-
Rais Ebrahim Raisi: Nchi za Asia Magharibi zinaweza kubuni ramani ya njia ya amani bila ya kutegemea madola ya kigeni
Aug 17, 2021 15:56Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa nchi za eneo la Magharibi mwa Asia zinaweza kubuni ramani ya njia na kuimarisha amani, utulivu na usalama endelevu kwa kushirikiana, na kuongeza kuwa uingiliaji wa madola ya kigeni katika masuala ya eneo hilo hauwezi kudhamini amani, ustawi na maendeleo.
-
Rais Assad wa Syria aalikwa kuhudhuria kikao cha Baghdad cha viongozi wa nchi za eneo
Aug 16, 2021 12:34Duru za habari zimeripoti kuwa serikali ya Iraq imemwalika rais wa Syria kushiriki katika kikao cha viongozi wa nchi jirani na Iraq kitakachofanyika mjini Baghdad.
-
Malengo ya Iraq katika kuandaa kikao cha nchi jirani
Aug 12, 2021 02:25Serikali ya Iraq inafanya juhudi za kuandaa kikao cha viongozi wa nchi za eneo na nchi kadhaa za kimataifa kufikia mwishoni mwa mwezi huu wa Agosti.
-
Asa'ib Ahl al-Haq ya Iraq: Tuna haki ya kujibu mashambulio ya Israel
Aug 11, 2021 03:47Katibu Mkuu wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ya nchini Iraq amesema kambi hiyo ya muqawama ina haki ya kujibu mapigo, kufuatia mashambulio ya utawala wa Kizayuni wa Israel ambayo yameua vijana kadhaa wa mrengo huo wa mapambao ya Kiislamu.
-
Maroketi mawili yapiga karibu na ubalozi wa Marekani, Baghdad
Jul 30, 2021 02:20Ripoti zinasema kuwa maroketi mawili yamepiga eneo la karibu na ubalozi wa Marekani mjini Baghdad katika eneo lenye ulinzi mkubwa la Green Zone.
-
Radiamali tofauti za maafisa na makundi ya Iraq kuhusu taarifa ya pamoja ya al-Kadhimi na Biden
Jul 28, 2021 08:23Rais Joe Biden wa Marekani na Mustafa al-Kadhimi, Waziri Mkuu wa Iraq wametoa taarifa mwishoni mwa duru ya nne ya mazungumzo ya kistratijia nya nchi mbili ambapo wamesema kuwa wameafikiana juu ya kufikia kikomo uwepo wa askari wa Marekani katika ardhi ya Iraq ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
-
Russia yaitaka Marekani iwaondoe wanajeshi wake Iraq, Libya, Syria na Afghanistan
Jul 28, 2021 07:47Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ameitaka Marekani iwaondoe wanajeshi wake huko Iraq, Libya, Afghanistan na Syria.
-
HRW: Israel ilitenda jinai za kivita katika vita vya siku 11 dhidi ya Ukanda wa Gaza
Jul 28, 2021 01:32Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema mashambulio yaliyofanywa na jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika vita vya siku 11 dhidi ya Ukanda wa Gaza yalifikia kiwango cha jinai za kivita.
-
Makundi ya Mashia Iraq yakaribisha makubaliano ya kuondolewa askari wa Marekani nchini humo
Jul 27, 2021 15:08Mirengo miwili ya Al Fat-h na An-Nasr pamoja na harakati ya Hekima ya Kitaifa na ile ya Sadr nchini Iraq zimekaribisha juhudi za timu ya mazungumzo ya nchi hiyo zilizowezesha kufikiwa makubaliano na Marekani ya kuwaondoa askari wake katika ardhi ya Iraq.
-
Safari ya Al Kadhimi mjini Washington sambamba na duru ya nne ya mazungumzo baina ya Iraq na Marekani
Jul 26, 2021 07:53Duru ya nne ya mazungumzo kati ya Marekani na Iraq ilianza siku ya Ijumaa ya tarehe 23 Julai mjini Washington, Marekani. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq Fuad Hussein na Qassem Al Aa'raji, Mshauri wa Usalama wa Taifa ndio wanaoiwakilisha nchi yao katika mazungumzo hayo.