-
Wapalestina 35 wachomwa moto wakiwa hai katika shambulio la kinyama la Israel Rafah
May 27, 2024 03:20Jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel limeshambulia kwa makombora kambi ya watu waliolazimika kuhama makazi yao na kuhamia eneo lililotengwa kuwa na usalama huko Rafah, na kuwaua shahidi Wapalestina 35, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.
-
Hizbullah, Harakati ya Muqawama Iraq zashambulia ngome za Israel
May 24, 2024 07:22Wanamapambano wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Iraq wamefanya operesheni tofauti dhidi ya kambi na ngome za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel, katika maeneo yaliyokaliwa kwa mabavu mwaka 1948, kwa ajili ya kulipiza kisasi cha vita vya umwagaji damu vya Israel dhidi ya Gaza.
-
Kwa mara ya kwanza, Hizbullah yashambulia ndani kabisa ya ngome za Wazayuni tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Apr 24, 2024 02:44Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa imefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani dhidi ya vituo viwili vya kiejshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel kulipiza kisasi cha mauaji ya wapiganaji wake wawili.
-
Hizbullah ya Lebanon yafanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya Israel
Apr 20, 2024 10:42Muqawama wa Kiislamu wa Lebanon umefanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Shambulio la makombora la Hizbullah lajeruhi askari 14 wa Israel, sita wako mahututi
Apr 18, 2024 07:08Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa imehusika na shambulio lililolenga kituo cha kijeshi kaskazini mwa 'Israel' na kuwajeruhi wanajeshi wasiopungua 14, na kusema, shambulio hilo limefanywa kulipiza kisasi cha mashambulizi ya utawala wa Kizayuni yaliyoua wanachama wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu.
-
Wazayuni wanakwepa kurejea maeneo wanayoishi kwa kuhofia mashambulio ya Hizbullah
Apr 16, 2024 10:48Televisheni ya utawala wa Kizayuni wa Israel imefichua kuwa, sehemu kubwa ya Wazayuni wanaoishi kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni, wanakwepa kurejea maeneo hayo wakihofia mashambulio ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Waisraeli 80,000 wakimbia makazi yao wakihofia makombora ya Hizbullah
Mar 13, 2024 07:44Makumi ya maelfu ya walowezi wa Kizayuni wamekimbia makazi yao katika maeneo ya kaskazini mwa Palestina yaliyopachikwa jinai bandia la Israel, wakihofia mashambulizi ya Harakati ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Hizbullah: Mhimili wa Muqawama umedhamiria kwa dhati kuikomboa Palestina kwa gharama yoyote
Feb 16, 2024 07:53Harakati ya Muqawama wa Lebanon ya Hizbullah imesema Mhimili wa Muqawama katika eneo umeazimia kuikomboa Palestina kutoka kwenye makucha ya uvamizi na ukatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa gharama yoyote.
-
Hizbullah yaapa kujibu mashambulizi ya Israel yaliyoua raia wakiwemo watoto wawili
Feb 15, 2024 07:49Afisa wa ngazi ya juu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amelaani mashambulizi ya hivi karibuni zaidi ya Israel kusini mwa Lebanon yaliyosababisha vifo vya watu kadhaa wakiwemo watoto wawili, ikiapa kwamba majibu ya harakati ya Muqawama ya Lebanon yako njiani.
-
Hizbullah yaonya dhidi ya sera ya kupenda vita ya Israel
Feb 12, 2024 04:37Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema mrengo wa muqawama haujatangaza vita kamili, lakini iwapo Israel itapanua vita vyake vya Gaza, wanamuqawama hawatasita kufanya mashambulizi ya kujibu chokochoko za adui huyo mpenda vita.