-
Licha ya vizuizi vikali vya Israel, Wapalestina laki moja wasali I'sha na Tarawehe Masjidul-Aqsa
Feb 21, 2026 11:07Licha ya vizuizi vikali vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa, makumi ya maelfu ya Wapalestina jana usiku walihudhuria katika msikiti huo mtukufu kusali Sala za I'sha na Tarawehe wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Waholanzi 640 waliohudumu katika jeshi la Israel Gaza kushtakiwa?
Feb 20, 2026 03:26Zaidi ya raia 640 wa Uholanzi wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Gaza na kwneye mashambulizi dhidi ya Ukingo wa Magharibi, takwimu mpya zinaonyesha, huku wataalamu wa sheria wakionya kwamba, wale waliohusika wanaweza kushtakiwa chini ya sheria za kimataifa na za nchi hiyo za uhalifu wa kivita.
-
Kwa kuwadia Ramadhani, mlowezi wa kizayuni auchoma moto Msahafu Baitul-Muqaddas
Feb 18, 2026 10:30Mlowezi mmoja Muisraeli wa kizayuni mwenye misimamo ya chuki ameichoma moto nakala ya Kitabu kitakatifu cha Waislamu, Qur'ani, akiwa katika eneo ambalo halijafahamika katika mji wa Baitul-Muqaddas, siku chache kabla ya kuanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Israel yashadidisha mateso kwa Wapalestina inaowashikilia kwenye magereza yake
Feb 18, 2026 03:03Jumuiya ya Wafungwa wa Palestina imetangaza kuwa, kwa mujibu wa ziara za ukaguzi zilizofanywa na wanasheria wake na ushuhuda uliorekodiwa, utawala wa kizayuni wa Israel umeshadidisha udhalilishaji na ushinikizaji wa kimfumo dhidi ya wafungwa Wapalestina unaowashikilia katika magereza yake ya kuogofya.
-
Wakenya: Mradi wa kilimo wa Israel Nakuru ni mwanzo wa unyakuzi wa ardhi zetu
Feb 17, 2026 06:22Mradi wa Israel wa kilimo na makazi wa ekari 520 huko Solai, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya umezua mjadala mkali wa kitaifa. Wakenya wametumia mitandao ya kijamii kupinga mradi huo, wanaotaja kuwa mwanzo wa unyakuzi wa ardhi za nchi hiyo na utawala ghasibu wa Israel.
-
"Ni muhali kufikia amani na Israel madhali inakiuka haki za Wapalestina"
Feb 16, 2026 10:17Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji wa Palestina, Varsen Aghabekian Shahin amesema kufikia amani na Israel "haiyumkiniki" madhali haki za Wapalestina zinakiukwa na utawala huo wa Kizayuni, akisisitiza kwamba sheria za kimataifa zinapasa kuzingatiwa, na uchukuaji wa hatua za upande mmoja lazima ukomeshwe.
-
Je, China ina msimamo gani kuhusu hatua mpya za utawala wa Israel katika Ukingo wa Magharibi?
Feb 16, 2026 03:35China sambamba na kuashiria kuidhinishwa kanuni mpya na baraza la mawaziri la usalama la Israel ili kuimarisha udhibiti wa Ukingo wa Magharibi, imeonya kuhusu matokeo mabaya ya hatua hiyo.
-
Israel yakasirishwa na kauli ya kumdhalilisha rais wake iliyotolewa na Trump
Feb 15, 2026 03:26Duru zilizo karibu na rais wa utawala wa kizayuni wa Israel zimeyaelezea matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kumtusi na kumdhalilisha rais wa utawala huo Isaac Herzog kuwa ni uvukaji mistari myekundu.
-
Umoja wa Afrika: Mateso dhidi ya Wapalestina lazima yakomeshwe
Feb 15, 2026 02:50Mahmoud Ali Youssouf Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) amesema kuwa, mauaji dhidi ya wananchi wa Palestina ni lazima yakomeshwe. Mahmoud Ali Youssouf alisema hayo jana (Jumamosi) wakati akiufungua mkutano wa kilele wa 39 wa umoja huo.
-
Zaidi ya raia 2,000 wa UK wamepigana kwa niaba ya Israel katika mauaji ya halaiki Gaza
Feb 13, 2026 02:02Maelfu ya raia wa Uingereza wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.