yataka wananchi washiriki vita dhidi ya waasi wa Tigray
Aug 10, 2021 23:19Waziri Mkuu wa Ethiopia amewataka wananchi wote wenye 'uwezo' wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika wajiunge na safu za wanajeshi wanaokabiliana na wapiganaji wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF).
-
Maiti nyingine zapatikana mpakani mwa Tigray, Ethiopia na Sudan
Aug 07, 2021 23:08Maiti zingine sita zimepatikana kwenye kingo za mto unaotenganisha Sudan na eneo la kaskazini mwa Ethiopia la Tigray.
-
UN: Watu laki mbili wamekuwa wakimbizi kutokana na vita nchini Ethiopia
Aug 04, 2021 22:45Mkuu wa Ofisi ya Uratibu wa masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa, watu laki mbili wamekuwa wakimbizi katika jimbo la Amhara na wengine elfu 45 katika jimbo la Afar huko Ethiopia kutokana na mapigano nchini humo.
-
Makumi ya maiti zapatikana kwenye mto ulioko mpakani mwa eneo la Ethiopia la Tigray na Sudan
Aug 03, 2021 07:45Maiti zisizopungua 30 zilizosombwa na maji zimepatikana kwenye kingo za mto unaotenganisha Sudan na eneo la kaskazini mwa Ethiopia la Tigray. Hayo ni kwa mujibu wa wakimbizi wawili wa Ethiopia na mashuhuda wanne raia wa Sudan waliookota maiti hizo.
-
Umoja wa Mataifa: Tuna wasiwasi baada ya misaada ya kibinadamu kuchelewa kufika Tigray Ethiopia
Jul 31, 2021 22:00Umoja wa Mataifa Uujmetangaza kuwa, una wasiwasi kufuatia ucheleweshaji katika kupeleka misaada ya kibinadamu jimboni Tigray, kwa minajili ya kukabiliana na hali mbaya inayolikumba jimbo hilo la kaskazini mwa Ethiopia.
-
Mamia ya raia wauawa katika eneo la Somali nchini Ethiopia
Jul 27, 2021 10:57Serikali ya jimbo la Somali huko mashariki mwa Ethiopia imewatuhumu waasi kutoka jimbo jirani la Afar kuwa wameua mamia ya raia katika shambulio la hivi karibuni.
-
Wapiganaji wa eneo la Tigray Ethiopia watishia kuelekea Addis Ababa
Jul 25, 2021 06:53Harakati ya Ukombozi ya eneo la Tigray (TPLF) imesema wapiganaji wa harakati hiyo ya kaskazini mwa Ethiopia hivi sasa wapo katika hali na nafasi nzuri ya kusonga mbele na kuelekea katika mji mkuu wa nchi hiyo, Addis Ababa.
-
Jeshi la Ethiopia lasema liko tayari kulinda Bwawa la Renaissance
Jul 23, 2021 23:25Meja Jenerali Yalma Merdasa, Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Ethiopia, amesema kwamba kikosi hicho hakijatoa jicho lake kwenye Bwawa la Renaissance hata kwa dakika moja, na kwamba kiko tayari kulinda usalama wa anga wa nchi hiyo.