-
Nujaba kwa maadui wa Iran: Vita vinaweza kufika milangoni kwenu
Jan 29, 2026 06:27Katibu Mkuu wa kundi la kupambana na ugaidi la Harakat al-Nujaba la Iraq amewaonya vikali maadui wa Iran kuhusu matokeo mabaya ya uchokozi wowote mpya ambao wanaweza kufanya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Trump atishia kuikatia misaada Iraq endapo Nouri al-Maliki atakuwa Waziri Mkuu
Jan 28, 2026 10:28Rais wa Marekani Donald Trump amedai katika ujumbe unaoakisi uingiliaji wa wazi wa masuala ya ndani ya Iraq kwamba Nouri al-Maliki hapasi kuwa waziri mkuu, kwa sababu kama atachaguliwa kushika wadhifa huo, Marekani haitatoa tena misaada kwa nchi hiyo.
-
Kata'ib Hizbullah yatoa wito kwa wanamuqawama kujiandaa kwa 'vita' ili kuinga mkono Iran
Jan 26, 2026 06:36Harakati ya Kata’ib Hizbullah ya Iraq (Brigedi za Hizbullah) imetangaza kuwa iko tayari kushiriki katika vita vyovyote vitakavyotokea ili kuilinda Iran, ikitoa wito kwa wanamapambano duniani kote kujiandaa kwa ajili ya hilo.
-
Wairaqi waunga mkono Hizbullah na Ansarullah baada ya tangazo la kuzuiliwa mali zao kimakosa
Dec 05, 2025 07:51Mitaa ya mji mkuu wa Iraq, Baghdad usiku wa kuamkia leo ilishuhudia misafara mirefu ya magari, yaliyokuwa yakipeperusha bendera za harakati za Muqawama wa Kiislamu za Hizbullah ya Lebanon na Ansarullah ya Yemen, na kutangaza mshikamano wa umma na harakati hizo za Muqawama dhidi ya vitisho vya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Al-Sudani asema, ataanza kufanya mazungumzo ya kuunda serikali mpya ya Iraq
Nov 13, 2025 12:25Waziri Mkuu wa Iraq Mohammad Shia al-Sudani amesema, ataanza kufanya mazungumzo hivi karibuni kwa ajili ya kuunda serikali mpya wakati muungano wake unaonekana kuongoza katika uchaguzi wa bunge.
-
Katibu Mkuu wa UN apongeza uchaguzi wa bunge Iraq, ahimiza kuundwa serikali kwa njia ya amani
Nov 12, 2025 11:12Wakati zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi wa Bunge la Iraq lingali linaendelea, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wananchi wa nchi hiyo kwa ushiriki wao katika uchaguzi huo na kuipongeza pia Tume Huru ya Uchaguzi (IHEC) kwa kuendelesha zoezi hilo kwa ufanisi.
-
Madai yasiyo na msingi ya Trump ya eti ushindi wa Marekani katika vita vyote; ni kujisahaulisha matukio ya Afghanistan na Iraq?
Oct 31, 2025 03:13Rais wa Marekani, Donald Trump, amedai kwamba nchi hiyo itashinda kama itaingia vitani na nchi yoyote.
-
Kwa nini Marekani inashinikiza kupokonywa silaha makundi ya muqawama ya Iraq?
Oct 23, 2025 07:53Tommy Piggott, Naibu Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani alisema siku ya Jumanne kwamba Marco Rubio Waziri wa Mambo ya Nje, katika mazungumzo yake na Mohammad Shia Al-Sudani, Waziri Mkuu wa Iraq, ametoa wito wa kupokonywa silaha makundi ya muqawama ya nchi hiyo akidai kuwa ni tishio kwa maslahi ya Washington na Baghdad.
-
Iraq: Hatutaruhusu ardhi na anga yetu zitumike kutishia usalama wa Iran, majirani wengine
Oct 21, 2025 07:01Iraq iimesisitiza kuwa haitaruhusu ardhi na anga yake zitumike kutishia usalama wa Iran au wa nchi nyingine yoyote jirani.
-
Jinai za Marekani wakati wa uvamizi wa Iraq
Oct 02, 2025 08:26Jinai za Marekani wakati wa kuikalia kwa mabavu Iraq zilikuwa kubwa na mfano mchungu sana wa mauaji na uharibifu chini humo ambazo wavamizi wa Kimarekani walijaribu na hadi sasa wanaendelea kujaribu kuzihalalisha kwa majina tofauti ya udanganyifu.