-
Iran yakosoa taarifa ya Arab League, yasema itaendelea kuwaadhibu watenda jinai
Jan 19, 2024 08:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa vikali taarifa ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusu hatua ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ya kufanya shambulio la makombora dhidi ya kituo kikuu cha ujasusi cha shirika la ujasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel Mossad katika eneo la Kurdistan ya Iraq.
-
Iran yaikosoa US kwa kuiweka Ansarullah katika orodha ya 'ugaidi'
Jan 19, 2024 00:00Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali hatua ya Marekani ya kuiweka Harakati ya Ansarullah ya Yemen kwenye orodha ya kile inachokiita "makundi ya kigaidi" na kueleza kwamba, kitendo hicho ni katika mfululizo wa hatua za Washington za kuuunga mkono utawala wa kigaidi wa Israel.
-
Balozi mdogo wa Pakistan Tehran aitwa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran
Jan 18, 2024 05:58Balozi mdogo wa Pakistan mjini Tehran ameitwa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kufuatia mlipuko uliotokea leo asubuhi katika kijiji cha mpakani katika mkoa wa Sistan na Baluchistan hapa nchini.
-
Watu saba wasio raia wa Iran wauawa katika miripuko iliyotokea kusini mashariki mwa nchi
Jan 18, 2024 03:41Watu saba wasio raia wa Iran wameuawa katika miripuko kadhaa iliyotokea katika mkoa wa Sistan na Baluchestan kusini mashariki mwa nchi.
-
Kundi la kigadi la Jaishu Dhulm lakiri kushambuliwa ngome zake Pakistan
Jan 17, 2024 04:35Kundi la kigaidi la Jaishu Dhulm limetangaza kuwa ngome zake zimelengwa na kushambuliwa kwa makombora usiku wa kuamkia leo katika mpaka wa Iran na Pakistan.
-
Raisi: Hujuma za Marekani dhidi ya Yemen zimefichua dhati yake ya shari
Jan 15, 2024 04:35Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen na kusema kuwa, hujuma hizo zimefichua dhati ya Washington ya kupenda shari, chokochoko na kukanyaga haki za binadamu.
-
Hatua za undumakuwili za nchi za Ulaya kuhusu ugaidi
Jan 13, 2024 23:13Mahakama ya Rufaa ya Denmark inayojulikana kwa jina la "The Eastern High Court" Ijumaa tarehe 12 Januari ilipasisha hukumu ya kifungo jela kwa watu watatu ambao ni wanachama wa kundi linalotaka kujitenga la "Al Ahwaziya" ambao walituhumiwa kueneza ugaidi nchini na kukusanya taarifa za kijasusi kwa ajii ya Shirika la ujasusi la Saudi Arabia.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran azungumza na mawaziri wenzake wa Saudia na Norway kuhusu Gaza
Jan 12, 2024 04:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia na Norway kuhusiana na kupanua uhusiano wa pande mbili na matukio yanayojiri katika Ukanda wa Gaza.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran lakamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama
Jan 11, 2024 12:06Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuikamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama katika Bahari ya Oman.
-
Kufichuliwa nafasi ya jasusi wa Uholanzi katika hujumu dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran
Jan 10, 2024 02:34Gazeti la Volkskrant la Uholanzi limefichua kuwa, raia mmoja wa nchi hiyo alikuwa na mchango mkubwa katika operesheni ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuhujumu kituo cha kurutubisha uranium cha Natanz nchini Iran.