-
Askari wa Israel wakiri, wengi waliowaua Ghaza kama 'magaidi' ni raia wa kawaida
Apr 01, 2024 23:18Maafisa na askari wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamekiri kuwa akthari ya vifo vilivyoelezewa na jeshi hilo kuwa ni vya kuua "magaidi" wakati wa vita vyake dhidi ya Ukanda wa Ghaza, kiukweli hasa ni vya mauaji ya raia wa kawaida.
-
Mbunge wa Marekani ataka kadhia ya Ghaza imalizwe kama zilivyofanyiwa Hiroshima na Nagasaki
Apr 01, 2024 23:18Tim Walberg, Mbunge wa jimbo la Michigan Kusini nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican amelazimika kufuta kauli aliyotoa ya kutaka Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, ambao ni makazi ya zaidi ya watu milioni mbili, ushughulikiwe kama ilivyofanyiwa miji ya Nagasaki na Hiroshima ya Japan ambayo ilishambuliwa na Marekani kwa mabomu ya nyuklia.
-
ICJ: Israel lazima ihakikishe msaada wa dharura, chakula vinaingizwa Ghaza bila kuchelewa
Mar 29, 2024 04:11Mahakama ya Juu zaidi duniani ya Haki ICJ imeuamuru utawala wa Kizayuni wa Israel "kuhakikisha msaada wa haraka wa kibinadamu" unaingizwa huko Ghaza bila kuchelewa, ikisisitiza kuwa "njaa imeshaingia" katika eneo hilo.
-
Wapalestina: Gati ya muda inayotaka kujenga Marekani Ghaza ni "Bandari ya Uvamizi"
Mar 29, 2024 03:54Wapalestina wanaielezea gati ya muda inayojengwa na Marekani kwenye pwani ya mji wa Ghaza kuwa ni "bandari ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu".
-
Kupokewa vizuri ripoti ya UN kuhusu mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel huko Ghaza
Mar 28, 2024 23:08Tathmini ya ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Palestina juu ya mauaji ya umati yanayofanywa na Israel kwenye Ukanda wa Ghaza imepokewa vizuri na kuungwa mkono na wawakilishi wa nchi za dunia ndani ya umoja huo.
-
Guterres akiri kashfa ya kimaadili ya utawala wa Kizayuni katika kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza.
Mar 25, 2024 22:30Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ametembelea kivuko cha Rafah (kati ya Ukanda wa Gaza na Misri), katika mwezi wa sita wa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni huko Gaza, na kukitaja kitendo cha utawala huo wa Kizayuni cha kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza kuwa ni "kashfa ya kimaadili".
-
Uchambuzi wa vita vya Gaza katika hotuba ya Nowruz ya kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Mar 22, 2024 03:34Katika hotuba yake ya siku ya kwanza ya mwaka mpya wa 1403 Hijria Shamsia, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amesema suala la Palestina na Gaza ni suala la daraja ya kwanza la kimataifa na kusisitiza kuwa: Kadhia ya Gaza imeonesha jinsi ulimwengu eti uliostaarabika na unaodai kutetea haki za binadamu, unavyofanya dhulma kubwa dhidi ya watu wa Gaza.
-
UNICEF: Israel inaendesha "vita vya kuwalenga watoto" wa Ghaza iliyowekewa mzingiro
Mar 21, 2024 23:00Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF James Elder amesema matukio yanayojiri katika Ukanda wa Ghaza ni "vita dhidi ya watoto," na kusisitiza kuwa eneo hilo hivi sasa si mahala pa kuishi watoto.
-
Msomi Myahudi akosoa vikali UN kushindwa kuchukua hatua juu ya Ghaza kutokana na kura za veto
Mar 21, 2024 22:56Mtengenezaji filamu mashuhuri wa Kiyahudi Haim Bresheeth, ambaye pia ni mpiga picha na msomi mtajika amekosoa vikali Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kushindwa kuchukua hatua katika mzozo wa utawala wa Kizayuni wa Israel na Palestina kutokana na kura ya turufu inayoshikiliwa na wanachama wake watano wa kudumu.
-
Mshauri wa zamani wa White House ametaka Wapalestina wahamishwe Ghaza na kupelekwa jangwani
Mar 20, 2024 08:03Mshauri wa zamani wa Ikulu ya Marekani (White House) Jared Kushner amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel inapasa uwaondoe Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na kuwahamishia kwenye jangwa la Negev kusini mwa ardhi zilizopachikwa jina bandia la Israel.