-
HAMAS yasisitizia mapambano na Wazayuni ili kulinda matukufu ya Palestina
Oct 10, 2017 04:38Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa suala la kupambana na Wazayuni maghasibu ambao wanayakalia kwa mabavu maeneo matakatifu ya Waislamu huko Palestina kama vile Masjidul Aqswa na Haram ya Nabii Ibrahim AS katika mji wa al Khalil wa kusini mwa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, ni muhimu sana.
-
Jeshi la Israel lashambulia ngome za Hamas Ukanda wa Gaza
Oct 09, 2017 04:30Vikosi vya Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel vimeshambulia kile vinachodai kuwa ni ngome za Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas, katika Ukanda wa Gaza.
-
Hamas: Utawala wa Kizayuni ndio unaopata hasara kutokana na umoja wa Wapalestina
Oct 04, 2017 12:52Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, utawala wa Kizayuni ndio unaopata hasara zaidi unapokuwepo umoja na mshikamano kati ya Wapalestina na ndio maana utawala huo wakati wote unafanya njama za kuyazozanisha makundi ya Palestina.
-
Ismail Haniya: Hatutaweka chini silaha madamu wavamizi wangaliko ndani ya Palestina
Oct 03, 2017 22:52Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: madamu wavamizi wangaliko katika ardhi ya Palestina wananchi wetu wana haki ya kuwa na silaha.
-
Hamas: Ukombozi wa Palestina unahijatia umoja wa kitaifa
Sep 30, 2017 12:57Naibu Mkuu wa Idara ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema kuwa, ukombozi wa Palestina na Quds tukufu na kukomeshwa uvamizi wa utawala haramu wa Israel kunahitaji umoja na mshikamano wa kitaifa.
-
HAMAS: Hakuna cha kuzungumzwa kuhusu silaha za muqawama
Sep 29, 2017 04:07Naibu Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kwamba katika mazungumzo na harakati ya Fat-h, Hamas haikukubaliana na wazo la kuwapokonya silaha wanamuqawama na kwamba suala hilo halikujadiliwa katika mazungumzo yaliyopita wala halitojadiliwa katika mustakabali.
-
Hamas yaipongeza UN kwa kuiweka Israel katika orodha nyeusi
Sep 25, 2017 04:22Harakari ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imepongeza hatua ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ya kuiweka Israel katika orodha nyesi ya nchi zinazokiuka haki za binadamu.
-
Hamas yaafiki kuvunja serikali yake Ghaza kwa ajili ya Umoja wa Palestina
Sep 17, 2017 23:13Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imekubali sharti kubwa lililowekwa na chama cha Fat'h cha Mahmoud Abbas ikiwa ni pamoja na kufanyika chaguzi za kitaifa Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Ghaza.
-
Hamas: Tutafungamana na chaguo la muqawama ili kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina
Sep 14, 2017 03:28Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesisitiza kuwa itaendelea kufungamana na chaguo la muqawama kama njia pekee ya kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina katika ardhi yenye uhuru na kujitawala.
-
HAMAS yatoa sharti la kuipatia Israel taarifa za askari wake iliowakamata mateka
Sep 13, 2017 10:29Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesema itaupatia utawala wa Kizayuni wa Israel taarifa kuhusu askari wake waliokamatwa mateka katika Ukanda wa Gaza kwa sharti utawala huo haramu uwaachie huru kwanza Wapalestina 54 unaowashikilia kwenye jela zake.