Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza kuwa serikali ya Marekani ina jukumu na inapasa kubeba dhima kwa shambulio la kigaidi katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus lililofanywa na utawala wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari huko Gaza.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uwepo wa vikosi vya kigeni katika ardhi ya Syria hakusaidii katu amani na uthabiti wa nchi hiyo wala wa eneo la Asia Magharibi.
Faisal al Miqdad Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amefanya ziara nchini Saudi Arabia kufuatia mwaliko rasmi wa mwenzake wa Saudi Arabia Faisal bin farhan.
Rais Ebrahim Raeisi wa Iran amesema ana yakini kuwa Syria ina mustakakbali mwema huku akiwapongeza wananchi wa Syria kwa mapambano na muqawama katika kipindi cha miaka 11 ya vita dhidi ya nchi hiyo ambavyo vinaungwa mkono na madola ya kigeni.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema kuwa, nchi za Magharibi hazipaswi kujipa uthubutu wa kuzungumzia uchaguzi wa nchi hiyo kwani hauzihusu kwa mbali wala kwa karibu nchi hizo za kibeberu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema kuwa uhusiano wa Tehran na Damascus ni mkubwa na wa kistratejia na kueleza kuwa: Syria ina uhusiano mkubwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesemam kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaendeleza maamuzi na irada ambayo imekuwa ikichukua katika kuiunga mkono serikali na taifa la Syria kama nchi muitifakii wake wa kistratejia na itakuwa bega kwa bega na Syria hadi kupatikana ushindi wa mwisho.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, tawala na jamii za Kiislamu ziutangazie ulimwengu kwamba, kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel ni kitendo kibaya na kisichofaa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria, amesema kuwa raia wa nchi hiyo hawakubali uvamizi wowote katika ardhi za nchi yao.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria sambamba na kumkosoa vikali Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki, amesema kuwa tangu mwanzoni mwa mzozo wa Syria, serikali ya Ankara imekuwa ikiwaunga mkono magaidi.