-
Mwanadiplomasia wa zamani wa US: Jinai za Ghaza 'zitamsakama' Blinken hadi mwisho wa maisha yake
Jan 17, 2025 23:54Mwanadiplomasia wa Marekani aliyejiuzulu mwaka jana kulalamikia vita vya Ghaza na uungaji mkono wa Washington kwa vita hivyo amesema, jinai zilizofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika vita hivyo 'zitamsakama' waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Antony Blinken kwa muda wote uliosalia wa maisha yake.
-
Araqchi aipongeza Hamas kwa ushindi dhidi ya Israel
Jan 17, 2025 10:33Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameipongeza Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) kwa ushindi wa muqawama na wananchi wa Palestina dhidi ya Israel katika vita na mauaji ya kimbari ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel imeshaua Wapalestina 40 Ghaza tangu baada ya kutangazwa makubaliano ya kusitisha vita
Jan 16, 2025 00:07Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeendeleza mashambulio katika Ukanda wa Ghaza licha ya kutangazwa makubaliano ya kusitisha vita kati ya utawala huo ghasibu na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS. Hadi wakati huu, Wapalestina wasiopungua 40 wameshauliwa shahidi na jeshi hilo.
-
Hamas: Wapalestina wanakufa kwa baridi kali Ukanda wa Gaza; yaitaka UN ichukue hatua
Jan 01, 2025 00:09Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeitolea wito jamii ya kimataifa na Umoja wa Mataifa kuchukua hatua hivi sasa ambapo raia wa Palestina wanaaga dunia kwa baridi kali huko Gaza huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo.
-
HAMAS yatumia droni iliyoiteka kutoka kwa Israel kuwatwanga Wazayuni
Dec 30, 2024 23:24Brigedi za Izzudin Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS zimetangaza kuwa, zimetumia droni ziliyoiteka kutoka kwa wanajeshi wa Israel kuwashambulia wanajeshi hao vamizi na Wazayuni wenzao.
-
Hamas yalaani vikali kushambuliwa hospitali Gaza; yasema Israel inafanya maangamizi ya kizazi
Dec 23, 2024 23:05Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani mashambulizi yanayoendelea kufanywa na jeshi la Israel katika hospitali ya Kamal Adwan kaskazini mwa Gaza na kusema kuwa, huo ni "uhalifu usio na mfano dhidi ya binadamu."
-
Hamas yaendeleza juhudi za kufikia mapatano ya kusitisha vita Ukanda wa Gaza
Dec 22, 2024 04:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palstina (Hamas) imeripoti kuwa makundi ya muqawama ya Palestina yamekutana katika kikao cha pamoja huko Cairo, Misri na kwamba upo uwezekano wa kufikia mapatano ya kusitisha vita huko Ukanda wa Gaza.
-
Hamas: Taasisi za kimataifa zisaidie kufikisha misaada ya kitiba Ukanda wa Gaza
Dec 16, 2024 03:46Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeziomba taasisi za kimataifa zitume misaada ya kitiba na kitabibu kwa ajili ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
HAMAS: Hakuna wa kuwaamulia Wapalestina, wao wenyewe wana haki kamili, uwezo na ustahiki
Dec 15, 2024 02:05Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, kwa mara nyingine tena imesema, inakaribisha uchukuaji hatua wowote ule wa dhati na wa kivitendo kwa ajili ya kusimamisha uchokozi na jinai za utawala ghasibu wa Israel na kukomesha vita katika Ukanda wa Ghaza.
-
HAMAS yajibu vitisho alivyotoa Trump kuhusu mateka wa Kizayuni wanaoshikiliwa Ghaza
Dec 04, 2024 03:12Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa jibu kwa ujumbe wa vitisho uliotolewa na rais mteule wa Marekani kuhusu mateka wa Kizayuni wanaoshikiliwa katika Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa, ni bora Trump atume salamu zake hizo kwa Netanyahu.