-
Papa Leo XIV : Uvamizi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran 'sio vita vya haki'
Jun 07, 2026 03:44Kiongozi wa kanisa katoliki Dunia, Papa Leo XIV amesema uchokozi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa "vita vya haki", akisisitiza kwamba itikadi hiyo ya karne nyingi haiendani na uhalisia wa vita vya kisasa.
-
WFP: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinasukuma mamilioni kukumbwa na njaa Afrika
Jun 06, 2026 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinawasukuma mamilioni ya watu duniani kuingia katika hali ya njaa huku bara Afrika likionekana kuathirika zaidi.
-
Foreign Policy: Chuki dhidi ya Wakristo imeongezeka huko Israel
Jun 04, 2026 03:12Uchunguzi uliofanywa na baadhi ya vyombo vya habari umebaini kuwa chuki na hujuma dhidi ya Wakristo vimeongezeka huko Israel.
-
Israel yafuta mpango wa kushambulia Beirut baada ya onyo kali la Iran
Jun 02, 2026 09:12Utawala wa Israel umeachana na mpango wake wa kufanya mashambulizi makali ya ya kijeshi dhidi ya mji mkuu wa Lebanon, Beirut. Haya yameelezwa siku ya Jumatatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia onyo kali kutoka kwa Iran kwamba haitavumilia wimbi jipya la uvamizi dhidi ya Beirut, hatua ambayo ingekiuka makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Marekani.
-
Mwanasiasa wa Ujerumani: EU ni mshirika katika ugaidi wa kimfumo wa Israel
Jun 01, 2026 02:55Mwanasiasa wa Ujerumani na mbunge wa zamani wa bunge la nchi hiyo amekosoa sera za utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema: "Walowezi wa Kizayuni wanafanya ugaidi wa kimfumo dhidi ya Wapalestina, na serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya wanashiriki katika uhalifu huo kwa kunyamaza kimya."
-
Waziri wa Israeli Ben-Gvir amhimiza Netanyahu 'kusawazisha vitongoji vya Beirut na ardhi'
May 31, 2026 12:48Waziri anayejiita wa usalama wa Israel, Itamar Ben-Gvir, amemtaka Waziri Mkuu wa utawaka huo katili, Benjamin Netanyahu, kusawazisha na ardhi vitongoji vya mji mkuu wa Lebanon, Beirut huku utawala huo ukizidisha mashambulizi yake dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iran yalaani ukiukaji wa Marekani wa makubaliano ya amani, yahimiza UN kuingilia kati
May 29, 2026 03:18Iran imelaani vikali vitisho vya mara kwa mara vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu na ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamisha vita haramu vya hivi karibun, ikiuhimiza Umoja wa Mataifa kuingilia kati.
-
Washington Post: Israel imetengwa duniani kutokana na vita vya mara kwa mara vya Netanyahu
May 29, 2026 02:57Gazeti la Washington Post limeandika kuwa: Vita vya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Lebanon, Syria, Iran na Yemen vimeiweka Israel katika njia ya mmomonyoko wa kijeshi, kushindwa kimkakati na kutengwa kimataifa.
-
Viwango vya Undumakuwili wa Ulaya; Kwa Nini Jinai za Israel Zinanyamaziwa Kimya?
May 22, 2026 15:20Hatua ya utawala wa Kizayuni ya kukamata meli 50 zilizokuwa zimebeba wanaharakati 428 wa haki za binadamu na misaada ya kibinadamu kutoka nchi 44 kwa ajili ya Wapalestina wanaozingirwa na utawala huo huko Gaza katika bahari ya Mediterania imeibua wimbi la hasira na chuki dhidi ya Wazayuni.
-
Picha za satalaiti zaonyesha uharibifu mkubwa kwenye kambi za kijeshi za Israel kutokana na mashambulizi ya Iran
May 22, 2026 14:53Picha mpya za satalaiti zilizochambuliwa zimefichua uharibifu na hasara kubwa iliyotokea katika vituo vingi vya kijeshi vya Israel kufuatia mashambulizi na operesheni za kujihami za Iran na harakati ya Lebanon Hizbullah na hivyo kuzusha maswali kuhusu ukubwa wa uharibifu ambao Tel Aviv inauficha mbele ya umma.