-
Iran yalaani chokochoko za Marekani Ghuba ya Uajemi, yamuita balozi wa Uswisi
Apr 23, 2020 22:15Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali chokochoko za jeshi la Marekani dhidi ya wanajeshi wa baharini wa Iran katika Ghuba ya Uajemi, sambamba na kukosoa bwabwaja na vitisho vya Rais Donald Trump dhidi ya askari hao wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH).
-
Njama za Trump za kuzusha mizozo na kutishia amani na usalama wa Ghuba ya Uajemi
Apr 23, 2020 08:26Baada ya Marekani kuchukua hatua ya upande mmoja na kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia mwezi Mei mwaka 20018, ilianza kutekeleza siasa za mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran.
-
Brigedia Amir Hatami: Matokeo ya uwepo wa Marekani Ghuba ya Uajemi ni ukosefu wa usalama
Apr 17, 2020 20:13Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali uwepo wa Marekani katika eneo la Ghuba ya Uajemi na kusema kuwa, hatua hiyo haina matokeo mengine ghairi ya ukosefu wa usalama.
-
Russia yatahadharisha juu ya athari mbaya za kuwepo majeshi ya nchi ajinabi katika Ghuba ya Uajemi
Mar 07, 2020 11:57Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ametahadharisha kuhusu athari mbaya za kuwepo majeshi ya nchi ajinabi katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
-
Raisi: Marekani ikituvamia tutavitimua vikosi vyake Ghuba ya Uajemi
Feb 07, 2020 23:29Mkuu wa Vyombo vya Mahakama vya Iran ameonya dhidi ya tishio lolote la adui dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu na kubainisha kuwa, iwapo Washington itathubutu kuchukua hatua yoyote iliyo dhidi ya Iran basi taifa hili litawatimua hadi chini ya Ghuba ya Uajemi wanajeshi wa Marekani.
-
Iran: Kujitoa Marekani hakutushughulishi, kama Ulaya wataheshimu JCPOA nasi tutaheshimu
Jan 22, 2020 22:58Mkuu wa Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, nchi zinazounda kundi la 4+1 katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA zinapaswa kuheshimu vilivyo makubaliano hayo na kama nchi za Ulaya zitaheshimu vipengee vya mapatano hayo, Tehran nayo bila ya shaka yoyote itaheshimu.
-
Tehran yampa Rais wa Ufaransa somo la jiografia kuhusu "Ghuba ya Uajemi"
Jan 19, 2020 04:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amempa Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa somo la jiografia na kumkosoa kwa kupotosha historia.
-
Iran: Wanaounga mkono siasa zisizo na hekima katika eneo wanapaswa kuwajibika
Dec 11, 2019 22:48Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali taarifa ya kikao cha 40 cha wakuu wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi na kusema kuwa, waungaji mkono wa siasa zisizo na hekima katika eneo hili la Mashariki ya Kati wanapaswa kutoa majibu na kuwajibika mbele ya fikra za waliowengi.
-
Safari ya Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa nchini Imarati; tangazo la kuundwa muungano wa baharini
Nov 26, 2019 22:11Ufaransa imekuwa na msimamo wa kindumakuwili kuhusiana na matukio ya hivi karibuni katika Ghuba ya Uajemi hususan masuala yanayohusiana na Iran; kwani sambamba na kuunga mkono makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, Paris inataka kuchukuliwa hatua dhidi ya kile kinachoelezwa kuwa, “hatua za Iran zinazohatarisha usalama wa eneo.”
-
Wito wa Putin wa kuanzishwa jumuiya ya kulinda usalama katika Ghuba ya Uajemi
Oct 05, 2019 10:20Baada ya Marekani kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka 2018, Washington iliazisha siasa za kuiwekea Iran mashinikizo ya kiwango cha juu zaidi. Vikwazo vya kiuchumi visivyo na kifani na mashinikizo makubwa ya Washington yamepelekea kuongezeka mivutano baina ya nchi hizo mbili na baadhi ya matokeo ya hali hiyo ni kuongezeka mivutano katika Lango Bahari la Hormuz na Ghuba ya Uajemi.