-
Taasisi ya EU yapiga kura ya kutaka kususiwa Vyuo Vikuu vya Israel
Nov 23, 2018 04:32Taasisi moja ya akademia ya Umoja wa Ulaya imepasisha kwa wingi wa kura muswada wa kutaka kususiwa Vyuo Vikuu na taasisi nyingine za elimu ya juu za utawala haramu wa Israel ambazo ziko katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Ripoti: 70% ya kauli za viongozi wa Israel wakiongozwa na Netanyahu, ni porojo
Nov 20, 2018 04:31Utafiti mpya umefichua kuwa, zaidi ya asilimia 70 ya matamshi yanayotolewa na wanasiasa wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni urongo, porojo na propaganda, huku Waziri Mkuu wa utawala huo pandikizi, Benjamin Netanyahu akiongoza katika orodha hiyo.
-
Abdollahian: Muqawama wa Wapalestina umewavunja moyo Wazayuni
Nov 19, 2018 00:45Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amesema Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu yuko katika ncha ya kuanguka, na kwamba muqawama wa Wapalestina umewavunja moyo Wazayuni.
-
Ayatullah Kashani: Wanaounga mkono jinai za Saudia na Wazayuni wana sura za kuogofya
Nov 16, 2018 11:27Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, nchi ambazo zinazipa himaya na kuunga mkono jinai zinazofanywa na Saudi Arabia na utawala wa Kizayuni wa Israel ndizo nchi zenye sura za kutisha zaidi duniani.
-
Duru za habari: Baada ya Lieberman, Waziri wa Uhajiri wa Israel naye pia amejiuzulu
Nov 15, 2018 03:48Vyombo vya habari vimeripoti kuwa waziri mwengine katika serikali ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, amejiuzulu.
-
Makubaliano ya usitishaji vita yamfanya Waziri wa Vita wa Israel ajiuzulu
Nov 14, 2018 11:05Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Avigdor Liberman ametangaza kujiuzulu wadhifa wake eti kulalamikia hatua ya harakati za mapambano za Palestina ikiwemo Hamas kufikia makubaliano ya kusitisha vita na utawala huo dhalimu katika Ukanda wa Gaza kupitia upatanishi wa Misri.
-
Wanamapambano wa Palestina wajibu mapigo, vituo vya Wazayuni vyamiminiwa makombora
Nov 13, 2018 23:07Harakati za mapambano za Palestina alfajiri ya Jumatatu zilijibu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuvishambulia kwa makombora vitongoji zaidi ya 50 vya walowezi wa Kizayuni na vituo kadhaa vya askari wa Israel.
-
Saudia inanunua kwa siri silaha za Israel katika fremu ya 'Muamala wa Karne'
Nov 11, 2018 04:38Vyombo vya habari vya Kiarabu vimefichua kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umeiuzia Saudia Arabia vifaru vya kivita 500 aina ya Merkava vilivyoundwa katika viwanda vya utawala huo. Ununuzi huo wa siri umetajwa kuwa mkubwa zaidi kuwahi kufanyika baina ya Saudi Arabia na utawala wa Kizayuni.
-
"Saudia ilitumia programu ya udukuzi ya Israel kumfuatilia Kashoggi"
Nov 08, 2018 11:49Edward Snowden, afisa wa zamani wa Shirika la Usalama wa Taifa la Marekani (NSA) amefichua nafasi ya utawala haramu wa Israel katika mauaji ya kikatili ya mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi yaliyofanywa na Riyadh nchini Uturuki mwezi uliopita.
-
Viongozi wa Kikristo mjini Quds wakosoa ubaguzi wa Netanyahu
Nov 06, 2018 04:30Wakuu wa Kanisa Katoliki katika mji wa Quds tukufu unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel wamemuandikia barua Waziri Mkuu wa utawala huo ghasibu wakikosoa misimamo yake ya kibaguzi.