-
Iran: Dunia haitasahau nafasi ya UK katika kuundwa utawala wa Kizayuni
Sep 02, 2024 23:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, mataifa ya kieneo na dunia kwa ujumla hayatasahau mchango na nafasi ya Uingereza katika kuundwa utawala wa kibaguzi wa Israel katika kitovu cha ulimwengu wa Kiislamu.
-
Pezeshkian afafanua mipango ya serikali yake katika mazungumzo na wananchi
Sep 02, 2024 09:02Katika mazungumzo yake ya kwanza ya televisheni na wanachi, Rais Masoud Pezeshkian amefafanua mipango ya serikali yake katika nyanja za ndani na nje ya nchi, na kusema kuwa vipaumbele vya serikali ya 14 ni kuwaridhisha wananchi, kuzingatia masuala ya kiuchumi na kuimarisha uhusiano na nchi mbalimbali.
-
Pezeshkian: Umoja ndio njia bora ya kukabiliana na matatizo ya kiuchumi
Sep 01, 2024 03:52Rais wa Iran Masoud Pezeshkian amesisitiza haja ya kulinda umoja wa kitaifa miongoni mwa mirengo na makundi mbalimbali ya kisiasa ili kuwatumikia vyema zaidi wananchi.
-
Rais wa Iran kushiriki mkutano wa BRICS nchini Russia
Aug 31, 2024 09:35Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian anatazamiwa kushiriki Mkutano wa BRICS wa 2024 nchini Russia karibuni hivi.
-
Iran yakanusha madai ya kuwapa mafunzo askari wa Russia huko Ukraine
Aug 31, 2024 08:18Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amepuuzilia mbali madai kwamba mwanajeshi wa Jamhuri ya Kiislamu amekuwa akitoa mafunzo kwa wanajeshi wa Russia katika ardhi ya Ukraine.
-
"Wazayuni, kizingiti cha kupatikana uthabiti katika umma wa Kiislamu"
Aug 31, 2024 07:51Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Amani na Usalama ya Kimataifa ya Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema utawala wa Kizayuni ndicho kikwazo kikuu cha kupatikana uthabiti na maendeleo endelevu katika ulimwengu wa Kiislamu na eneo la Asia Magharibi.
-
Wanafunzi wa Iran waibuka wa kwanza katika Olympiad ya Kimataifa ya Astronomia, Astrofizikia
Aug 28, 2024 23:21Wanafunzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamechukua nafasi ya kwanza katika Olympiadi ya 17 ya Kimataifa ya Astronomia na Astrofizikia.
-
Msumbiji yawaachia huru mabaharia kumi wa Kiirani
Aug 28, 2024 23:21Mabaharia 10 wa Iran waliokuwa wanashikiliwa nchini Msumbiji wameachiliwa huru.
-
Iran yakosoa misimamo ya kindumakuwili ya Uingereza kuhusiana na vita vya Gaza
Aug 26, 2024 08:41Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini London umekosoa misimamo ya kindumakuwili ya serikali ya Uingereza kuhusiana na matukio ya eneo la Asia Magharibi na kusema, huku London ikionyesha kidhahiri kuwa inaunga mkono usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza, lakini imefumbia macho jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Israel dhidi ya watu madhulumu wa Palestina.
-
Kipaumbele cha sera za kigeni za Iran; nchi jirani, eneo na muqawama
Aug 25, 2024 08:45Waziri mpya wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema kuwa kipaumbele cha kwanza katika sera za kigeni ni nchi jirani na kipaumbele cha pili ni kupanua uhusiano na Afrika, Amerika ya Latini na Asia Mashariki.