-
Iran: Wanaounga mkono siasa zisizo na hekima katika eneo wanapaswa kuwajibika
Dec 12, 2019 02:18Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali taarifa ya kikao cha 40 cha wakuu wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi na kusema kuwa, waungaji mkono wa siasa zisizo na hekima katika eneo hili la Mashariki ya Kati wanapaswa kutoa majibu na kuwajibika mbele ya fikra za waliowengi.
-
Safari ya Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa nchini Imarati; tangazo la kuundwa muungano wa baharini
Nov 27, 2019 01:41Ufaransa imekuwa na msimamo wa kindumakuwili kuhusiana na matukio ya hivi karibuni katika Ghuba ya Uajemi hususan masuala yanayohusiana na Iran; kwani sambamba na kuunga mkono makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, Paris inataka kuchukuliwa hatua dhidi ya kile kinachoelezwa kuwa, “hatua za Iran zinazohatarisha usalama wa eneo.”
-
Wito wa Putin wa kuanzishwa jumuiya ya kulinda usalama katika Ghuba ya Uajemi
Oct 05, 2019 13:50Baada ya Marekani kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka 2018, Washington iliazisha siasa za kuiwekea Iran mashinikizo ya kiwango cha juu zaidi. Vikwazo vya kiuchumi visivyo na kifani na mashinikizo makubwa ya Washington yamepelekea kuongezeka mivutano baina ya nchi hizo mbili na baadhi ya matokeo ya hali hiyo ni kuongezeka mivutano katika Lango Bahari la Hormuz na Ghuba ya Uajemi.
-
Ushirikiano na nchi za Mashariki ya Kati; stratijia ya Iran ya kulinda usalama wa safari za baharini Ghuba ya Uajemi
Sep 30, 2019 07:37Hossein Dehghani, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran katika Masuala ya Sheria na Kimataifa amesema katika kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC pambizoni mwa kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York Marekani kwamba, mizozo ya aina yoyote ni hatari kwa eneo hili zima.
-
Ukosoaji mkali wa Sergey Lavrov kuhusiana na miamala haribifu ya Marekani dhidi ya mapatano ya JCPO na Ghuba ya Uajemi
Sep 30, 2019 02:36Hatua zilizo kinyume cha sheria za Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka jana na kisha kuiwekea Iran vikwazo vikali ambavyo vilikuwa havijawahi kushuhudiwa tena huko nyuma, na baada ya hapo kuzidisha uwepo wake wa kijeshi katika Ghuba ya Uajemi ambao umeshadidisha mizozo katika eneo hilo la kistratijia, ni mambo ambayo yameizidishia wasi wasi serikali ya Russia.
-
Zarif: Iwapo Marekani inataka mazungumzo na Iran lazima itekeleze ahadi zake
Sep 29, 2019 07:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran haitaacha mustakabali wa uchumi na wananchi wake utegemee mkutano wa kimaonyesho na Rais Donald Trump wa Marekani. Ameongeza kuwa, kama ambavyo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alivyosema, 'iwapo Mareknai inataka kufanya mazungumzo na Iran, ni lazima kwanza itekeleze ahadi zake na isitishe vikwazo.'
-
Katika mtazamo wa Kansela wa Ujerumani; Mwarubaini wa kupunguza mivutano Magharibi ya Asia ni kurejea kwenye JCPOA
Sep 18, 2019 11:55Kwa mtazamo wa Umoja wa Ulaya na Troika ya umoja huo inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yana mchango muhimu sana katika kulinda amani na usalama katika eneo la Magharibi ya Asia na katika uga wa kimataifa. Kwa mtazamo wa nchi za Ulaya, kujitoa Marekani katika JCPOA kumekuwa chanzo cha kujitokeza mivutano na hali ya wasiwasi katika Ghuba ya Uajemi na Magharibi ya Asia.
-
Baqeri: Iran iko tayari kulinda kikamilifu maslahi yake katika Ghuba ya Uajemi
Sep 12, 2019 11:26Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Iran amesema: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kulinda kikamilifu usalama na maslahi yake katika Ghuba ya Uajemi."
-
Ukosoaji wa Russia kwa nafasi haribifu ya Magharibi katika Ghuba ya Uajemi
Sep 11, 2019 02:31Baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kuiondoa nchi hiyo katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mnamo tarehe 8 Mei mwaka uliopita, alianza kutekeleza mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran.
-
Sisitizo la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa EU juu ya kulinda makubaliano ya JCPOA na kuimarisha usalama wa Ghuba ya Uajemi
Aug 31, 2019 12:10Umoja wa Ulaya pamoja na Troika ya Ulaya zikiwa wanachama wa kundi la 4+1 mara kadhaa zimesisitiza kuwa kuna udharura wa kuyalinda makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na wakati huo huo kurejesha uthabiti na usalama katika Ghuba ya Uajemi kwa kuzingatia chokochoko za Marekani katika eneo hilo la maji lenye umuhimu wa kijio-stratejia.