-
Iran na Sudan zasisitiza kupanua ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara
Nov 07, 2024 23:07Waziri wa Uchumi na Fedha wa Iran na Waziri wa Fedha na Mipango ya Kiuchumi wa Sudan wamekutana na kujadili upanuzi wa uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara.
-
Uhusiano wa Iran na Tunisia wazidi kuimarika, Tunis yataka safari za moja kwa moja za ndege
Nov 07, 2024 06:25Balozi wa Tunisia mjini Tehran ametaka kuweko safari za moja kwa moja za ndege baina ya Tehran na Tunis hasa kwa vile uhusiano wa nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unazidi kuimarisha siku baada ya siku.
-
Aragchi: Kuna uhusiano wa karibu kati ya kijikundi cha kigaidi cha Jaysh al-Dhulm na utawala wa Kizayuni
Nov 06, 2024 10:03Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Iran na Pakistan zinaamini kuna uhusiano wa karibu kati ya kundi kijikundi cha kigaidi cha Jaish al Dhulm na utawala wa Kizayuni na zinasisitiza juu ya kupigana na kukabiliana nalo.
-
Mafanikio mapya ya anga za mbali ya Iran: Kurushwa angani satelaiti mbili za Kowsar na Hod'hod
Nov 06, 2024 07:23Watafiti wa moja ya mashirika ya anga za juu ya Iran kwa kubuni na kutengeneza satelaiti mbili za Kowsar na Hod'hod wameweza kuziingiza kwa mafanikio satelaiti hizo mbili kwenye mzingo wa dunia wenye umbali wa kilomita 500 kwa kutumia roketi ya Soyuz kutokea kituo cha Vostochny nchini Russia, hapo siku ya Jumanne tarehe 5 Novemba.
-
Kulaaniwa na Jumuiya ya NAM uvamizi wa Israel dhidi ya Iran
Nov 05, 2024 22:44Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM), imelaani uovu wa utawala wa Kizayuni na hujuma yake ya makusudi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutangaza kuwa, shambulio hilo ni ukiukaji mkubwa wa mamlaka na umoja wa ardhi ya Iran.
-
Waziri wa Croatia: Iran ni mfano kwetu wa kuiga wa watu wa dini mbalimbali kuishi kwa amani
Nov 05, 2024 09:02Waziri wa Utamaduni wa Croatia ametoa wito wa kuitumia tajiriba na uzoefu wa wafuasi wa dini tofauti nchini Iran katika kustawisha utamaduni wa kuishi pamoja kwa amani na masikilizano watu wa dini mbalimbali.
-
Iran yasisitiza kuwa bila shaka itajibu uchokozi wa Israel
Nov 04, 2024 23:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei amesema bila ya shaka utawala wa Kizayuni wa Israel utapokea jibu kali kutokana na uchokozi wake wa hivi karibuni dhidi Iran.
-
Mazungumzo ya Waziri wa Mawasiliano wa Iran na Naibu Waziri Mkuu wa Cuba
Nov 04, 2024 08:13Katika siku ya kwanza ya ziara yake nchini Cuba, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa nchi hii katika masuala ya sayansi na teknolojia na kuzungumzia nyanja za maendeleo ya ushirikiano wa kisayansi, kiteknolojia na mawasiliano.
-
Wairani waadhimisha Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Uistikbari
Nov 03, 2024 03:58Sherehe za kuadhimisha Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Uistikbari wa Dunia ambayo huadhimishwa tarehe 13 Aban (Novemba 3 au 4) kila mwaka hapa Iran, zinaendelea mjini Tehran na katika miji mingine kote Iran.
-
Kuendelea hatua na misimamo ya undumakuwili ya Marekani dhidi ya Iran
Nov 02, 2024 07:45Rais Joe Biden wa Marekani jana Ijumaa aliwatumia barua wakuu wa bunge la wawakilishi na seneti ambapo amerefusha kwa mwaka mmoja mwingine muda wa hali ya hatari kitaifa kuhusu Iran. Biden amechukua hatua hii katika miezi yake ya mwisho akiwa White House na kabla ya kufanyika uchaguzi wa Rais wa Marekani tarehe 5 mwezi huu wa Novemba.