-
CAIR: UN ichunguze jeshi la Israel lilivyowaua Wapalestina bila sababu na kuzifukia maiti zao
Mar 28, 2024 06:39Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani [CAIR] limetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuchunguza video inayoonyesha wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wakiwapiga risasi bila sababuu Wapalestina wawili wanaoonekana kuwa hawana silaha kisha kuzifukia maiti zao kwa buldoza.
-
Haniya: Azimio la Baraza la Usalama linaonesha Israel imetengwa duniani
Mar 27, 2024 04:10Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema utawala wa Kizayuni wa Israel umetengwa vibaya na dunia kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa; siku moja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupasisha azimio la kutaka kusitishwa mara moja mapigano huko Gaza.
-
Yemen yafanya mashambulizi 6 dhidi ya US, UK na Israel
Mar 27, 2024 04:09Vikosi vya Jeshi la Yemen vimefanya mashambulizi sita dhidi ya meli za Marekani, Uingereza na utawala haramu wa Israel, ukiwa ni muendelezo wa operesheni za kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kujibu uvamizi wa Washington na London dhidi ya Yemen.
-
Soda ya 'Palestine Cola' yazinduliwa, mashirika ya Magharibi yaendelea kususiwa
Mar 26, 2024 22:38Ndugu wawili wa Kipalestina wamezindua soda waliyoipa jina la 'Palestine Cola' na kusema kuwa, faida zote zitakazotokana na mauzo ya kinywaji hicho zitawaendea Wapalestina.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani Israel kuzuia malori ya misaada yasiingie Ghaza, 7,000 yamepanga safu Misri
Mar 24, 2024 03:33Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani kuzuiwa kwa malori ya misaada yaliyoko katika upande wa Misri wa mpaka na Ukanda wa Ghaza, akiielezea hatua hiyo kuwa inasababisha "ghadhabu ya kimaadili."
-
Muqawama wa Iraq: Tumeshambulia kwa droni makao makuu ya wizara ya masuala ya kijeshi ya Israel
Mar 24, 2024 03:06Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Iraq imetangaza kuwa imeshambulia makao makuu ya wizara ya masuala ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kutumia ndege isiyo na rubani mapema leo Jumapili.
-
Bajeti ya muda ya US yaidhinisha msaada wa kijeshi kwa Israel, yazuia ufadhili kwa UNRWA
Mar 24, 2024 03:06Bunge la Marekani limepitisha pendekezo la bajeti ya muda ambayo imeidhinisha msaada mpya wa kijeshi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusitisha ufadhili kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) hadi Machi 2025.
-
Israel yapora ekari 2,000 za ardhi ya Wapalestina Ukingo wa Magharibi
Mar 23, 2024 04:10Utawala ghasibu wa Israel umetangaza habari ya kunyakua ekari karibu 2,000 (hektari 800) za ardhi ya Palestina katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu na utawala huo haramu.
-
Hizbullah yajibu mapigo, yapiga ngome za Israel kwa droni na mizinga
Mar 23, 2024 04:06Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imejibu jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza kwa kupiga ngome na kambi za kijeshi za Wazayuni kaskazini mwa ardhi za Palestina zilizopachikwa jina bandia la Israel, kwa makombora ya mizinga na ndege zisizo na rubani (droni).
-
Bandari ya Israel kuwatimua nusu ya wafanyakazi kutokana na hujuma za Yemen
Mar 22, 2024 07:25Asilimia 50 ya wafanyakazi katika bandari ya Eilat ya utawala wa Kizayuni wa Israel wapo hatari ya kupigwa kalamu nyekundu kutokana na athari za mashambulizi ya vikosi vya Yemen katika Bandari Nyekundu.