Mar 15, 2019 07:20
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Serikali ya Marekani ndiyo mkiukaji mkubwa kabisa wa haki za binadamu za wananchi wa Iran, kwani kwa kuwatwisha vikwazo vyake haramu vya nje ya mipaka na vya upande mmoja, Washington haijasita kuchukua hatua yoyote ya kukanyaga haki za raia wa Iran.