Jul 06, 2020 03:26
Mshauri wa Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ameonya kuwa, Intifadha ya Tatu ya wananchi wa Palestina inanukia na bila shaka itaibuka mara moja iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utatekeleza mpango wake wa kulipora na kuliunganisha eneo la Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan na ardhi za Palestina zilizopewa jina la Israel.