-
Uungaji mkono mkubwa wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa magaidi kusini mwa Yemen
Jul 24, 2017 12:09Shirika la kutetea haki za binadamu la Ulaya na Mashariki ya Kati limetoa ripoti inayoeleza kuwa kuna makundi kadhaa ya kigaidi yanayoendesha harakati zao katika mji wa Aden kusini mwa Yemen kwa uungaji mkono kamili wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
Imarati na Saudia zakataa wito wa Qatar wa mazungumzo
Jul 23, 2017 14:07Umoja wa Falme za Kiarabu umekataa wito uliotolewa hivi karibuni na Amir wa Qatar, Sheikh Tamin bin Hamad al-Thani, wa kufanyika mazungumzo ya kuupatia ufumbuzi mgogoro uliopo, na kusisitiza kuwa Doha sharti ibadili sera zake kabla ya kufanyika jitihada zozote za kuiondolea vikwazo nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi, iivyowekewa na Saudia na wapambe wake.
-
Imarati: Juhudi za upatanishi wa Kuwait katika mgogoro wa nchi za Kiarabu zitaambulia patupu
Jul 19, 2017 02:27Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa serikali ya Imarati, Anwar Mohammed Qarqash amesema kuwa, juhudi za upatanishi wa Kuwait kwa ajili ya kutafuta utatuzi wa mgogoro wa nchi za Kiarabu, zitaambulia patupu iwapo Qatar haitabadilisha siasa zake.
-
Qatar kuishtaki Imarat kwa kuhusika na udukuzi
Jul 18, 2017 15:14Serikali ya Qatar imeeleza kusikitishwa sana na hatua ya Imarat ya kudukua mitandao ya intaneti ya serikali ya Doha, suala ambalo limeibuka mgogoro wa sasa kati ya nchi hizo mbili na kusisitiza kuwa, Doha itawafungulia mashtaka wahusika wa uhalifu huo.
-
Nchi za Kiarabu zilizoiwekea vikwazo Qatar zadhurika kiuchumi
Jul 09, 2017 02:51Kuongezeka mivutano katika uhusuano wa nchi nne za Kiarabu na Qatar kumezisababishia madhara makubwa ya kiuchumi nchi za Saudia na Imarati.
-
Chama cha Leba cha Uingereza chataka uchunguzi kuhusu jela za Imarati Yemen
Jul 02, 2017 15:17Mkuu wa chama cha Leba cha nchini Uingereza amesema kuna udharura wa kufanyika uchunguzi kuhusu jela za siri za mateso za Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Yemen.
-
Kufichuliwa ushiriki wa Imarati katika vitendo vya kigaidi vya Israel
Jun 17, 2017 12:19Habari mbalimbali zimearifu tukio jipya la namna Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) unavyoshiriki katika vitendo vya kigaidi vya utawala wa Israel; suala ambalo katika siku za hivi karibuni kwa mara nyingine tena limeakisi ushirikiano uliopo kati ya watawala wa Kiarabu na maghasibu wanaoikalia Quds Tukufu kwa mabavu katika kuwakandamiza wananchi wa Palestina na kusogeza mbele siasa za kigaidi za Israel.
-
Ripoti: Imarati ilitoa dola bilioni 3 kufadhili mapinduzi ya kijeshi Uturuki
Jun 14, 2017 04:18Gazeti moja la kila siku la Uturuki limeandika kuwa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ulitoa kitita cha dola bilioni 3 za Marekani kwa ajili ya kufadhili jaribio la mapinduzi ya kijeshi lililofeli mwezi Julai mwaka jana 2016 nchini Uturuki.
-
Amnesty yashutumu uamuzi wa Saudia na wapambe wake dhidi ya Qatar
Jun 13, 2017 13:56Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekosoa vikali hatua zisizo na mantiki za Saudi Arabia na wapambe wake dhidi ya Qatar.
-
UN: Imarati imekiuka vikwazo vya silaha, Libya
Jun 10, 2017 15:56Umoja wa Mataifa umesema kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) umekiuka vikwazo vya silaha vya Libya.