-
Harakati ya Hizbullah: Marekani inaondoka Syria kutokana na kushindwa
Dec 21, 2018 23:27Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Marekani inaondoka nchini Syria kutokana na kushindwa siasa zake katika Mashariki ya Kati na kutoweza kuuhami na kuulinda utawala haramu wa Israel.
-
Hizbullah: Hakuna hata sehemu moja ya Israel itakayosalimika na makombora yetu
Dec 09, 2018 11:41Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema, hakuna hata sehemu moja ya Israel ambayo haiwezi kufikiwa na makombora ya harakati hiyo ya muqawama.
-
Hizbullah: Quds tukufu haiwezi kugawanyika
Nov 25, 2018 04:37Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema ni muhali na jambo lisiloyumkinika kuugawanya mara mbili mji mtukufu wa Quds (Jerusalem).
-
Uwezo wa makombora ya Harakati ya Hizbullah, nukta ya nguvu ya taifa la Lebanon
Nov 12, 2018 04:02Akihutubu kwa mnasaba wa 'Siku ya Shahidi' Sayyid Hassan Nasrullah ameashiria nukta ya nguvu ya Lebanon na kusema kuwa uwezo wa nchi hiyo unapatikana katika uwezo wa makombora ya muqawama na ndio maana adui hathubutu kuichokoza nchi hiyo.
-
Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah: Kuundwa serikali ya Lebanon kunategemea uamuzi wa Saad Hariri
Nov 09, 2018 01:10Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, waziri mkuu mwenye jukumu anao uwezo wa kupata njia ya ufumbuzi wa kimantiki kwa ajili ya kuunda serikali mpya na kwamba suala hilo kwa sasa linategemea uamuzi wake yeye.
-
Wazayuni wangali wana kiwewe na uwezo wa makombora ya Hizbullah ya Lebanon
Oct 29, 2018 01:07Jenerali wa zamani wa jeshi la utawala haramu wa Israel amesema kuwa, Hizbullah ya Lebanon ni kundi lenye uratibu na lililojipanga na kuongeza kuwa, maelfu ya makombora ya Hizbullah yenye umakini wa hali ya juu yanaweza kulenga eneo lolote katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavuu (Israel)
-
Hizbullah ya Lebanon yataka kuundwa serikali mpya haraka iwezekanavyo
Oct 22, 2018 04:13Viongozi wa ngazi ya juu wa harakati ya mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah wametaka kuundwa haraka iwezekanavyo serikali mpya nchini humo na kupatiwa ufumbuzi hitilafu zilizosalia.
-
Sayyid Hassan Nasrullah: Hizbullah inatumia weledi kusambaratisha fitina za maadui wa muqawama
Oct 19, 2018 21:39Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, harakati hiyo inatumia weledi wa hali ya juu kusambaratisha njama za maadui wenye lengo la kuzusha fitina dhidi ya muqawama.
-
Sayyid Nasrullah: Trump anatumia propaganda chafu dhidi ya Iran kuuza silaha kwa nchi za Kiarabu
Oct 12, 2018 23:19Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Rais Donald Trump wa Marekani anatumia sera ya kueneza propaganda chafu dhidi ya Iran kwa shabaha ya kutaka kuuza silaha za mabilioni ya dola kwa nchi za Kiarabu.
-
Gebran Bassil: Israel ndio mtendaji wa ugaidi wa kiserikali katika Mashariki ya Kati
Oct 01, 2018 23:41Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Lebanon amesema kuwa, utawala haramu wa Israel ndio mtendaji wa ugaidi wa kiserikali katika eneo la Mashariki ya Kati lakini umekuwa ukizituhumu nchi nyingine.