• Wizara ya Ulinzi ya Iran: Tutaendelea kuunga mkono muqawama wa Palestina

    Wizara ya Ulinzi ya Iran: Tutaendelea kuunga mkono muqawama wa Palestina

    May 23, 2020 05:45

    Wizara ya Ulinzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema itaendelea kuziunga mkono na kuzipa misaada isiyo na kikomo harakati za muqawama za Palestina zinazopambana na utawala wa Kizayuni wa Israel.

  • Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; jitihada zisizo na tija za utawala wa Trump

    Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; jitihada zisizo na tija za utawala wa Trump

    May 23, 2020 02:45

    Baada ya kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran mnamo Mei 2018, serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani imekuwa ikitekeleza mashinikizo ya juu kabisa kwa kuiwekea Iran vikwazo shadidi zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia. Pamoja na kuwa vikwazo hivyo havijaweza kufanikiwa, Marekani inasisitiza kuendelea na sera yake hiyo ya vikwazo.

  • Jihadul Islami: Iran inahimili vikwazo vya kila namna kwa ajili ya kuihami Palestina

    Jihadul Islami: Iran inahimili vikwazo vya kila namna kwa ajili ya kuihami Palestina

    May 22, 2020 22:06

    Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amegusia maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds yaliyofanyika jana Ijumaa kote duniani na kukumbusha kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imejikubalisha kuhimili na kuvumilia mashinikizo na vikwazo vya kila namna vya mabeberu kwa ajili ya kuhami malengo matukufu ya Palestina.

  • Russia na Venezuela zakosoa hatua zisizo za kisheria za Marekani

    Russia na Venezuela zakosoa hatua zisizo za kisheria za Marekani

    May 22, 2020 02:00

    Tangu Rais Donald Trump mwenye kashfa nyingi wa Marekani aingie ikulu ya White House ameshadidisha siasa za uhasama dhidi ya Venezuela ambapo pia amefanya njama nyingi za kuiondoa madarakani serikali halali ya Rais Nicolás Maduro wa nchi hiyo sambamba na kuiwekea vikwazo vikali.

  • Sisitizo la Russia juu ya kutoweza Marekani kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran

    Sisitizo la Russia juu ya kutoweza Marekani kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran

    May 19, 2020 02:52

    Tarehe 8 Mei 2018, Marekani ilijitoa kijeuri katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA, lakini hivi sasa inafanya njama kubwa za kujaribu kuzuia utekelezaji wa makubaliano hayo hasa kipengee cha kuondolewa Iran vikwazo vya silaha kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hapo tarehe 18 Oktoba mwaka huu wa 2020. Hata hivyo wajumbe wa Mashariki wa kundi la 4+1 yaani Russia na China wamepinga vikali njama hizo za Marekani.

  • Kamati ya Bunge la Iran yaidhinisha muswada dhidi ya utawala wa Kizayuni

    Kamati ya Bunge la Iran yaidhinisha muswada dhidi ya utawala wa Kizayuni

    May 18, 2020 05:30

    Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni katika Majlisi ya Ushauri ya Kiisalmu (Bunge la Iran) imeidhinisha muswada wa namna ambavyo Iran itakabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika upeo wa kitaifa na kimataifa.

  • Ombi la Umoja wa Mataifa kuhusu kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran

    Ombi la Umoja wa Mataifa kuhusu kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran

    May 17, 2020 02:17

    Baada ya serikali ya Rais Donald Trump kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mwaka 2018 katika fremu ya sera za mashinikizo ya juu kabisa na kisha kushadidisha vikwazo ambavyo havijawahi kushuhudiwa katika historia dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na licha ya kuibuka ugonjwa wa COVID-19 nchini Iran, lakini bado Trump anasisitiza kuendeleza vikwazo vyake vilivyo dhidi ya ubinadamu dhidi ya taifa hili.

  • Marekani ya Trump; nembo na mshirika wa ugaidi wa kiserikali ulimwenguni

    Marekani ya Trump; nembo na mshirika wa ugaidi wa kiserikali ulimwenguni

    May 15, 2020 21:58

    Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani ni nembo ya ugaidi wa kiserikali na kueleza kwamba, historia ya nchi hiyo katika kuunga mkono ugaidi iko wazi kabisa.

  • Waliopona ugonjwa wa COVID-19 nchini Iran wakaribia 92,000

    Waliopona ugonjwa wa COVID-19 nchini Iran wakaribia 92,000

    May 15, 2020 08:02

    Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma na Upashaji Habari ya Wizara ya Afya ya Iran ametangaza kuwa, hadi hivi sasa waathiriwa zaidi ya 91,836 wa ugonjwa wa COVID-19 au corona humu nchini wamepata afueni na kuruhusiwa kurejea nyumbani kutoka mahospitalini.

  • Sayyid Hassan Nasrallah atetea msimamo wa Iran kuhusu mgogoro wa Syria

    Sayyid Hassan Nasrallah atetea msimamo wa Iran kuhusu mgogoro wa Syria

    May 15, 2020 03:03

    Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ametoa hotuba yenye kukosoa vikali sera za Marekani na utawala Israel kuhusu misimamo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mgogoro wa Syria.