-
IRGC: Uhusiano wa kina kati ya serikali, wananchi na vikosi vya ulinzi ni dhamana ya Iran yenye nguvu
Aug 24, 2025 07:25Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) limeashiria umuhimu wa uhusiano wa kina uliopo kati ya serikali, taifa na vikosi vya ulinzi likiutaja kuwa muhimu kwa ajili ya kuwa na nchi yenye nguvu na iliyoendelea. Jeshi la IRGC aidha limesisitiza dhamira yake ya kuimarisha uwezo wa kiulinzi na usalama kwa kuzingatia vitisho vilivyopo.
-
Iran: Tutatumia zana mpya iwapo adui ataanzisha tena uchokozi
Aug 23, 2025 03:33Waziri wa Ulinzi wa Iran, Brigedia Jenerali Aziz Nasirzadeh amesisitiza kuwa, iwapo maadui watafanya uchokozi mwingine dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, bila shaka majeshi ya nchi hii yatatumia vifaa, silaha na zana za kijeshi ambazo hazijawahi kutumiwa kufikia sasa.
-
Iran yaionya Ulaya juu ya matokeo mabaya ya kuamilisha 'snapback'
Aug 23, 2025 02:46Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi ameionya Ulaya juu ya matokeo mabaya ya kuamilisha "utaratibu wa snapback", akisisitiza kwamba Troika ya Ulaya (Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani) pamoja na Umoja wa Ulaya hazina haki ya kisheria na ya kimaadili ya kutumia utaratibu huo.
-
Mkuu wa Jeshi: Iran itatoa 'jibu kali la kusagasaga zaidi' kwa uchokozi wowote mpya wa adui
Aug 22, 2025 08:20Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu Iran Meja Jenerali Amir Hatami amesisitiza kuwa Vikosi vya Ulinzi vimejiweka tayari kutoa jibu kwa wavamizi ambalo ni la "kusagasaga zaidi" kuliko lile lililoonekana wakati wa uchokozi uliofanywa na utawala haramu wa kizayuni wa Israel na Marekani dhidi ya taifa hili.
-
Pezeshkian: Iran, Belarus zimesimama kidete kukabiliana na ubeberu wa US
Aug 20, 2025 09:03Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema Marekani na baadhi ya washirika wake wa Magharibi wanalenga kupanua ubeberu na msimamo wa upande mmoja duniani kote, sambamba na kuyaburuza mataifa mengine, akisisitiza kwamba si Iran wala Belarus itavumilia muenendo huo.
-
Komandi ya jeshi ya ngazi ya juu ya Iran: Vikosi vya ulinzi viko tayari kuzima vitisho vyovyote
Aug 20, 2025 08:43Kamandi ya jeshi ya ngazi ya juu ya Iran imesisitiza utayarifu kamili wa jeshi la nchi hii katika kupambana na vitendo vyovyote vya uchokozi vinavyoweza kufanywa na maadui dhidi ya ardhi ya Iran.
-
Iran na Armenia zatia saini hati 10 za maelewano wakati wa ziara muhimu ya Pezeshkian
Aug 19, 2025 08:06Iran na Armenia zimetia saini hati 10 za maelewano kuhusu ushirikiano wa nchi hizo katika nyanja zote wakati wa ziara muhimu ya kiserikali ya Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huko Armenia. Lengo la ziara hiyo limetajwa kuwa ni kuimarisha uhusiano kati ya nchi mbili.
-
Ripota wa UN: HAMAS ni taasisi ya kisiasa iliyochaguliwa kupitia uchaguzi, si genge la wauaji
Aug 19, 2025 03:05Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, amesisitiza kwamba Hamas inapasa itambuliwe kama harakati halali ya kisiasa badala ya kundi la wauaji.
-
Naibu kamanda wa IRGC: Israel ilikwenda kombo katika hesabu zake katika vita vya siku 12 dhidi ya Iran
Aug 18, 2025 23:27Naibu Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa Israel ilifanya mahesabu ghalati katika vita vya sku 12 ilivyovianzisha dhidi ya Iran licha ya kwamba utawala huo ulitumia nguvu kamili dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yaonya: Israel itajitanua zaidi Asia Magharibi iwapo haitadhibitiwa
Aug 18, 2025 07:34Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei amesema Israel ni tishio kwa usalama na uthabiti wa Asia Magharibi kutokana na mwenendo wake wake kupenda kujitanua, akionya kuwa eneo hili la kistratejia linaweza kukabiliwa na vita visivyoisha ikiwa utawala huo hautazuiwa.